Kama kijana mdogo nisiyekuwa na uzoefu  hata kidogo  wala msaada katika biashara, nilijikuta nikiona jinsi gani duka la Mangi lilikuwa likikua kwa kasi, na la kwangu taratibu mno, nilijiuliza maswali mengi lakini kwa sababu Mangi alikuwa mfanyabiashara mwenzangu na rafiki yangu sikusita kumuomba ushauri, na ndipo aliponiambia mambo haya amabyo yalibadilisha biashara yangu na mtazamo wangu katika uwanda huu wa biashara.

MTAJI.
Unapoanzisha biashara na unapokuwa na mtaji wako wa kiasi fulani , unapokuwa ukipata faida . inakupasa ufanye kila liwezekanalo kutogusa FAIDA, sijakosea sio MTAJI pekee bali FAIDA na MTAJI kwa mwaka mzima, hapo ndipo utaona ukuaji wa duka unaostahili..utapata wapi hela ya kula na matumizi mengine we mtu mzima umiza kichwa.

UENDESHAJI
Imezoeleka kuwaweka ndugu na jamaa au hata watu tuu tunaowaajiri kama wauzaji halafu sio tukaendelea na kufanya kazi nyingine.HAYO NI MAKOSA TENA NI MWIKO KUFANYA HIVYO.
Wafanyakazi waajiriwa wengi wameanzisha maduka yamekufa kwa sababu hiyo.
Wanaopaswa kuendesha duka lako ni "WEWE", "MKEO" na "WEWE+MKEO" kama watu hao hawatakuwepo, tafuta shughuli nyingine ya kufanya na hela yako.

MUNGU
Unaweza ukafanya vizuri kote katika hayo niliyoyasema hapo juu, lakini ukweli ni kwamba biashara zimetawaliwa na nguvu za giza sana, ni lazima uchague utakaa upande gani na ukae huko moto  moto na sio robo au nusu, kama ni uchawi ujue ipo siku utakufa na biashara yako itakufa vibaya na utaangamiza watoto na familia yako so nakushauri mtafute Mungu wako.

NIDHAMU
Watu wengi huchukia mabosi, wakiwaona kama wanawanyanyasa wanavyowashurutisha kufanya kazi, yaani wakitunza nidhamu kazini, lakini ukweli ni kwamba biashara inahitaji nidhamu ya hali ya juu mno, isiyosuburi kukumbushwa...mazoea, uchelewaji, kauli chafu,uvivu huua biashara mara moja.

UTU
lazima uwe na utu, ujali wafanyakazi wako, kimahitaji na hata kimahusiano yaani waheshimu, hata kama umewazidi kipato kiasi gani.
"Kumbuka wamiliki wengi wa biashara wameuawa na majambazi kwa mpango uliosukwa na wafanyakazi wao au hata kuporwa mali kutokana na kisasi walichonacho wafanyakazi"

FULLITIME/PARTTIME
Biashara sio part time nik full time job kama hauko teyari kuwekeza muda wako wote nenda kanunue hisa wekeza huko maana huko hauhitajiki sana kama una hisa ndogo na hisa zikizidi bado ushauri wangu utaendelea utakabidhiwa ofisi tuu.

Kwa hayo nimeona nikushirikishe wewe ili kama umejipanga kufanya biashara basi uwe makini usije ukapoteza hela zako bure.
Mangi yeye ni mfanyabishara mkubwa wa maduka ya jumla ya vyakula kwa aina nyingine ya biashara tanua fikra zako.

Tehama inaleta mabadiliko makubwa sana katika ulimwengu wetu tena kwa kasi kubwa mno, kasi hii ina pande mbili  yaani nzuri na upande mwingine ni hatari. Katika uzuri wake ni kweli mtumiaji wa mwisho hupata urahishwaji zaidi wa kazi na ubora zaidi ila kasi hii kwa upande wa biashara na wataalamu waliopo ndani inaweza kukuza na hata kuua biashara kwa kuchelewa kidogo.

Yafuatayo ni mambo 5 muhimu kujua kama unataka kuingia katika ulimwengu huu wa tehama kwa njia ya kusoma au kufanya biashara.


  1. Kubali mabadiliko haraka na zaidi jifunze kuendana nayo kwa uharaka huo huo kama yalivyoingia, kwa sababu unavyoyagomea au kuchelewa kubadilika ni kama kuivisha biashara yako kitanzi.
  2. Mfano :
    kampuni ya zamani ya kutengeneza programu za kusafu(browse) mtandao yaani browser inayoitwa Netscape ilikuwa inauza programu zake na kufaidika sana lakini ghafla kampuni ya Microsoft iliamua kutengeneza na kugawa bure browsers hali iliyopelekea kampuni ya Netscape kwenda mahakamani kuizuia kampuni ya Microsoft ila haikufanikiwa ilikufa baadaye kwa kukataa mabadiliko.
     2. Uwe mtu wa kupenda kujifunza sana kupitia mtandao wa internet na mara kwa mara kuangalia            teknolojia mpya ili usije ukashtuliwa na kuingia kwa teknolojia mpya.
    
    3. Weka maono makubwa na ya mbali yanayoendana na eneo husika na ukuaji wake wa teknolojia          na pia ukilinganisha na ukuaji wa teknolojia hiyo duniani.
       Mfano: unapofungua Internet cafe sehemu nyingine hazihitaji kabisa hiyo huduma kwa sababu             ya jamii husika ina kipato kikubwa na sehemu nyingine inahitaji huduma za printing tuu na              copy, na sehemu nyingine inahitaji zote yaani internet,printing na copy(ila hiyo sio investment               pekee).
        
     4.Kwa Wanafunzi
   Wanafunzi wa ulimwengu huu wa tehama wana kazi mbili ya kwanza ni upokea kinachotoka               chuoni na ya pili ni kuupdate kile kinachotoka chuoni kwa sababu teknolojia hukua kwa kasi na        hata ikibadilishwa mitaara kwa kasi kiasi gani vyuo havitaweza kuendana na kasi hiyo na hata           kuwafanya wanafunzi kupoteza kufahamu misingi ya teknolojia kwa uzuri zaidi.

    5.Kutokana na kubadilika badilika kwa sekta hii inakupasa kuweza kujua kiwango cha mabadiliko ndani ya sekta hii . Mfano biashara ya kuuza simu ina kiwango kikubwa sana cha mabadiliko(simu hupitwa na wakati kwa haraka zaidi ya laptop) ukilinganisha na biashara ya kuuza kompyuta pakato(Laptop) ila zote zinabadilika.

    6.Onana na wafanyabiashara husika na pia IT Professionals au IT Consultants maana wao hujua soko lipoje na faida ipoje katika maeneo mengi ya ICT na kitu cha kuwekeza kwa sasa na kwa njia gani utaanza kuwekeza.

  Kwa ushauri zaidi wasiliana nasi!



Kwa miaka tumekua tukiona watu wanaanzisha mablogu kama michuzi, milardayo na wengineo wengi, na tunafurahi maana wanatuletea taarifa nyingi kwa kweli, lakini unajua hawa wanapata hela nyingi ambazo hata wewe unaweza pata!!!

Blogu ni tovuti ambazo zinaruhusu mtumiaji aweze kuhusishwa na kile ambacho kimewekwa kwenye tovuti, kama habari kwa mfano, mtu anaweza iona na kuandika yeye ameiopokeaje na hata kuwasiliana papo na hapo kwa watu wengine kuhusu habari hiyo.

Je kuanzisha biashara hii inagharimu kiasi gani?
Kuanzisha biashara hii inahitaji uwelewa wa utumiaji wa mtandao, inahitaji uwe na internet zaidi ya hapo hakuna gharama nyingine zaidi...Kumbuka: uelewa huu wa mtandao sio wa kwenda chuo ni uelewa mdogo tuu  ambao unaweza kujua ndani ya wiki 2 au moja tuu.

Nini kinahitajika ili kuanzisha biashara hii?
unahitaji kitu cha kuandika, mfano michuzi yeye kaamua kujikita kwenye habari na kwa hilo amewapata wengi ambao wanatembelea kwenye blogu yake...kama hauna fikiri kwanza ni kitu gani  watu gani wanataka.

Unapataje pesa sasa?
Jinsi blogu yako itakavyo vuta watu wengi na kuingia, basi utapata hela kwa njia zifuatazo;

  • Matangazo
Ukitembelea blogu hizi utakuta matangazo kama ya vodacom na makampuni mengine ambayo hulipa mtu anapoclick tuu na hata mtu anapoliona hilo tangazo. Mfano mkikubaliana mtu anapoclick upate Tsh 100 na kuendelea na kwa mwezi labda ulipwe laki 4 ni wewe utachagua na kukubaliana na mwenye tangazo.

  • Pia unaweza uza vitu kama vitabu vya mtandao vyenye mafunzo mbali mbali kwa njia ya sauti au video kwa watu.

  • Unaweza pia ukauza post zako kwa njia ya kuwaweka kampuni kama ndio wamechangia kuileta...mfano: unawe za kwenye TV kipindi cha Tamthilia unasikia tamthilia hii imeletwa kwenu na Wizara ya afya.
Ukweli ni kwamba huku ubunifu wako utakuletea pesa, na kujitoa kwako na ukitaka kujifunza hivi endelea kutembelea hapa na karibuni tutaleta mafunzo haya bure.
Tehama(ICT) na Teknolojia kwa ujumla imeweza kuajiri zaidi ya milioni 6.7 na inawalipa mara 2 zaidi ya sekta nyingine katika Nchi ya Marekani(compIT), lakini kwa hapa Tanzania bado fani hii ina watu wachache sana na ukizingatia vijana wengi wanalalamika ukosefu wa ajira.

Kwa nini ni jawabu mojawapo la Ajira?

  • Mtaji wake ni mdogo sana na ukilinganisha na maeneo mengine ya kuwekeza kama kilimo na sekta nyingine na pia unalenga vijana zaidi ambao ndio wanakumbwa na tatizo hilo la ukosefu wa ajira.
  • Tehama haihitaji mtu aajiriwe ili aweze kujipatia kipato kwenye sekta hii kwa maana hutegemea zaidi ubunifu wa mtu na juhudi zake binafsi na mahali mtu alipo ndio panaweza geuka ofisi.
  • Unaweza ukajifunza tehama bila hata kuingia darasani au kwenda chuoni na ndani ya mwezi ukawa vizuri kabisa.

Ukitaka kujifunza tehema tupigie nasi tutakupa mwanga katika tasnia hii.
Mobile: +255753592886     
Office:   +255714323785   
 Programu bora Afrika
   Afrika hatuna haja ya kushindana kugundua teknolojia kama Mataifa mengine kwa maana huko huhitaji pesa nyingi sana, ila tunaloweza kufanya ni kuitumia teknolojia iliyekuwepo na kuiweka katika mazingira ambayo itatusaidia katika maisha, Pongezi ziwaendee hawa wataalamu hawa wa tehama walivyo weza kufanya haya. Angalizo zipo nyingine sokoni pia ila muda unavyozidi kwenda tutazigundua na kuzitangaza ili zifahamike. Tazama hapa

Hebu jaribu kuchukua nafasi ya Human resource manager(Meneja wa rasilimali za binadamu) akiwa amepokea maombi ya watu 5000 kwa ajili ya nafasi moja ya kazi aliyoitangaza, unadhani atapitia na CV yako kwa jinsi ilivyo?

Basi kama unataka kufanya CV yako, ipendeze kimuonekano na hata iweze kumzuia meneja aliyechoka kupitia CV za watu hebu ingia hapa tengeneza akaunti yako bure na fuata maelekezo maana ni rahisi mno kutumia.
 
  • Kwanza Relax acha uoga na punguza presha, kutype ni kitu chepesi sana.
  • Fahamu herifu za kompyuta zilipo na ukumbuke taratibu taratibu mahali zilipo kila moja hata ikiwa moja kwa siku.
  • Acha kutype kwa kidole kimoja, tafadhali weka mikono yako yote kwenye keyboard na yote ifanye kazi ya kutype.
  • Acha kutumia kidole kimoja kwa kutype kwa kila mkono, tumia vidole vyote kwa kila mkono.
  •  Hakikisha kila kidole kina herufi ambazo kina husika na kutype zinaweza zikawa mbili au tatu ...mfano kidole changu kidogo kinahusika na herufi A,Q huku kidole gumba kikitumika kwa space.
  • Usiogope kukosea kutype herufi pindi unapotype kwa haraka maana hamna shortcut lazima ukubali makosa ili uweze kupata spidi nzuri ya kutype.
  • Tumia programu za bure kabisa za kukufundisha kutype ndani ya wiki moja utakuwa vizuri kabisa. mfano: tembelea hapoa ujipatie programu yako ya bure www.typingmaster.com
  1. Usiishi katika mitandao ya kijamii HAMNA MAISHA HUKO UNAJIDANGANYA TUU!!
Siku ina masaa 24, usitumie masaa mengi huko maana sio maisha halisi kama unavyodhani. kaa na watu unaowajali zaidi, watu halisi wa karibu yako ie majirani,utakapoumwa au kuwa na tatizo la ghafla huyo rafiki yako mbelgiji au mnamibia au muafrika ya kusini hataweza kukusaidia.

    2.Usipende kuandika ujinga.
Katika ulimwengu wa sasa, watu wengi hutafuta kuwafahamu wengine katika uelewana hekima kwa vile wanavyoandika kwenye mitandao ya kijamii, kwa hali hiyo waajiri kama serikali na makampuni huhakiki sana watu kabla hawajawaajiri kuwa ni wema.

   3.Usipige picha za ajabu na zisizona maadili.
Hili wote tulishuhudia pale muheshimiwa alipoteua wanawake kadhaa na pindi tuu walipoingia ofisini ghafla picha zao za ajabu zikaibuka mitandaoni zikiwachafua wao na muheshimiwa kwa ujumla akishushiwa hadhi yake.

   4.Usipende kuandika taarifa zinazoonyesha mahali ulipo.
Ni vyema kushare mahali ulipo kama ni pazuri lakini kumbuka kuna waovu wengi wanaweza kuchukulia hiyo kama nafasi ya kukufanyia uhalifu wewe au familia yako ulipoiacha...hizi ni nyakati ngumu.

   5.Usitaje majina ya watu mashuhuri au yeyote yule pale unapoandika kitu.
Sheria ya Tanzania ya mtandao ni kali sana, hata kama mamia wamemtaja wewe unashauriwa usimtaje maana huo ndio utakuwa ushahidi tosha wa kukufunga...Hili limekuwa tatizo hata tunaona muheshimiwa raisi amekuwa akikamata wengi ambao wanamtukana, hafanyi ubabe au hayuko njee ya sheria, yuko katika sheria kabisa na ana haki ya kumshtaki yeyote atakayemnenea vibaya bila kibali chake.

   6.Unapotumiwa picha chafu na mtu yeyote yule futa na umkanye huyo mtu na kama una uwezo nenda hata polisi kama utakuwa hujafuta hizo picha kama unataka huyo mtu akamatwe.

   7.Usikubali kuwa tagged katika post zozote zile za uchochezi au uchafu wowote ule.

  8.Kama una addiction au tatizo la kutumia mitandao hii bila kipimo, vunja kwa kutafuta kitu cha kuchukua nafasi yake hiyo taratibu taratibu..mfano anza kujiuliza taratibu maswali kama "Una hela za kutosha? unaenda wapi? uko wapi?" pia FANYA KAZI,  Omba Mungu akusaidie na incase ACHA UMBEA.
Kutokana na  maendeleo ya kiteknolojia, sio jambo la kuepuka tena kufanya manunuzi kwa njia mtandao wa internet, maana umejaa vitu vya thamani ndogo na vizuri lakini pia umejaa wezi.  Fuatilia haya ili uweze kufanya manunuzi bila kujutia...

  1. Fungua akaunti pekee benki ambayo itatumika kwa ajili ya matumizi hayo ya manunuzi tuu, na uweke hela tuu pale pindi unapotaka kununua vitu, tunafanya hivyo ili endapo akaunti ikafikiwa na wezi wasiweze kuiba chochote.
  2. Pata elimu ya kutosha benki juu ya kitu gani cha kulinda kuhusu taarifa zako.
  3. Nunua sehemu maarufu au kwenye tovuti zinazofahamika dunia nzima kwa manunuzi mfano...GooglePlay, Amazon,eBay na alibaba.
  4. Usimtumie mtu usiyemfahamu taarifa zako za kibenki kwa njia ya email au yeyote ile.
  5. Hakikisha katika browser yako wakati unataka kufanya manunuzi pale kwenye sehemu ya address  imeandikwa au inaanza address kwa njia hii "HTTPS://....." na sio "HTTP://...." ina maana ya kitaalamu "Hyper text transfer protocol secure"
  6. Jiridhishe ya kwamba hiyo ndio tovuti yenyewe au kuna mtu ametengeneza tovuti feki ili kukuibia taarifa zako.
  7. Ukimaliza kufanya manunuzi yako ni vyema zaidi ukafuta browsing history yako yote ili kufuta cookies zenye mabaki ya taarifa zako.
  8. Muone mtaalamu wa Ecommerce ili akusaidie unapotaka kufanya manunuzi makubwa.
Battery hutumika kuendesha umeme ndani ya laptop yako endapo pale unapokuwa hujaichomeka kwenye charge laptop yako.


Uharibifu unaofanyika.
  1. Unapotumia laptop ikiwa imechomekwa kwenye umeme siku nzima bila kuichomoa pale battery inapojaa.
  2. Unaposafiri kwa muda mrefu au kiacha laptop bila kuitumia kwa muda mrefu, na kuiacha battery ya laptop ndani ya laptop bila kuitoa.
  3. Unaponunua adapter feki ili kuchaji battery ya laptop yako.
Ufumbuzi.
  • Laptop ikijaa charge chomoa kwenye umeme na ikiisha chomeka.
  • Ukiona unasumbuka na chomeka chomoa ya hapo juu, tafuta energy management software hiyo itakusadia.
  • Unaposafiri kwa muda mrefu zaidi ya siku moja au kupanga kuto kuitumia laptop yako kwa muda mrefu, chomoa battery ya laptop na uihifadhi mahali salama.
  • Tumia vifaa au adapter original vya laptop husika vyenye meno matatu(Earth,Live and Neutral).
  • Ukiona hali inakuwa mbaya omba msaada.



Anti-Virus ni programu ambayo hutumika kuilinda kompyuta, kutoka kwa mashambulizi ya virusi ambavyo huathiri mifumo yake na uwezo wake wa kiutendaji kazi.

Jinsi Anti-virus inavyofanya kazi.
kama bodyguard anavyomlinda mtu, basi na anti-virus hulinda kompyuta kwa staili hiyo. Yenyewe huhakiki na kupitia kila kinachofanywa na kompyuta ili kuweza kujua kama kitakuwa na madhara au la!
Mfano:
Unapoingiza tuu flash yako kwenye kompyuta kabla hata hujaifungua anti virus ni ya kwanza kuleta warning kama kuna kirusi au la kwa sababu imeshaipitia kabla.

Tatizo lilipo:
Kutokana na kitendo hicho processor ya kompyuta hufanya kazi mara mbili zaidi kwa kila kitendo kinachofanyika, ya kwanza ikiwa ni kazi ya Anti virus(ukaguzi) na ya pili ikiwa ni kazi ya Operating system(windows) ya kumhudumia mtumiaji matakwa yake.

kwa hali hiyo anti virus kubwa zenye nguvu kama karspesky, avg, avast huhitaji uwezo mkubwa zaidi wa ukokotoaji ili ziweze kufanya kazi na kompyuta na endapo uwezo wa kompyuta ni mdogo, hapo husababisha kompyuta kufanya kazi kwa utaratibu na hata husababisha ukwamaji(stucking) wa kompyuta ikiwa inafanya kazi mara kwa mara.

Ushauri.
kwa matumizi ya sasa unashauriwa kuongeza uwezo wako wa kompyuta mpaka kufikia RAM=4GB na zaidi muone mtaalamu wa tehama ili aweze kukusaidia kusimamia matumizi mazuri ya diski yako inayobeba Operating system iwe na nafasi ya kutosha.
Je ni nani mwenye kiwanda hichi? na ni kwa nini Rwanda, je kompyuta hizi zina uwezo gani?

Soma zaidi.. Rwanda ni kati ya nchi zinazokua kiuchumi kwa kasi hapa katika Afrika Mashariki na miaka ya hivi karibuni imeanzisha utengenezwaji wa kompyuta, kwa kusaini mkataba na kuiruhusu kampuni ya POSITIVO BGH kuweza kuanza utengenezaji wa kompyuta nchini mwake.

POSITIVO BGH  ni muunganiko wa kampuni 2 kubwa, kutoka Amerika ya kusini, ambazo ni POSITIVO yenye makao yako nchini Brazil na BGH yenye makao yake Argentina, kampuni zilianza tangia muda kufanya biashara kwa kuungana na katika moja ya mipango yake ziliamua kuanzisha kiwanda Afrika ili kupanua soko lake.

Kwa nini Rwanda?
Kutokana na maelezo ya Juan Ponelli, Rais wa POSITIVO Afrika, Rwanda imeonesha juhudi kubwa za kusaka maendeleo na pia ina GDP nzuri ya 8.8% ukilinganisha na nchi nyingine hapa Afrika na pia ina utulivu wa kutosha...soma zaidi

Hii ni mojawapo ya kompyuta zinazotengenezwa..

Positivo BGH 11CLE2-R

Specifications
OS: Windows 8.1 Pro
Processor: Intel® Celeron® N2840
Platform: Bay Trail
RAM Memory: 2 GB
Storage: 320 GB
Screen: 11,6"
Camera: 1 Mpx HD
Video: Intel® HD Graphics; DirectX 11
Audio: High Definition
Ports: VGA y HDMI
Memory Reader: 9-in-1 memory multi reader
Security: Kensington port


Kompyuta ni kama yalivyo magari, yanatembea na ya na kimbi lakini yanatofautiana na yana hadhi na uwezo tofauti kulingana na mtengenezaji.
Kwanza nakupa aina ya kompyuta pamoja na matumizi yanayofaa zaidi.
LAPTOP VS DESKTOP
  • Unashauriwa kutumia desktop maofisini kwa sababu zifuatazo za kiulinzi na za kiusalama, kwani ni rahisi kwa laptop kuibwa na nyaraka nyingi kupotea au kuibiwa kuliko desktop, na pia kompyuta ya desktop  ina uwezo mkubwa sana ukilinganisha na kompyuta ya laptop.
  • Unashauriwa kutumia laptop kama ni mfanyabiashara au mwanafunzi,kwa sababu ya wewe kuhitajika kutembea mara kwa mara na kompyuta yako ila inakupasa kuwa na desktop au external hard drive,  mahali ili kuweza kuwa na back up ya data zako.
MAKAMPUNI YA KOMPYUTA NA SIFA ZAKE
HPa.
Kompyuta hizi zina uimara mkubwa sana na hudumu kwa muda mrefu sana,pia zina hali ya juu ya utendaji na mara nyingi hutumiwa kwakazi zinazohitaji ukokotoaji mkubwa. Pia hutumika katika kwenye tasnia ya uhandisi na hata designing.

DELLa
 Kompyuta hizi zina sifa ya ubora sana zaidi husifika kwa kioo(monitor) chake kizuri sana cha HD(High definition) amabcho ni kizuri kuliko vya computer nyingine.

Kompyuta hizi hutumika sana maofisini na hata kwa kujiliwaza kwa kuangalia videos kutokana na ubora wa kioo chake.

LENOVOr
Kompyuta hizi zinasifika kwa kuishi kwa muda mrefu kama ikitumika kwa matumizi ya kawaida, yaani yasiyo hitaji ukokotoaji wa hali ya juu.,kama kuangalia movies sana na kucheza michezo kama fifa, magari.

APPLEs
Kompyuta hizi zina ubora wa hali ya juu pamoja na uwezo mkubwa sana na pia hudumu kwa muda mrefu. Katika USALAMA haziingiwi na virus kama kompyuta nyingine na ikitokea vimeingia ni mara chache sana. UTENDAJI wake ni mkubwa maana zina nguvu kubwa za ukokotoaji. Pia ni rahisi kubeba kwa maana ni nyembamba na nyepesi kubeba.

MUHIMU 
Nimejaribu kukupa mwanga kuhusu makampuni haya, haimaanishi mapungufu haya utayakuta katika kompyuta zao zote, kwa maana hushughulika kila siku kuweza kurekebisha mapungufu hayo. Ni bora kununua kompyuta za toleo jipya kuweza kuepukana na shida zozote..


 

Fuatilia kwa umakini mambo haya ili usije ukapoteza hela yako bure au kupata kompyuta isiyolingana na mahitaji yako.
MATUMIZI
Kwa matumizi ya kiofisi ,kama kuandika (microsoft word)  na kutumia spreadsheet(excel),intaneti na kusoma barua pepe unapaswa kununua kompyuta yenye uwezo mdogo hadi yenye uwezo wa kati:
vipimo:
RAM=2GB-4GB
Processor= 1.8-2.0 Ghz 
Architecture= 32Bit.

Kwa matumizi ya kujiliwaza(Entertainment) mfano kucheza michezo kama mpira(FIFA) magari,au kwa matumizi ya kudesign hii unahitaji kompyuta yenye uwezo mkubwa:
Vipimo:
RAM=4GB-8GB
Processor=2.5Ghz--> Nakuendelea, Dual-->na Kuendelea
Architecture= 64Bit.

VIFAA VINAVYOAMBATANA NA KOMPYUTA.
Ni muhimu sana kuhakikisha vifaa kama adapter vinavyokuja na kompyuta kama vimetengenezwa na mtengenezaji halisi wa kompyuta hiyo na ni original! Unapokuwa unapewa Vifaa hivyo hakiki kama vimeandikwa jina la mtengenezaji wa kompyuta hiyo mfano HP na adapter yake iandikwe HP na hata muonekano wake uwe unaridhisha machoni ya kwamba ni original ukijimuisha uzito wake pia. 

HAKIKI UKUBWA WA HARD DRIVE, RAM NA PROCESSOR .
hakikisha kompyuta inapowashwa inaonesha ukubwa halisi kama ulivyoandikwa kwenye vitabu vyake au kama mlivyokubaliana na muuzaji. Ili usidanganywe, inapowashwa kompyuta pale kwenye desktop right-click computer halafu chagua properties hapo utaweza kuona ukubwa wa vitu hivyo.

NENDA MAHALI PANAPO AMINIKA KWA UUZAJI WA VITU ORIGINAL.
Usijaribu kununua kompyuta maeneo ambayo yamezoeleka kwa wizi kwa maana , kuna mambo mengi ambayo mtu mwingine hawezi kukagua zaidi ya mtaalamu wa Tehama. Na kama utahitajika kununua huko tafadhali nenda na mtaalamu wa tehama.

HAKIKI THIBITISHO(WARRANTY) YA KOMPYUTA HIYO.
Kama kompyuta ni mpya ni lazima na muhimu iwe na thibitisho hata la kuanzia mwaka mmoja(1) na ikipungua sana napo haishauriwi mwisho miezi sita(6).

USIJARIBU KUNUNUA KOMPYUTA MPYA KUTOKA KWA MTU AU KOMPYUTA YENYE UWEZO MKUBWA KWA GHARAMA NDOGO.
Kuwa makini kizuri chajiuza kibaya chajitembeza. Unapoona kompyuta yenye uwezo mkubwa kwa gharama ndogo usinunue mpaka umeipeleka kwa mtaalamu aihakiki kama ni nzima.

Imeandaliwa na 
Elisante Shibanda.
 
Usipate tabu tena, jifunze computer kwa lugha ya asili yako,lugha unayoielewa, Lugha ya Kiswahili.
Hii ni zawadi kutoka ECL Computer Clinic bure kabisa na wewe ufahamu kutumia computer. Furahia zawadi hii.Soma Kitabu hapa