Kwa miaka tumekua tukiona watu wanaanzisha mablogu kama michuzi, milardayo na wengineo wengi, na tunafurahi maana wanatuletea taarifa nyingi kwa kweli, lakini unajua hawa wanapata hela nyingi ambazo hata wewe unaweza pata!!!

Blogu ni tovuti ambazo zinaruhusu mtumiaji aweze kuhusishwa na kile ambacho kimewekwa kwenye tovuti, kama habari kwa mfano, mtu anaweza iona na kuandika yeye ameiopokeaje na hata kuwasiliana papo na hapo kwa watu wengine kuhusu habari hiyo.

Je kuanzisha biashara hii inagharimu kiasi gani?
Kuanzisha biashara hii inahitaji uwelewa wa utumiaji wa mtandao, inahitaji uwe na internet zaidi ya hapo hakuna gharama nyingine zaidi...Kumbuka: uelewa huu wa mtandao sio wa kwenda chuo ni uelewa mdogo tuu  ambao unaweza kujua ndani ya wiki 2 au moja tuu.

Nini kinahitajika ili kuanzisha biashara hii?
unahitaji kitu cha kuandika, mfano michuzi yeye kaamua kujikita kwenye habari na kwa hilo amewapata wengi ambao wanatembelea kwenye blogu yake...kama hauna fikiri kwanza ni kitu gani  watu gani wanataka.

Unapataje pesa sasa?
Jinsi blogu yako itakavyo vuta watu wengi na kuingia, basi utapata hela kwa njia zifuatazo;

  • Matangazo
Ukitembelea blogu hizi utakuta matangazo kama ya vodacom na makampuni mengine ambayo hulipa mtu anapoclick tuu na hata mtu anapoliona hilo tangazo. Mfano mkikubaliana mtu anapoclick upate Tsh 100 na kuendelea na kwa mwezi labda ulipwe laki 4 ni wewe utachagua na kukubaliana na mwenye tangazo.

  • Pia unaweza uza vitu kama vitabu vya mtandao vyenye mafunzo mbali mbali kwa njia ya sauti au video kwa watu.

  • Unaweza pia ukauza post zako kwa njia ya kuwaweka kampuni kama ndio wamechangia kuileta...mfano: unawe za kwenye TV kipindi cha Tamthilia unasikia tamthilia hii imeletwa kwenu na Wizara ya afya.
Ukweli ni kwamba huku ubunifu wako utakuletea pesa, na kujitoa kwako na ukitaka kujifunza hivi endelea kutembelea hapa na karibuni tutaleta mafunzo haya bure.
Tehama(ICT) na Teknolojia kwa ujumla imeweza kuajiri zaidi ya milioni 6.7 na inawalipa mara 2 zaidi ya sekta nyingine katika Nchi ya Marekani(compIT), lakini kwa hapa Tanzania bado fani hii ina watu wachache sana na ukizingatia vijana wengi wanalalamika ukosefu wa ajira.

Kwa nini ni jawabu mojawapo la Ajira?

  • Mtaji wake ni mdogo sana na ukilinganisha na maeneo mengine ya kuwekeza kama kilimo na sekta nyingine na pia unalenga vijana zaidi ambao ndio wanakumbwa na tatizo hilo la ukosefu wa ajira.
  • Tehama haihitaji mtu aajiriwe ili aweze kujipatia kipato kwenye sekta hii kwa maana hutegemea zaidi ubunifu wa mtu na juhudi zake binafsi na mahali mtu alipo ndio panaweza geuka ofisi.
  • Unaweza ukajifunza tehama bila hata kuingia darasani au kwenda chuoni na ndani ya mwezi ukawa vizuri kabisa.

Ukitaka kujifunza tehema tupigie nasi tutakupa mwanga katika tasnia hii.
Mobile: +255753592886     
Office:   +255714323785   
 Programu bora Afrika
   Afrika hatuna haja ya kushindana kugundua teknolojia kama Mataifa mengine kwa maana huko huhitaji pesa nyingi sana, ila tunaloweza kufanya ni kuitumia teknolojia iliyekuwepo na kuiweka katika mazingira ambayo itatusaidia katika maisha, Pongezi ziwaendee hawa wataalamu hawa wa tehama walivyo weza kufanya haya. Angalizo zipo nyingine sokoni pia ila muda unavyozidi kwenda tutazigundua na kuzitangaza ili zifahamike. Tazama hapa