Ulimwengu wa teknolojia ya mtandao yaani Information technology ni mkubwa sana, na  wengi huwa wanajikuta wanashindwa kufikia malengpo yao, kwa  kushindwa kujua tofauti ya kozi zilizopo, hebu fuatilia uelewe kipi ni kipi?

Information Technology

Hii ni kozi ambayo inadili zaidi na mawasiliano ya njia ya kompyuta na uendeshaji wa mifumo/systems ya kompyuta na hata designing. 

kozi hii hutoa watu/professionals ambao ni system administrators,ICT officers, Graphics Designers etc 


watu ambao wapo kwa ajili ya kuwasaidia watu wengine kuweza kutumia vizuri, mifumo ya kompyuta.

Kazi.

Hawa watu wengi huwa wanaajiriwa, 

zaidi ila pia wanaweza kuajiajili kwa katika kufanya maintenance ya vifaa vya ICT, ICT Equipment supply, 

na hata kufunga mifumo ya network sehemu mbali mbali na akijiendeleza huweza kuwa Webmaster wa tovuti mbali mbali.

Kipato.

Mishahara yao hulipwa kulingana na elimu ya Degree au ya diploma aliyonayo kama fani nyingine na Zaidi ikizingatia kazi anayofanya na unyeti wa kazi hiyo.



Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   

Computer science.

Uwanda huu upo ndani zaidi kuliko IT, maana hawa watu mbali na kujua vitu vyote vya kozi ya IT,


pia huweza kujua kutengeneza program za aina mbali mbali za computer, na pia hufundishwa lugha nyingi za computer na huwa wako vizuri kiasi hata kwenye hardware ya computer.

Kazi.

Hawa watu utawakuta kama pia ma system administrators, business analysts, system analysts, ICT Officers, Application programmers, software developers. 

Pia wengi hujiajiari na kuanzisha makampuni/biashara za kutengeneza kompyuta hardware na software, 
websites na kazi nyinginezo nyingi katika uwanda wa technology.

Kipato

Wanapoajiriwa kipato chao hakitofautiani na IT.

Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   

Computer Engineering

Fani hii, hujikita Zaidi na hardware ya computer, huku tunapata watu ambao wanaunda vifaa ambavyo vinaweza fanya kazi na mifumo ya computer. 

Hawa kwa nchi zenye viwanda vya kutengeneza vifaa hivyo,  huwa ni soko kubwa sana, 

ila kwa nchi ambazo zinaendelea huwa bado wana soko dogo sana, na hata huogopwa kuajiriwa kulingana na Title yao ya Kuwa engineer.

Kazi.

Hawa hufanya kazi ya kutengeneza vifaa ila pia huweza kufanya kazi nyingi ambazo mtu wa computer science anafanya, 
pia ni mafundi waliobobea katika kurekebisha computer mbovu.

Kipato

Hawa huwa na mshahara wa juu kuliko IT na Computer Science, maana hulipwa katika kiwango cha ma engineers,

 lakini pia hufungua biashara kubwa za computer maintenance na hardware Suppliers na zaidi...
  

Software engineering

Katika Fani hii tunakutana na watu ambao wanataka kubobea katika kutengeneza programu za computer, 

hawa watadeal na program tuu na kidgo sana mambo mengine katika fani ya teknolojia.


Kazi.

Hawa hufanya kazi kutengeneza program za kila aina, pia huingia kwenye network na kubobea humo,

na huwa pia kuweza kufanya kazi za Computer Science kwa kiasi na hukinzana kabisa na computer engineers maana wao hufanya kazi na hardware.

Kipato

Hawa wana mshahara mkubwa wa kiwango cha Engineer kama computer engineer anavyolipwa na pia huwa wanajiajiri sana na kuanzisha makampuni ya kutengeneza programu.

 

Jinsi ya Kujiendeleza…

Ulimwengu wa Computer umejaa vyeti vya mafunzo mbali, 

ili mtu abobee katika sehemu maalumu hizo huitwa certifications mfano mafunzo ya Network hutoa vyeti,

kama CCNA, CCNP na kuendelea na mafunzo ya database kama Oracle , na hata auditing(Ukaguzi) kwa maelezo Zaidi fuatilia article yangu ya kuhusu certications za IT.


Lakini pia anaweza jiendeleza katika masters degree za vitu mbali na hata kuwa Tutorial au lecturer au professor maana bado kuna upungufu mkubwa mno katika ngazi hizo.

Kwa muongozo zaidi, Wasiliana nami katika email elisanteshibanda@yahoo.com au

Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa    



 

Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   



Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   


Fahamu jinsi ya kuuingiza biashara yako katika ulimwengu wa kisasa wa computer, wenye ufanisi na faida kwako maradufu.

Programu ni kitu gani?

Programu ni maelekezo ambayo huandikwa na mwanadamu katika lugha za ki computer ili computer iweze kuyafuata na kurahisisha ufanyikaji wa kazi fulani.

Ni biashara gani unaweza tumia 

programu hizi?

Biashara ya aina yeyote ile inaweza kurahishishwa uendeshaji wake, kwa asilimia 80% na zaidi, katika uendeshaji wake.

Faida ya kutumia programu ni zipi?

Faida ni nyingi sana ila kuzitaja kwa uharaka ni kurahisisha uendeshaji wa biashara mfano duka linalotumia programu katika kuhifadhi mauzo yake, huwa lina uwezo kujua nini kipo na nini kimekwisha kwa uharaka zaidi na hata ni bidhaa gani imekwisha muda wake wa matumizi kwa uharaka zaidi na pia hata kujua faida iliyopatikana kwa siku mara moja, kwa kubonyeza button moja tuu na hata kujua biashara inaendeleaje na hata kupewa ushauri na programu hiyo hiyo kipi cha kuongeza na kipi kimekaa muda mrefu.

Aina za programu ambazo hutumika.

Programu hizi zipo na zinatofautiana kutokana na vipengele vifuatavyo.
·         UTENDAJI KAZI
Hapa kuna programu ambazo zenyewe zimetengenezwa kwa ajili ya shughuli zote za kibiashara na za kiofisi, hizi mfano ni Microsoft office package, hizi hutumiwa kwenye biashara yeyote ile, kwa mafunzo mafupi sana.
Pia Kuna programu ambazo zinatengenezwa mahususi kwa ajili ya biashara yako na wataalamu wa computer ambao wewe utawalipa kwa ajili ya kazi hiyo, programu hizi huwa na ufanisi mkubwa mno kulinganisha na hizo za awali hapo juu.

·        Gharama
Programu zote zile ambazo utahitaji utengenezewe na wataalamu wa computer hizi zitakugharimu zaidi, ila kwa bei ya soko la sasa, huwa zinaanzia kiasi cha Tsh.400,000/= na kuendelea hii ni kutokana na mfumo wa biashara yako, kama ni mkubwa sana basi gharama huwa juu, kama ni mdogo sana basi gharama huwa chini.

Ila kwa programu ambazo zimeshatengenezwa teyari kwa ajili ya kazi hiyo, nikiamaanisha mfano microsoft office zenyewe ni gharama nafuu zaidi kuanza kutumia, chini sana ukilinganisha na  kundi la programu za hapo juu.
Jinsi ya kupata programu mahususi 

ajili ya biashara yako.
 Ondoa shaka kabisa hapa kuna wataalamu mbali mbali ambao wamebobea katika utengenezaji wa programu hizi kwa sasa ni....
·         Duka Pro
·         Nyumbani Creative
Endapo utahitaji maelezo mengine yeyote zaidi, kuhusu maswala haya, usisite kuwasiliana nami, nitakusadia zaidi katika elisanteshibanda@yahoo.com na +255753592886 
 Jinsi ya kupata programu ya kiofisi 
  ajili ya biashara yako.

Jinsi ya kupata programu hizi na mafunzo ya jinsi ya kuitumia, tafadhali wasiliana nami pia kwa namba nilizozitoa hapo juu au unaweza kutafuta madukani na wakakuwekea kwa gharama nafuu zaidi ila kwa mafunzo inabidi utafute vyuo vinavyotoa mafunzo ya "computer course" ambayo pia hata mimi ni trainer/mwalimu wa hayo mafunzo ndani ya wiki chache tuu utakuwa teyari kabisa.
  Hitimisho

Computer huwa zinaathiriwa na virusi na hata watu wenye nia mbaya wanaweza ingia na kufuta taarifa zako, kwa hiyo kuwa makini computer yako kujua nani anaitumia na jee ni muhusika, na pia kutumia programu za kujikinga na virus zinazoitwa Anti-Virus mfano Karspesky na zaidi hifadhi data zako sehemu mbali mbali mfano kwenye external drives, flash drives na internet.

Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   
Elisante Shibanda.
IT Consultant/Trainer 
elisanteshibanda@yahoo.com
+255753592886