Showing posts with label interview. Show all posts
Showing posts with label interview. Show all posts


Interview za mchujo ni interview za awali, ambazo hutumika kupunguza watu wengi walioomba kazi husika,

ili wabaki wachache kwa ajili ya hatua ya pili ya interview(usaili).
Interview hizi zina sifa kubwa sana ya kuvunja mioyo ya watu walioomba kazi, kwa watu wengi hujikuta wamejiandaa visivyo na kufanya vibaya.



Hebu kwanza tufahamu mambo ya kuzingatia unavyojiandaa na interview.


Muombe Mungu akusaidie kujibu kwa ufasaha, maana ni rahisi sana kujibu visivyo, pamoja ya kuwa unajua kila kitu.



Fahamu kwa undani kazi iliyotangazwa. Ni rahisi kusema, mimi nimesoma chuo kama IT, Computer science N.K na ndio maana kozi yangu imeorodhoshwa na nikaitwa, 
ila kufikiri huko sio sahihi na wengi hufeli maswali yanayohusiana na kazi hiyo. 
Fanya utafiti wa hali ya juu kwenye mtandao au kwa waliokwisha fanya teyari na uelewe.

kozi za IT Tanzania na Soko lake

Fahamu majukumu yaliyotangazwa na kazi husika na uhakikishe unayafahamu jinsi ya kuyatekeleza yote
au kama ukishidwa yote angalau ujue nini kinaendelea,     kwa maana maswali mengine hulenga humo.


Fahamu ni masomo/kozi gani yanayoendana na kazi husika,uliyoyasoma chuoni, halafu uyapitie kwa umakini.



MIUNDO YA MASWALI YA INTERVIEW(USAILI)

Muundo wa 1

Muundo huu utakutana na maswali 40 hadi 50, yanayokuwa ya kuchagua, na huwa yanagusa sehemu mbali mbali, ila zaidi sehemu zinazohusiana na kazi husika na sub course husika mojawapo huonekana kwa wingi.

Mfano:
Kazi ya Business analyst, maswali mengi asilimia 60-70 yatakuwa ya software engineering.

Jinsi ya kujiandaa:
Tafuta subcourse husika na uisome sana gusia maeneo mengine pia.

Muundo wa 2

Muundo huwa na maswali 4 hadi 5, ila maswali huwa yanalenga maeneo husika na yale ya kuzunguka.

Mfano:
System Administrator, maswali 2 yatahusiana na Networking lakini 2 mengine yawaweza kugusa database na hardware.

Jinsi ya kujiandaa:
Soma yote yanayoendana na kozi husika na course zinazoendana na hiyo course.

Muundo wa 3

Muundo huu una maswali 4 hadi 5, na maswali hugusa course husika tuu na huulizwa kwa mfumo wa maswali ya scenario.
Mfano:
System Administrator, maswali yote ni ya networking, na yanaulizwa yakitakiwa kujibiwa kitaalamu na sio kitaaluma
Namaanisha kitaalumu ujibu kama mtu mwenye ujuzi na scenario hiyo  na sio kama mtu aliyakariri kutoka kwenye kitabu. 

Jinsi ya kujiandaa:
kama una uzoefu kumbuka uzoefu wako, kama una mafunzo ya certifications yatumie ipasavyo, lakni kama huna hivyo vyote usijali jiandae vyema na sub course husika nawe utafanikiwa.

Muundo wa 4

Muundo huu huwa na maswali 4 hadi 5, ambayo hujikita zaidi kitaalamu na katika majukumu yaliyorodheshwa na tangazo la kazi.

Jinsi ya Kujiandaa:
Soma kwa umakini yale majukumu ujue jinsi ya kuyatimiliza kivitendo kila moja na kama kuna vigezo vipitie hata ujue tuu kwa mbali nini kinaendelea.

Angalizo:
Ni kawaida kabisa kumaliza mtihani huu usijue kama umefaulu au umefeli, na hali hii huifanya ionekane ngumu sana, ila kabla ya kujibu swali tafakari linahitaji nini na ujibu vizuri ukujibu juu juu uamini kuna watu watajibu kwa umakini kuliko wewe.


Hiyo ni muundo ambayo imekuwapo ila inaweza badilika muda wowote hata kesho ikaja mengine zaidi, na sijakugusia interview za awamu ya pili na za mahojiano,ila kwa hayo chukua hatua, na nikutakie interview njema.
Kwa ushauri zaidi wasiliana nami 


Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   






Fahamu Business Analyst ni nani? 
na nini kinahitajika ili kuwa Business Analyst,
ili uweze kufahamu 
kama je una muhitaji mtu kama huyu katika biashara yako au 
ujiandaaje kufanya interview ya nafasi ya Business Analyst na zaidi 
unafanyaje kujiboresha zaidi kama wewe ni Business Analyst.

Business Analyst Ni Nani?

Business Analyst ni mtaalamu ambaye anahusika katika kuisaidia biashara 
kutumia teknolojia kwa gharama nafuu, 
ili kuboresha mfumo wa biashara uweze kuipatia kampuni faida kubwa zaidi.

Chimbuko lao

Hii kazi ilianza kuchukua nafasi kubwa katika karne ya 21, wakiwa na kazi moja kubwa 
ya kuunganisha teknolojia 
iliyopo na utimizaji wa malengo ya kampuni husika.

Kazi yao

Kuleta ufanisi katika uendeshaji wa biashara.

Huhusika katika kupanga mipango mbali na kufuatilia mipango hiyo kwa umakini.


Kufuatilia mahitaji yanayojitokeza siku hadi siku katika uendeshaji wa biashara.


Kuboresha mfumo wa uendeshaji uliokowapo ili ufanye kazi kwa ufanisi zaidi.


Kutafuta majibu ya kiteknolojia juu ya changamoto zote katika mfumo wa uendeshaji wa biashara.


Sifa za kuwa Business Analyst

Uwezo wa kuwasiliana vizuri kwa njia ya kuandika na kuongea, kawaida na kitaalamu zaidi.

Uelewa wa mambo kadha yanayohusu software engineering.

Uwezo wa kufanya cost/benefit analysis.

Uwezo wa kufanya Business Case development

Uwezo wa kutumia modeling techniques 

Uongozi.

Elimu na Mafunzo ya Business Analyst

Kazi hii huwa inahitaji zaidi digrii ya Information technology, Computer Science au Software Engineering na kozi zinazolingana na zilizotajwa hapo juu.

Halafu unatakiwa ila sio lazima upate mafunzo zaidi(Certifications) kama IIBA and CBAP ila ukiwa na hizo   digrii hapo juu unafaa kuanza kazi. 


Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   
Kwa maswali zaidi wasiliana nasi.

Fanya Maandalizi ya Kutosha, ili uweze kufanikiwa na hatimaye kupata kazi kama System Administrator.

Mambo ya Kuzingatia.

👉Uwe umesoma IT au Computer Science au 
  una Elimu ya mambo hayo,  

kwa maana vitu kadhaa ambavyo vinahitajika humo vilishafundishwa katika kozi hizo.




👉Uwe umejiongeza mwenyewe binafsi na unafahamu fika,
nini kinaendelea katika nafasi hiyo, 
kwa maana wewe unahusika na usalama wa taarifa 



nyeti za kampuni na muundo mbinu yote ya Tehama.


👉Itafaa zaidi kama utakuwa una vyeti vya CISCO au Microsoft,



Ili uwaaminishe watu yakuwa wewe unaweza ukaihudumia vizuri mitambo ya IT. Ukitaka kujua ni zipi soma article yangu ya certifications hapa...


👉Cha mwisho lakini cha muhimu sana, jifunze Linux, 



ni muhimu hata Microsoft katika server zake nyeti anatumia Linux.


Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   


Hayo yalikuwa, kutoka kwangu kama IT Consultant.

Yafuatayo yatakusaidia kukuandaa zaidi katika Interview yako....Mungu akusaidie.

Kwa mambo ya kujisomea binafsi, maswali na majibu kwa interview ya kuandika(written)

Link hii hapa...

Kwa mambo ya kujisomea binafsi, maswali na majibu kwa interview ya Kuongea(oral)

Link hii hapa...


Angalia hii video kukubrush na kazi ya System Administration



Hii Video ya pili itakupa kujiamini katika maswali utakayoulizwa...




Kwa ushauri zaidi, wasiliana nami katika elisanteshibanda@yahoo.com.
Interview Njema.