Fahamu kozi za IT zinazotolewa kwa sasa Tanzania.

Misamiati muhimu:

Self employing - unaweza kujiajiri

Marketable - Ajira nyingi

Less marketable - Ajira chache

Poorly marketable - Ajira hakuna


Kozi za degree.

Business Information system - Marketable

Computer and information systems security - Less marketable(better in masters

computer engineering - Poorly marketable

computer science  - Self employing and marketable

Geoinformatics - Less marketable but needed.

ICT mediated content development - New and poorly marketable

information systems - Marketable

Multimedia Technology and animation - Self employing course, marketable in Medias

software engineering - Marketable and self employing

Telecommunication Engineering - Marketable


Kozi za Diploma

Computer and business management - Marketable and self employing.

computer networks - Less marketable( uwanda mdogo)

Computer system administration - Marketable like IT

Graphics Design and web technology - Self employing

information and telecommunication technology - Marketable

information technology - Marketable

 





Kama unasoma IT, tambua CV yako haitakiwi kuishia na diploma/degree pekee  inatakiwa kuwe na certifications au skills ili uweze kuwa na tija kwa waajiri.
Certifications zinahitaji pesa, skills hazihitaji pesa ila zinahitaji jitihada binafsi na kujifunza.

App Development.

Siku hizi kuna soko kubwa sana la application za android na iOS maana watu wanatumia sana smart phones ambazo zinafanya vizuri zaidi katika hizo application/programu. Na kwa sasa gharama za kutengeneza App moja ya Android inafika millioni 5, ukisoma mtandaoni kwa njia ya video unaweza tengeneza ila sio vyepesi ni ngumu sana.
Kazi ambazo utapita kirahisi ukiwa na ujuzi huu ni Software Engineer, System Analyst, Business Analyst etc.

Networking

Huu ni ujuzi wa kufunga networks za computer, ujuzi huu huwa na certifications za Cisco ila kuufahamu kutakusaidia kupita kwenye interview nyingi za Kazi za IT.

Cyber security

Kama Networking na hii ni certification, ila unaweza soma online kwa bei nafuu na kuwa na hichi cheti utakua lulu katika kazi za makampuni ya mawasiliano, TCRA, na mabenki huwachukua mara moja watu hawa.

Comp TIA

Huu ni ujuzi wa computer in general maintenance na zaidi, harwdare na software ukiwa nao huuu kazi za ICT Officer utakuwa una nafasi kubwa sana za kuzipata..unaweza ukasoma yote bure mtandaoni ukafahamu ujuzi au ukasoma na kulipia certfication yake ukawa nayo.


Web Development

Huu ni ujuzi wa kutengeneza tovuti/website, kampuni nyingu huingia gharama za kuwaajiri watu kutengeneza website na kuzi maintain na nyignine bado hazina, ukiwa na huu ujuzi unaweza hata uka suggest katika application letter ya kwamba unaweza ukatengeneza na website ya kampuni pia.


Graphics Design

Hakuna kampuni isiyojitangaza na makampuni hulipia gharama kubwa sana kudesign haya matangazo, so ukiwa na ujuzi huu, utaokoa pesa kwenye kampuni inayotaka kukuajiri na hyo ukijtetea hata kwenye application letter wanaweza wakaona una umuhimu zaidi kuliko watu wengine kwenye interview.

Na skills nyingine kama za MS office, database na kadhalika...zote hizi kama upo chuo basi hakikisha unazizoa kwa hali na mali maana chuoni una muda huko njee hakuna muda wa kujifunza kuna muda wa kufanya tuu.






Rekebisha haya ili CV yako in'gae na upate kuitwa kwenye interviews/usaili.

Daftari/kitabu

Usiandike kitabu na experience ya kuandika huna, acha iwe page 1 au 2 tuu inatosha, kwa nini? Mfano wewe ndio afisa rasilimali watu ina CV 300 mezani utasoma CV ndefu?


Usiandike majukumu yako uliyokuwa unafanya awali.

Yeah naona kuna mtu alikuwa anakula baada ya kusoma hiyo anatafuna taratibu sasa, NDIO andika mafanikio na sio majukumu, mfano wewe ni mwalimu usiandike nilikuwa nafundisha, natunga mitihani, na kusahihisha instead andika nimefanikiwa kufundisha wanafunzi 500 geography na katika hao walifaulu 400, rafiki unaitwa haraaakaaa kuanza kazi.


kuweka vipengelea ambavyo havihusiani na kazi unayoitiwa.

CV sio ukishatengeneza basi ndio imetoka hapana, ukiitwa kwenye kazi ya jamii CV yako ioneshe sehemu ulijitolea hata kwenye vikundi vya dini, kuonyesha uongozi,  ila ukiitwa kazi ya ofisini, toa vipengele vya vikundi vya kijamii unavyojitolea maana utaonekana uko busy na kazi yao unaweza lipua au ukawa na visingizio vingi vya kutoka kazini.


Hobbies

Kama bado unaweka hizi acha huu uhuni.


Referees.

Usiweke mtu ambaye hajawahi kuwa supervisor wako au boss wako, kama unatoka chuo si  ulienda field? kawatafute huko, na utafute lecturer  hata mmoja, chondechonde usimuweke ndugu yako.


BONUS

Hebu nenda katafute muundo mzuri wa CV mambo ya CV Kuonekana kama CV ya Chifu Mashuposhupo acha...tembelea cvmkr.com itakusaidia.

Kwa ushauri na mawasiliano tembelea rainstech.com wasiliana nasi kupitia live chats






Ili uweze kufanya kazi mtandaoni unahitaji kuwa na ujuzi ambao mtu anaweza kuutumia ujuzi wako bila kuonana na wewe, na pia uwe na ujuzi wa lugha ya kiingereza vizuri ikiwezekana na lugha nyingine kubwa kama kifaransa.

Na hapo ndio unaona ujuzi wa IT huongoza katika hili lakini pia hata secretarial ila hizi kuna program nyingi ambazo zinafanya kazi zaidi ya secretary.

ujuzi au skills ambazo huhitajika mara kwa mara na watu haujiriwa  na kulipwa mtandaoni ni kama ziifuatazo:

Advanced microsoft office Skills( Excel, Word, Powerpoint, access)

Application development(Android, IOS, web applications)

Web design

Graphics Design( artworks, branding, video editing, adverts etc)

Mitandao inayotoa ajira hizi, inahitaji vitambulisho na sometimes ukitaka kuwa member basi utagharamia membership kama 10 dollars inategemea ila huwa ni bure, na katika kila malipo yako utakwatwa hela hapo.

Freelancer.com

upwork.com

Guru.com

na mingineyo ila hiyo ndio naona vijana wa Tanzania hapa hapa wanalipwa hela.

kwa ushauri wasiliana nasi kupitia rainstech.com live chats.



IT(Information Technology) ni kozi nzuri sana kwa vijana na pia ni mojawapo ya sekta ambayo makampuni yaliyowekeza humo yanatengeneza pesa nyingi sana.

Na tunapokwenda IT Imekuwa ikifuta nafasi za kazi nyingi sana kwa kompyuta kuzifanya hizo kazi, mfano;

Assembly line & factory workers

Phone Operators and receptionists

Cashiers

Bank tellers and clerks

Pilots

Journalists and reporters

Stock traders

Postal workers

Travel agents

Accountants

Na kadhalika ni kazi nyingi zinapotea,hatuwezi maliza ila pia IT inatengeneza ajira zake nyingi sana, nyingine hazihitaji hata uajiriwe na mtu.

NJIA  YA SHULE KUPITIA ADVANCE HIGH SCHOOL

Kuanza kama ni mwanafunzi wa sekondari hakikisha unasoma masomo ya science na biashara na uendelee advance na masomo hayo hlafu ukifika chuo  chagua kozi za IT.


NJIA YA SHULE KUPITIA CHUO

Soma mpaka form four masomo ya science na biashara, halafu chukua certificate ya IT, halafu diploma halafu degree. Vyuo bora ni University of Dodoma, St.Joseph University in Tanzania, Dar es salaam Institute of Technology,College of Information and Communication Technologies (CoICT) - University of Dar es salaam na University of Dar es salaam Computing centre.


NJIA YA  KUTOKEA CHUO NA KUENDELEA.

Soma kozi yeyote halafu ukimaliza unaweza nenda kwenye vyuo vya IT, kama unaweza soma degree nyingine ya IT au nenda kwenye vyuo vinavyotoa ujuzi wa IT na ujifunze unaotaka.

Mfano Degree ya Uchumi ila unapenda IT. basi nenda kwenye chuo kinachotoa IT, tafuta Ujuzi unaoutaka mfano:

Application Development

Networking(Inategemea vigezo)

Cyber security(Inategemea vigezo)

Computer TIA

Web development

Graphics Design.

Accounting package Training.

Halafu tafuta college inayotoa ujuzi husika katika vyuo nilivyoviorodhosha hapo juu.

Mara nyingi kozi nyingine hapo huwa hazifundiswi mavyuoni mfano cyber security au App development kwa hizi kozi inabidi ufanye paid online training katika mitandao kama Udemy, Tutsplus etc.


NJIA YA BURE

Kama unapenda IT na hauna hela zaidi ya hela ya bundle, basi chagua kozi unayotaka kusoma, halafu nenda kwa wanao download movies mtandaoni waambia wakusaidie kukutafutia hizo online courses then wakuwekee kwenye hard drive ili ukajifunze wemyewe privately, na watu wengi wamejifunza kwa njia hii, ila hautapata cheti chochote zaidi ya ujuzi.