Showing posts with label Tanzania. Show all posts
Showing posts with label Tanzania. Show all posts

Tehama(Information technology) Katika nchi za chini ya jangwa la Sahara, Afrika Mashariki bado ni changa sana. Na kama inavyofahamika teknolojia hurahisisha sana maisha na hupunguza mzigo mkubwa wa kazi kwa watu.

GUNIA ZITO.

Nimeifananisha na gunia zito kwa sababu kutengeneza teknolojia mbadala ili kuweza kutatua changamoto katika jamii inahitaji mafunzo, moyo wa kujitoa binafsi na jitihada zaidi.

Lakini pia inahitaji macho ya kuona hizo fursa katika jamii ili uweze kuzifanyia kazi. Watu wengi hukimbilia kazi ambazo hazihitaji sana ubunifu lakini huku ubunifu ndio mahali pake, pindi unapokosa akili za  ubunifu basi utashindwa kufanya lolote katika tehama.

LENYE PESA

Kama nilivyoeleza hapo mwanzo, pindi teknolojia hizi zinapotengenezwa na wataalamu, huingia sokoni na kurahisisha maisha ya wengi.
watu wengi, makampuni mengi na watu wengi yametajirika sana duniani kwa tehama, mfano 

kampuni kubwa zaidi ya Tax duniani haimiliki tax hata moja bali imeunganisha wamiliki wa Tax,
lakini tatizo waliloliona ni shida ya kupata Tax pale ambapo unaihitaji na haupo barabarani. 

UBER  kwa sasa inaingiza mabilioni ya Pesa duniani kote, hata hapa Tanzania zipo programu kama za mpesa, tigopesa zinaingiza pesa nyingi mno, 

zipo programu za vituo vya mafuta kama Petronite

zipo programu za maduka kama duka pro,

na programu za masomo kama thL na kadhalika na kadhalika...

JINSI YA KUWA MMOJAWAPO WA WABEBAJI.

1. Uwe na uwezo kujifunza kwa bidii sana, na kukuballi kutatua changamoto mbali mbali hata zisizolipa kwa muda huo.

2. Chukua masomo ya Tehama kuanzia ngazi mbali mbali kama cheti, diploma au degree.

3. Ikiwa huna vigezo, basi ujue kusoma na kuandika kiingereza vizuri na uwe na moyo wa kishujaa wa kusoma zaidi ya wale wanaosoma darasani ila ni lazima utafanikiwa.

Janga la ukosefu wa ajira haliwezi kuisha kama tutaendelea kusaka watu kutoka njee wafungue makampuni ndio tuajiriwe ila tuu kama sisi wenyewe tutakapoamua kutoka na kugeuza changamoto kuwa mtaji wetu.


Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   
au elisanteshibanda@yahoo.com








Tehama(Information Technology), imejaa fursa nyingi, na katika nchi zetu changa, fursa ni nyingi mno.

Katika Tehama juhudi za mtu binafsi na Mungu wake, ndio zitamfanya afinikiwe au asifanikiwe.

Mtaji wa Tehama ni computer tuu, ambayo ni gharama ndogo sana kuipata.

Ni vitu gani mtu anaweza soma/jifunza ili afanikiwe katika Tehama.

Graphics Design(Sanaa ya Matangazo)
Hii ni sanaa ya matangazo ya biashara. Hakuna biashara duniani isiyotaka matangazo

na ukiangalia dunia ya leo, tumezungukwa na matangazo, yanazidi kuwepo na jinsi biashara zinavyozidi kuongezeka kasi ya uhitaji wa matangazo inazidi kuongezeka.

Jinsi ya Kujifunza
@ Chukua kozi fupi ya wiki 6, na wewe utaweza kuwa vizuri kwenye sanaa hii. 
Vigezo: Kuanzia Form Four Leaver
Price: 300,000Tsh
Training: MAXPO training
Mahali: Rains Technologies, Ilala Bungoni, Chunya str.

@Tumia njia ya Video ya kujifunza, kwa kutumia mitandao kama Youtube.






Web Development
Huu ni utaalamu wa kutengeneza tovuti mfano wa tovuti ni kama cnn.com, bbc.co.uk n.k 
Kila biashara inavyokua na kutaka kupita mipaka ya kiwilaya, kimkoa au kitaifa inahitaji tovuti kwa ulazima. Maana tovuti ni ofisi pekee ya kampuni ambayo inaweza fikiwa na mteja ,
Akiwa kokote kule duniani.

Kwa kuangalia uchumi wetu unavyokua na ongezeko la makampuni soko la tovuti litaongezeka maradufu.




Jinsi ya kujifunza
@Chukua kozi fupi ya wiki 8, ujifunze kutengeneza tovuti.
Training: MAXPO Training
Bei: 400,000/-Tsh
Mahali: Rains Technologies, Ilala Bungoni, Chunya str.

@Chukua certificate in InformationTechnology/Diploma/Degree kwa mwaka 1, 2, 3 N.k
Mahali: University of Dar es salaam Computing Centre
Vigezo: Tembelea chuoni.

@Tumia mafunzo ya vitabu na video za kwenye mtandao ili kujifunza kutoka kwa watu mbali mbali.


Computer Application
Kozi hii inakuweza kuifahamu computer ndani na njee, kuendesha stationery, na hata kutumia computer ya windows 10 na Apple computer(MAC OS) kama mtaalam.


Lakini pia inakupa uwezo wa kujifunza microsoft office yote.
Pamoja computer networks.

Jinsi ya kujifunza
@Chukua kozi fupi  ya wiki 4 ya Computer application.
Vigezo: Yeyote
Training: MAXPO Training
Bei: 250,000/-Tsh
Mahali: Rains Technologies, Ilala Bungoni, Chunya str.


@Chukua certificate /diploma/ degree katika Information Technology, computer science, ICT.
Mahali: University of Dar es salaam Computing Centre
Vigezo: Fika Chuoni.

@Tumia mtandao wa youtube kujifunza na google kupata vitabu.

Mafunzo ya Tehama, yanaanza taratibu na ni marahisi kwa mtu mwenye jitihada ya kusoma na nidhamu ya kujifunza bila kukata tamaa.
Kwa mawasiliano zaidi wasiliana nami.




Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   

au katika elisanteshibanda@yahoo.com
                  



Elimu ya IT hapa Tanzania ni changa sana na imejaa ujuzi mwingi na unahitajika sana katika Taifa hili, 
ujuzi wa IT wa ngazi ya chini kabisa, unaweza ukampa mtu uwezo mkubwa tuu wa kujiajiri na  
kuendeleza maisha yake.

Zifuatazo ni kozi ambazo zinaweza kumsaidia yeyote kuwa na uwezo wa kujiajiri.


Jinsi ya kufanya kazi na kulipwa mtandaoni ukiwa Tanzania

Course in Graphics Design.

 Kozi hii itamuwezesha mwanafunzi kufanya yafuatayo;
  • Kuchora chochote kwa njia ya kompyuta.
  • Kubuni/design magazeti, vitabu,vipeperushi,kalenda n.k
  • Kutengeneza matangazo makubwa na madogo kwa ajili ya kuprint au kuweka mtandaoni.
  • Kubuni/design business cards, cover letter, cards za mialiko N.K
  • Kurekebisha picha zilizopigwa na camera kiustadi zaidi na kuboresha muonekano wake.

Course in Web Design

 

Kozi hii inajikita katika kuunda tovuti za aina mbali mbali yaani za kibiashara na binafsi, na hii itampa mwanafunzi uwezo kufanya yafuatayo.
  • Kuweza kuunda tovuti(website) na kuelewa inayoendana na tovuti.
  • Kuipandisha tovuti kwenye mtandao.
  • Kuunda tovuti za kisasa kwa njia tofauti.
  • kutengeneza mablogu(tovuti ambazo watu wanaweza kuongea humo yaani kuchat mfano hii ni blogu) ya aina zote.
  • kusajili tovuti ndani na njee ya nchi.
  

Course in Computer Administration

 


  1. Ujuzi huu utamsaidia mwanafunzi kupata uwezo wa kufanya yafuatayo;
  2. Kufahamu kompyuta na mifumo inayoendana nayo.
  3. Kufahamu Computer Hardware, yaani vifaa vyake  na jinsi inavyofanya kazi, na hata kujua jinsi ya kuitengeneza pale inapoharibika. 
  4. Kufahamu Computer software, yaani programu za kompyuta na aina zake, jinsi ya kuziweka, kuzitoa na hata kuzishughulikia na kuzitibu pale ambapo zinakuwa hazifanyi kazi vizuri.
  5. Kufahamu mfumo wa usalama wa kompyuta, jinsi ya kuilinda kompyuta  yako na mshambulizi ya kimtandao ya virusi na watu wa njee wanaokuzunguka.
  6. Kufahamu mifumo ya mawasiliano(Networks) ya kompyuta, jinsi inavyofanya kazi na jinsi ya kuifunga njia ya kuilinda pia.
  7. Kufahamu jinsi ya kutumia windows 10 na programu nyingine za kuendesha kompyuta mfano windows 8 na Linux.
             



Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na magroup ya Whatsapp ya MAXPO Tanzania  Maximize your potential   

Course in Advanced Microsoft Office

Kozi hii inamsaidia mtu kuweza kufanya shughuli zote za kiofisi kwa njia ya kompyuta, kuanzia zile nyepesi mpaka zile ngumu kufanya kwenye kompyuta.
Kozi hutoa uwezo wa kufanya yafuatayo;

Kutumia programu za microsoft office zifuatazo

        Microsoft Word
        Microsoft Powerpoint
        Microsoft Excel

Kwa kiwango cha juu kabisa katika

        Kukusanya data
        Kuchambua data
        Kupresent/wasilisha data mbele za watu
Na pia kutengeneza njia za kuingiza data na kutumia microsoft office katika biashara yako yoyote ile 

kwa  ajili ya kumbu kumbu na hata kuonyesha muelekeo wa biashara, katika mapato na matumizi. 



Kumalizia kozi zote hizi hupatikana kwenye vyuo vya kitaalamu yaani Professional colleges ambazo zimejikita tuu katika kozi hizi, 
 kuchagua chuo chenye uwezo mdgo utakupelekea kupoteza muda wako na kutoka katika kiwango kibaya.

Nakushauri chukua mafunzo ya MAXPO Tanzania, yanatolewa na Kampuni ya Rains Technologies Co LTD iliyopo Ilala, Bungoni Str/Chunya Str Dar es salaam.

 na wanakupangia ratiba kulingana na ratiba yako na wana Professional Lecturers wenye uzoefu na pia ni wafanyabishara katika Tehama, kwa hiyo utapata, elimu na ushauri na kusaidiwa jinsi ya kuanza, ila pia kuna vyuo vingine vipo ila sina uhakika na hivyo ila pia ukumbuke jitihada zako binafsi zitakusaidia kupata ujuzi zaidi  

Kwa ushauri zaidi wasiliana nami katika 


Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na magroup ya Whatsapp ya MAXPO Tanzania  Maximize your potential   







Katika Upande wa Elimu ya juu, ni vizuri kupata ushauri bora kabla hujaenda kujiunga na chuo chochote.
Kwa maana uamuzi wako huo utaamua mambo yafuatayo katika maisha yako...




JINSI YA KUSOMA IT: Mwongozo kwa Wanafunzi Waliofeli Form Four, 2024

KIPATO CHAKO BINAFSI
Kozi hii ya IT, Kichwa chako ni ofisi yako, kwa hiyo kama utapata elimu mbovu,utapoteza uwezo wako wa kujiajiri na unaweza ishia pabaya.


AJIRA
Interviews za kazi hizi za IT, sio nyepesi, na kwa hali hii itakushinda kushindana na watu waliofundishwa vyema na kuwa wazuri katika maeneo muhimu ya Information Technology.

MCHANGO WAKO KWA TAIFA
Kozi hii au profession hiii au kazi hii ya IT ina mzigo mkubwa katika taifa hili changa kiteknolojia.
Kuna matatizo katika jamii ambayo yanahitaji kutatuliwa kidigitali,kwa sababu hii kama utakuwa na elimu mbovu,

utakuwa mmoja wa walalamikaji badala ya wabunifu na watatuaji matatizo.



VIGEZO VYA CHUO BORA KATIKA IT
Vifuatavyo ni mojawapo ya vigezo muhimu,ila vinaweza vikawepo vingine zaidi.




UBUNIFU UNAOFANYA KAZI
katika mavyuo mengi sikatai kama kuna ubunifu ila mwingi unaishia kwenye makaratasi ya chuo na kutupwa stoo(store). 
Ubunifu hujulikana kwa project ambazo zinavuka mipaka ya chuo na kuifikia jamii.

UFUATILIAJI WA CHUO KWA PROJECT ZA WANAFUNZI.
Kuna mavyuo yanaongoza kwa kutupa store project za wanafunzi lakini pia kutokuchukulia kwa umakini project zinazofanywa na wanafunzi, kiasi kwamba wanafunzi wako huru kuforge project zao na chuo kuzipokea tuu kwa kutokujali ya kwamba hii project imefanyika au laa. 

ASILIMIA YA VITENDO KATIKA ELIMU INAYOTOLEWA.
Ni muhimu kwa chuo kuwa na asilimia kubwa sana ya vitendo kuliko nadharia

VIFAA VYA KUJIFUNZIA IT
Ni muhimu kusoma  kwenye chuo chenye vifaa vya kutosha ili ujue haswa nini kinaendelea makazini ila ni kwa  asilimia ndogo hii pointi ina umuhimu maana IT inakuwa kwa kasi na Vyuo vya haviwezi kuwa na vifaa vya kisasa kila wakati.


"Chuo kinaweza kumtengeneza mhitimu wa IT,ila ni jukumu la mwanafunzi binafsi akiwa chuoni, kutoka chuoni kama mtaalamu,na sio mhitimu pekee kwa maana wahitimu hupata shida sana kutafuta ajira wakati wataalamu hutafutwa na ajira na pia hujiajiri."




Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na magroup ya Whatsapp ya MAXPO Tanzania  Maximize your potential   


VIFUATAVYO NI VYUO BORA KUJIFUNZA IT  TANZANIA.
 1. Dar es salaam Institute of Technology (DIT)

2. St. Joseph University in Tanzania.

3.University of Dar es Salaam.

4. University of Dodoma



Kwa kumalizia, vyuo vipo vingi na wanafunzi wanazidiana uwezo 
kwa hiyo inawezekana ubunifu wa hali ya juu ukatokea kwenye chuo ambacho hakipo hata kwenye list hii, 
na pia vyuo vingine vinaweza vikaboresha ufundishaji wake na kuvipiku vyuo vilivyopo sasa.

Na la muhimu college za IT zipo nyingi na kwenye mikoa mingi, kwa hiyo kukosa nafasi kwenye vyuo hapo juu haimaanishi IT yako umeitupa, ila ina maana wewe ndio wa kukin'garisha chuo ulichokuwepo.




Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na magroup ya Whatsapp ya MAXPO Tanzania Maximize your potential  


 





Fahamu kitovu cha teknolojia( Technology Hub) hapa Tanzania ambacho wanafunzi wa chuo na wataalamu katika nyanja mbali mbali za teknolojia yaani Software developers, Web developers, Electricians, Electronics Engineers and Computer Engineers n.k hukutanika na kuvumbua au kuboresha vitu.

Kitovu cha teknolojia au kwa lugha ya kiingereza technology hub ni sehemu ambazo huanzishwa kwa malengo ya uvumbuzi na utatuzi wa matatizo kwa nji ya teknolojia. 


Kwa Afrika, sehemu hizi zimefikia 314 katika miji 93 katika inchi 42 nchi kama South Afrika ikiwa inaongeza kuwa na vitovu vingi.

Kwa hapa Tanzania, tuna kitovu cha teknolojia kimoja ambacho kinaitwa Buni Hub.

BUNI Hub.
Buni huhusika zaidi na kuwasaidia wanafunzi hata watu wabunifu katika teknolojia kwa kuwapa ushauri(mentoring) na kuwaongoza kupata uwezo wa kufanya ujasiriamali kwa kupitia teknolojia n.k.


BUNI huwa inaendesha semina, mafunzo mafupi mara kwa mara ili kuweza kuwajenga wanachama wake katika uanzishwaji wa project na hata usimamizi wa project hizo za kitaalamu na kuwaongoza waweze kufikia malengo yao.
Kwa maelezo zaidi tembelea tovuti ya BUNI hapa na wasiliana nao kuweza kujiunga. 

MANUFAA YA KUJIUNGA.
Utajenga uwezo wako binafsi katika kubuni mambo mbali mbali ya kiteknolojia.


Utakutanishwa na watu ambao wana mawazo kama yako ambao watakusaidia kusimama vizuri zaidi.

Ni sehemu ambayo inaweza ikawa uwanda wa wewe kuelewa njia ya kupata hata ufadhili wa kazi yako. 

Muhimu zaidi chochote ambacho hutumii kitapotea na kama wewe ni mwanafunzi wa IT,au kozi zozote za science ni muhimu kuwa pamoja na watu ambao wana elimu kama yako ili elimu yako isije ikalala na ukaanza kufakamia fani za watu wengine.

Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   

Application Programmer huhusika na kudesign, kutest programu katika upande wa logic, pia huandaa documentation na kutengeneza programu kwa ajili ya matumizi ya kampuni husika.


Kazi Afanyazo

  • Anafanya coding, testing, debugging, documenting na installation ya programu.

  • Anatumia lugha maalumu za computer ili kuongeza ufanisi wa programu zinazoendelea kufanya kazi.

  • Anafuatilia ufanyaji kazi wa ufanisi wa programu zote zinazofanya kazi, na kushughulikia mapungufu yote yanayojitokeza.

  • Anatumia mahitaji maalumu ambayo amepewa na kampuni, na kutengeneza programu mbazo zitasaidia kutimiza malengo hayo...mfano: Vodacom wanapotaka kuongeza offer kwenye menu ya MPESA watahitaji kumuona huyu mtu.

  • Muda wote huutumia kujiupdate ili kuhakikisha ya kwamba mifumo yote ya kampuni inafanya kazi katika viwango vya kisasa.

  • Hujifunza na kuchambua kazi mbali mbali za kampuni na kutoa mchango wake katika kuboresha mifumo husika ili kuleta ufanisi wa hali ya juu katika MIS(Management Information Systems).


Vigezo Vya Kazi.
  • Awe na uelewa mzuri wa software na hardware( Technical Capacity)

  • Awe na uwezo mzuri wa kutatua changamoto zote zinazojitokeza kwa kutengeneza majawabu ya kiteknolojia.(Problem Solving/ Analysis)

  • Awe na uwezo wa kujisamamia mwenyewe na kuchukua hatua mbali mbali za kiutendaji(Initiative).

  • Uwe na uwezo mzuri wa kuwasiliana na wengine na kuweza kuwasilisha kile ambacho unataka kufanya kwa lugha nyepesi na ya kueleweka zaidi.

  • Uwe vizuri katika kutumia muda vizuri.


Elimu na Mafunzo
Uwe amepitia kozi zifuatazo , lakini pia awe na ujuzi binafsi wa lugha za computer kama zifuatazo Java, Android, PHP, SQL, HTML,CSS, ASP.Net, Javascript, Python, VB.Net etc.

Bachelor in Computer Science

Bachelor in Information Systems

Bachelor in Software Engineering

Bachelor in Computer Engineering

Bachelor in Information Technology

Na kozi nyingine zinazofanana na hizo hapo juu. 
Kwa maelezo, msaada au ushauri zaidi usisite kuzungumza nami. 

Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa    

elisanteshibanda@yahoo.com



Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa