Tofauti kati ya IT na ICT

Hapo awali kulikuwa na ulimwengu tofauti wa Computer na Mawasiliano,  Ulimwengu wa computer ulitumia njia zake ndani ya njia za mawasiliano, na haukufananishwa sana na mawasiliano kwa sababu  tulitumia computer kufanya mambo makubwa sana na kidgo sana kuwasiliana na hiyo ni kutokana na kutokuwa na urahisi wa kupata na kutumia computer ndio maana ulikuwa umejiweka tofauti...(SImu zote za smartphone ni computer hizo, kama laptop na desktops)
Sasa tunavyozidi kwenda mbele computer zimekuwa gharama nafuu na ndio zimekuwa njia kuu za mawasiliano, na ndio maana kwa ufupi tunaondoka katika kuita tuu IT(information technology) na kuita ICT(information Communication Technology)

Angalizo.
Natumia lugha nyepesi ili kila mtu aelewe, kuna vitu vingi vya kitaalamu nitaviacha.

IT(INFORMATION TECHNOLOGY)
Huu ni ulimwengu wa computer ambao kwa sasa una maanisha mifumo ya computer inayoendesha biashara, taasisi, mabenki n.k lakini unajumuisha fani mbali mbali kama systems administrator, programming, system analysis, computer science, database administration n.k..

ICT(Information Communication Technology)
Huu ni uwanda wa IT lakni ambao umeongezewa mawasiliano ndani yake. Hapo awali kulikuwa na field iliyokuwa inaitwa Telecommunication ambayo ilikuwa inajikita katika njia za mawasiliano. Mfano hawa watu unawaona wana deal na minara ya simu, nyaya huwa tunawaita telecommunication engineers lakni katika IT kuna watu hao wanadili na Network ila wao tunawaita Network engineers.

Kufupisha zaidi ICT ni pana zaidi na inajumisha field yote IT pamoja na njia za mawasiliano.

Ila ieleweke watu wa telecomunications ni tofauti kabisa na watu wa IT hata wanavyosema na kazi zao hawawezi kubadilishana.

Pia term ya ICT inatumika tuu katika kutoa Elimu ya IT na mawasiliano lakini katika kikazi zaidi tunatumia IT.
Unaweza soma kozi ya bachelor of science in ICT, lakni ukimaliza usije ukajiita wewe ni ICT professional utatia aibu, wewe katika field wewe ni IT professional.

Kwa hiyo hili wimbi la ma Vyuo kubadili majina ya course kutoka IT kwenda ICT lisikutishe, ujue tuu hiyo term ya ICT inatumika zaidi katika Elimu, ila ukimaliza wewe ni IT kama kawaida.



Kwa Maelezo zaidi wasiliana nami kupitia elisanteshibanda@yahoo.com. au jiunge la MAXPO Tanzania ukutane na wataalamu wengine wa IT.


 


Ninachopenda kuhusu IT na fani hii kwa ujumla ni jinsi ilivyo na uwezo kumpa mtu yeyote fursa ya kufanikiwa na jinsi ilivyounganisha dunia nzima.
katika miaka ya karibuni Watu na makampuni mashuhuri makubwa yamekuwa yakija Africa na Asia na hata Ulaya pia kufanya mashindano ya kutafuta watu wenye mawazo makubwa yanayoweza kugeuka biashara kubwa na pia kutatua changamoto duniani, yote katika fani ya teknolojia.

Vigezo

  • Uwe na biashara/kampuni ya IT, yenye wazo zuri ambalo limeshaanza kufanya kazi, na maanisha kama una software uwe umshatengeneza atlleast linaonekana au kama ni tech nyingine basi umeshaanza ku operate na watu wameipokea ila hauna uwezo wa kukua kibiashara.

  • Usiwe peke yako tuu, kuanzia wawili au watatu(Tech IT, Business, Administration)

  • Uwe na uwezo mzuri wa kujieleza kiingereza kwa maaana utakutana na watu kutoka mataifa yote duniani.

  • Uwe na ujasiri wakusimama mbele za watu wengi na kutetea wazo lako.

  • Hakikisha wazo lako liwe kweli linatatua changamoto ambayo inaikabili jamii, iili watu wakimbilie kununua solution yako haraka.

Mashindano hayo ni kama yafuatayo, yabonyeze vichwa vyake vya habari kujua zaidi...

MEST AFRICA CHALLENGE



START UP WORLD CUP



NETPRENEUR PRIZE



PROPTECH INNOVATION AWARD







START PRIZE



START UP ENERGY TRANSITION AWARD


 
Watanzania waliowahi kushinda mashindano haya ni


Wengine tumeshiriki ila hatukufanikiwa (MEST AFRICA) safari bado inaendelea, ila kuna wengine wengi zaidi wameshinda ila sina taarifa zao kama wewe umeshawahi kushiriki naomba unitafute tuongeze maelezo zaidi ili wengi wapate mwanga zaidi.



 



CERTIFICATIONS  CERTIFICATIONS CERTIFICATIONS

Sijui niseme ni ubaya au uzuri Ukimaliza kusoma IT au computer science au computer engineering ndgu safari yankupata ajira itakuwa ngumu sana kwako unahitaji kwenda kusoma tena vyeti vya ujuzi maalumu ili uonekane umebobea wapi.

NI gharama ila ukitaka kazi haraka basi nenda kasome hivyo vyeti yaani utapata kazi haraka sana.


Cisco Certified Network Professional (CCNP)

The Cisco Certified Network Associate (CCNA) certification hii inatoa  specializations katika  security, wireless, routing and switching, industrial, IoT, data center, cyber operations, collaboration and cloud.

kama unataka kazi yeyote ya system administration kama huna hichi cheti sahau kupata kazi...nenda University of Dar es salaam computing centre wanatoa.

Oracle Certified MySQL Database Administrator (CMDBA)

kama unahitaji kuhudumia systems za database bado haswa katika kazi ya system administration unahitaji sana hichi cheti, na  ni kama dhahabu maana hakuna program inayo run bila database. 

Certified Information Systems Security Professional (CISSP)

Security sasa hivi ni issue moja kubwa sana kwa makampuni mengi maana wizi ni mwingi sana, unahitaji hichi cheti ili uwe vizuri katika kulinda systems za organization, na katika certifications za muhimu kabisa hichi ni bora uanze nacho.

Microsoft Certified Solutions Associate (MCSA)

Certifications hizi zinakusaidia kuweza kuoperate na ku maintain server infrastructure za office, Servers kama kompyuta nyingine huwa zinapata changamoto nyingi unaposomea haya mambo unakuwa fundi kabisa tena certified kabisa.

Certified Data Professional (CDP)

Ulimwengu unapoelekea sasa hivi unaendeshwa na data. Certfications kama hizi zintakuweka katika ramani ya makampuni ya mawasiliano, kamali yaani yote yanayodeal na big data.

Kwa maswali zaidi wasiliana nami kupitia elisanteshibanda@yahoo.com

 


Ninavyozungumzia Information technology course najumuisha computer science, computer engineering, Software engineering etc.
Sasa zingatia vigezo vifuatavyo kwa ngazi tofauti.

CHETI


Utahitaji cheti cha form four (CSEE) chenye kuanzia pass 4 (Ukiondoa masomo ya dini)


au 
     

Utahitaji  cheti cha National vocational training award level 3.


au


Kwa kwenda kusoma business Informational technology unaweza ukapeleka hata National Business certificate stage 1 kikiwa na pass 2.




DIPLOMA

Utahitaji cheti cha advanced Certificate of Secondary Education(ACSE) ukiwa na principal pass 1 na subsidiary pass 1


au

Basic Technician Certificate (NTA Level 4) katika kozi za certificate in computer science, IT, Business IT, Computer Engineering na Electrical Engineering.


DEGREE

Utahitaji cheti cha advanced Certificate of Secondary Education(ACSE) ukiwa na principal pass 2 ambayo mojawapo lazima iwe Advanced Mathematics 

au 

ufaulu wa pass katika masomo yeyote mawili ya sayansi na Advanced Mathematics uwe na ufaulu wa subsidiary pass.

au 

Uwe na ufaulu wa GPA zaidi ya 3.0 katika ngazi ya Diploma.


Kwa maelezo zaidi wasiliana na uongozi wa vyuo vinavyotoa IT kwa kutembelea tovuti zao. Kila la kheri.

Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na magroup ya Whatsapp ya MAXPO Tanzania  Maximize your potential 





Fahamu kozi za IT zinazotolewa kwa sasa Tanzania.

Misamiati muhimu:

Self employing - unaweza kujiajiri

Marketable - Ajira nyingi

Less marketable - Ajira chache

Poorly marketable - Ajira hakuna


Kozi za degree.

Business Information system - Marketable

Computer and information systems security - Less marketable(better in masters

computer engineering - Poorly marketable

computer science  - Self employing and marketable

Geoinformatics - Less marketable but needed.

ICT mediated content development - New and poorly marketable

information systems - Marketable

Multimedia Technology and animation - Self employing course, marketable in Medias

software engineering - Marketable and self employing

Telecommunication Engineering - Marketable


Kozi za Diploma

Computer and business management - Marketable and self employing.

computer networks - Less marketable( uwanda mdogo)

Computer system administration - Marketable like IT

Graphics Design and web technology - Self employing

information and telecommunication technology - Marketable

information technology - Marketable

 





Kama unasoma IT, tambua CV yako haitakiwi kuishia na diploma/degree pekee  inatakiwa kuwe na certifications au skills ili uweze kuwa na tija kwa waajiri.
Certifications zinahitaji pesa, skills hazihitaji pesa ila zinahitaji jitihada binafsi na kujifunza.

App Development.

Siku hizi kuna soko kubwa sana la application za android na iOS maana watu wanatumia sana smart phones ambazo zinafanya vizuri zaidi katika hizo application/programu. Na kwa sasa gharama za kutengeneza App moja ya Android inafika millioni 5, ukisoma mtandaoni kwa njia ya video unaweza tengeneza ila sio vyepesi ni ngumu sana.
Kazi ambazo utapita kirahisi ukiwa na ujuzi huu ni Software Engineer, System Analyst, Business Analyst etc.

Networking

Huu ni ujuzi wa kufunga networks za computer, ujuzi huu huwa na certifications za Cisco ila kuufahamu kutakusaidia kupita kwenye interview nyingi za Kazi za IT.

Cyber security

Kama Networking na hii ni certification, ila unaweza soma online kwa bei nafuu na kuwa na hichi cheti utakua lulu katika kazi za makampuni ya mawasiliano, TCRA, na mabenki huwachukua mara moja watu hawa.

Comp TIA

Huu ni ujuzi wa computer in general maintenance na zaidi, harwdare na software ukiwa nao huuu kazi za ICT Officer utakuwa una nafasi kubwa sana za kuzipata..unaweza ukasoma yote bure mtandaoni ukafahamu ujuzi au ukasoma na kulipia certfication yake ukawa nayo.


Web Development

Huu ni ujuzi wa kutengeneza tovuti/website, kampuni nyingu huingia gharama za kuwaajiri watu kutengeneza website na kuzi maintain na nyignine bado hazina, ukiwa na huu ujuzi unaweza hata uka suggest katika application letter ya kwamba unaweza ukatengeneza na website ya kampuni pia.


Graphics Design

Hakuna kampuni isiyojitangaza na makampuni hulipia gharama kubwa sana kudesign haya matangazo, so ukiwa na ujuzi huu, utaokoa pesa kwenye kampuni inayotaka kukuajiri na hyo ukijtetea hata kwenye application letter wanaweza wakaona una umuhimu zaidi kuliko watu wengine kwenye interview.

Na skills nyingine kama za MS office, database na kadhalika...zote hizi kama upo chuo basi hakikisha unazizoa kwa hali na mali maana chuoni una muda huko njee hakuna muda wa kujifunza kuna muda wa kufanya tuu.






Rekebisha haya ili CV yako in'gae na upate kuitwa kwenye interviews/usaili.

Daftari/kitabu

Usiandike kitabu na experience ya kuandika huna, acha iwe page 1 au 2 tuu inatosha, kwa nini? Mfano wewe ndio afisa rasilimali watu ina CV 300 mezani utasoma CV ndefu?


Usiandike majukumu yako uliyokuwa unafanya awali.

Yeah naona kuna mtu alikuwa anakula baada ya kusoma hiyo anatafuna taratibu sasa, NDIO andika mafanikio na sio majukumu, mfano wewe ni mwalimu usiandike nilikuwa nafundisha, natunga mitihani, na kusahihisha instead andika nimefanikiwa kufundisha wanafunzi 500 geography na katika hao walifaulu 400, rafiki unaitwa haraaakaaa kuanza kazi.


kuweka vipengelea ambavyo havihusiani na kazi unayoitiwa.

CV sio ukishatengeneza basi ndio imetoka hapana, ukiitwa kwenye kazi ya jamii CV yako ioneshe sehemu ulijitolea hata kwenye vikundi vya dini, kuonyesha uongozi,  ila ukiitwa kazi ya ofisini, toa vipengele vya vikundi vya kijamii unavyojitolea maana utaonekana uko busy na kazi yao unaweza lipua au ukawa na visingizio vingi vya kutoka kazini.


Hobbies

Kama bado unaweka hizi acha huu uhuni.


Referees.

Usiweke mtu ambaye hajawahi kuwa supervisor wako au boss wako, kama unatoka chuo si  ulienda field? kawatafute huko, na utafute lecturer  hata mmoja, chondechonde usimuweke ndugu yako.


BONUS

Hebu nenda katafute muundo mzuri wa CV mambo ya CV Kuonekana kama CV ya Chifu Mashuposhupo acha...tembelea cvmkr.com itakusaidia.

Kwa ushauri na mawasiliano tembelea rainstech.com wasiliana nasi kupitia live chats






Ili uweze kufanya kazi mtandaoni unahitaji kuwa na ujuzi ambao mtu anaweza kuutumia ujuzi wako bila kuonana na wewe, na pia uwe na ujuzi wa lugha ya kiingereza vizuri ikiwezekana na lugha nyingine kubwa kama kifaransa.

Na hapo ndio unaona ujuzi wa IT huongoza katika hili lakini pia hata secretarial ila hizi kuna program nyingi ambazo zinafanya kazi zaidi ya secretary.

ujuzi au skills ambazo huhitajika mara kwa mara na watu haujiriwa  na kulipwa mtandaoni ni kama ziifuatazo:

Advanced microsoft office Skills( Excel, Word, Powerpoint, access)

Application development(Android, IOS, web applications)

Web design

Graphics Design( artworks, branding, video editing, adverts etc)

Mitandao inayotoa ajira hizi, inahitaji vitambulisho na sometimes ukitaka kuwa member basi utagharamia membership kama 10 dollars inategemea ila huwa ni bure, na katika kila malipo yako utakwatwa hela hapo.

Freelancer.com

upwork.com

Guru.com

na mingineyo ila hiyo ndio naona vijana wa Tanzania hapa hapa wanalipwa hela.

kwa ushauri wasiliana nasi kupitia rainstech.com live chats.



IT(Information Technology) ni kozi nzuri sana kwa vijana na pia ni mojawapo ya sekta ambayo makampuni yaliyowekeza humo yanatengeneza pesa nyingi sana.

Na tunapokwenda IT Imekuwa ikifuta nafasi za kazi nyingi sana kwa kompyuta kuzifanya hizo kazi, mfano;

Assembly line & factory workers

Phone Operators and receptionists

Cashiers

Bank tellers and clerks

Pilots

Journalists and reporters

Stock traders

Postal workers

Travel agents

Accountants

Na kadhalika ni kazi nyingi zinapotea,hatuwezi maliza ila pia IT inatengeneza ajira zake nyingi sana, nyingine hazihitaji hata uajiriwe na mtu.

NJIA  YA SHULE KUPITIA ADVANCE HIGH SCHOOL

Kuanza kama ni mwanafunzi wa sekondari hakikisha unasoma masomo ya science na biashara na uendelee advance na masomo hayo hlafu ukifika chuo  chagua kozi za IT.


NJIA YA SHULE KUPITIA CHUO

Soma mpaka form four masomo ya science na biashara, halafu chukua certificate ya IT, halafu diploma halafu degree. Vyuo bora ni University of Dodoma, St.Joseph University in Tanzania, Dar es salaam Institute of Technology,College of Information and Communication Technologies (CoICT) - University of Dar es salaam na University of Dar es salaam Computing centre.


NJIA YA  KUTOKEA CHUO NA KUENDELEA.

Soma kozi yeyote halafu ukimaliza unaweza nenda kwenye vyuo vya IT, kama unaweza soma degree nyingine ya IT au nenda kwenye vyuo vinavyotoa ujuzi wa IT na ujifunze unaotaka.

Mfano Degree ya Uchumi ila unapenda IT. basi nenda kwenye chuo kinachotoa IT, tafuta Ujuzi unaoutaka mfano:

Application Development

Networking(Inategemea vigezo)

Cyber security(Inategemea vigezo)

Computer TIA

Web development

Graphics Design.

Accounting package Training.

Halafu tafuta college inayotoa ujuzi husika katika vyuo nilivyoviorodhosha hapo juu.

Mara nyingi kozi nyingine hapo huwa hazifundiswi mavyuoni mfano cyber security au App development kwa hizi kozi inabidi ufanye paid online training katika mitandao kama Udemy, Tutsplus etc.


NJIA YA BURE

Kama unapenda IT na hauna hela zaidi ya hela ya bundle, basi chagua kozi unayotaka kusoma, halafu nenda kwa wanao download movies mtandaoni waambia wakusaidie kukutafutia hizo online courses then wakuwekee kwenye hard drive ili ukajifunze wemyewe privately, na watu wengi wamejifunza kwa njia hii, ila hautapata cheti chochote zaidi ya ujuzi.