Showing posts with label computer science. Show all posts
Showing posts with label computer science. Show all posts

Imekuwa ni jambo la kawaida huku mavyuoni kutenganisha ajira na masomo, 
haswa katika vyuo vyetu hapa Tanzania, 
kiasi ambacho tumekuwa na tatizo kubwa la ukosefu wa ajira,
 ambalo ukilatazama kwa umakini kuna uwezo fulani wahitimu wanakosa ndio maana, tatizo linakuwa kubwa mno. 
Lakini pia kuna sababu za msingi tuu ambazo ni za kiuchumi ambazo hata wahitimu hawahusiki ambazo zinakuza tatizo hili.

Kwa upande wa Information Technology na kozi zote zinazoendana na hiyo kozi, 

kuna vitu vifuatavyo ambavyo mwanafunzi akivifanya vinaweza fungua njia au 
kupanua wigo wako wa ajira kwa kiasi kikubwa sana. 


GPA/ UFAULU CHUONI

Huu ni ufaulu wako chuoni, najua ninavyozungumza hivi kwa wingine ni kama kuwaambia wanywe maji ya sumu, ila ndugu zangu hakuna jinsi, 
 GPA ina faida kwanza GPA kubwa inachangia kwa kiasi kukuitisha katika interview ya kazi,

kwa maana inaonesha una uelewa mkubwa na inaonesha kwa kiasi unaweza chapa kazi,
kama ulisoma kwa bidii kwa kiasi hicho basi unaweza ukawa na bidii hata kazini.

Lakini pia mavyuoni tunahitaji wahadhiri na kigezo kikubwa ni GPA ndio utaitwa kwenye interview za huko na hata watu wanaoomba ni wachache sana.
GPA nzuri huanzia 3.5 na kuendelea ila vyuoni ajira zake inategemea huwa inaweza anzia 3.5 wakati mwingine 3.8.


PROFESSIONAL CERTIFICATIONS/ VYETI VYA UTAALAMU.

Hivi ni vyeti vya kitaalamu yaani kubobea katika sehemu fulani, 
hivi havikupi degree au diploma, ila inapewa hadhi ya kuwa mtaalamu katika eneo moja tuu la IT mablo linaweza likawa sio kubwa. 


Mfano 
ukitaka kubobea kwenye networking lazima upitie CCNA Certifications, MCSA na kadhalika. 
Katika kazi kama za System Administrator bila vyeti kama hivi kuapply ni kazi bure na hata kama ukiitwa mitihani inaweza kukushinda kwa ugumu wake. 



SKILLS/UJUZI BINAFSI

 Katika maswala ya IT, swali halipo sana unamefundishwa nini
 ila lipo katika unaweza kufanya nini 
na unajua nini?


Hakuna muda mzuri wa kujifunza lugha mbali mbali za computer 
na kujua jinsi ya kuzitumia kama muda huo, 
maana kuna kujiajiri kwingi sana huko na hata serikali na mashirika,
yanatafuta watu wa kutengeneza software  mbali mbali.
Mfano wa lugha za kujifunza ni Android, Java, HTML, PHP,Javascript, CSS, Ruby, Python N.K.
Na pia uwezo binafsi wa kutengeneza programs peke yako, websites, blogs N.K

PUBLIC WORKING PROJECTS/Project ambazo umefanya na bado zinafanya kazi.

Tofauti ya elimu ya vyuo vyetu na vyuo vya njee,
ni kwamba mkazo uliokuwepo upo kwenye projects au practical,
ni mkubwa sana ukilinganisha na hapa ambao upo kwenye nadharia zaidi. 

Kwa hiyo hakikisha projects unayofanya inatatua matatizo ya jamii.
Hiyo hata kwenye interview sehemu ya projects inaweza mvutia HR kukuita.


IMPORTANT INTERNSHIP EXPERIENCE/MAFUNZO YA VITENDO YENYE TIJA.

Unapofika muda wa kutafuta field usifanye mzaha, tafuta makampuni ya kiteknolojia, ili ijifunze jinsi yanavyofanya kazi na hata kupata kazi kwenye makampuni mengine itakuwa rahisi kwa maana mzigo wa kuku train utakuwa umepungua.


Hayo ni maeneo muhimu ambayo ukiyashughulikia vizuri hautapoteza muda mwingi kutafuta ajira, kama hali itakuwa shwari ya uchumi.
Kwa ushauri zaidi wasiliana nami,


Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   

elisanteshibanda@yahoo.com







Katika Upande wa Elimu ya juu, ni vizuri kupata ushauri bora kabla hujaenda kujiunga na chuo chochote.
Kwa maana uamuzi wako huo utaamua mambo yafuatayo katika maisha yako...




JINSI YA KUSOMA IT: Mwongozo kwa Wanafunzi Waliofeli Form Four, 2024

KIPATO CHAKO BINAFSI
Kozi hii ya IT, Kichwa chako ni ofisi yako, kwa hiyo kama utapata elimu mbovu,utapoteza uwezo wako wa kujiajiri na unaweza ishia pabaya.


AJIRA
Interviews za kazi hizi za IT, sio nyepesi, na kwa hali hii itakushinda kushindana na watu waliofundishwa vyema na kuwa wazuri katika maeneo muhimu ya Information Technology.

MCHANGO WAKO KWA TAIFA
Kozi hii au profession hiii au kazi hii ya IT ina mzigo mkubwa katika taifa hili changa kiteknolojia.
Kuna matatizo katika jamii ambayo yanahitaji kutatuliwa kidigitali,kwa sababu hii kama utakuwa na elimu mbovu,

utakuwa mmoja wa walalamikaji badala ya wabunifu na watatuaji matatizo.



VIGEZO VYA CHUO BORA KATIKA IT
Vifuatavyo ni mojawapo ya vigezo muhimu,ila vinaweza vikawepo vingine zaidi.




UBUNIFU UNAOFANYA KAZI
katika mavyuo mengi sikatai kama kuna ubunifu ila mwingi unaishia kwenye makaratasi ya chuo na kutupwa stoo(store). 
Ubunifu hujulikana kwa project ambazo zinavuka mipaka ya chuo na kuifikia jamii.

UFUATILIAJI WA CHUO KWA PROJECT ZA WANAFUNZI.
Kuna mavyuo yanaongoza kwa kutupa store project za wanafunzi lakini pia kutokuchukulia kwa umakini project zinazofanywa na wanafunzi, kiasi kwamba wanafunzi wako huru kuforge project zao na chuo kuzipokea tuu kwa kutokujali ya kwamba hii project imefanyika au laa. 

ASILIMIA YA VITENDO KATIKA ELIMU INAYOTOLEWA.
Ni muhimu kwa chuo kuwa na asilimia kubwa sana ya vitendo kuliko nadharia

VIFAA VYA KUJIFUNZIA IT
Ni muhimu kusoma  kwenye chuo chenye vifaa vya kutosha ili ujue haswa nini kinaendelea makazini ila ni kwa  asilimia ndogo hii pointi ina umuhimu maana IT inakuwa kwa kasi na Vyuo vya haviwezi kuwa na vifaa vya kisasa kila wakati.


"Chuo kinaweza kumtengeneza mhitimu wa IT,ila ni jukumu la mwanafunzi binafsi akiwa chuoni, kutoka chuoni kama mtaalamu,na sio mhitimu pekee kwa maana wahitimu hupata shida sana kutafuta ajira wakati wataalamu hutafutwa na ajira na pia hujiajiri."




Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na magroup ya Whatsapp ya MAXPO Tanzania  Maximize your potential   


VIFUATAVYO NI VYUO BORA KUJIFUNZA IT  TANZANIA.
 1. Dar es salaam Institute of Technology (DIT)

2. St. Joseph University in Tanzania.

3.University of Dar es Salaam.

4. University of Dodoma



Kwa kumalizia, vyuo vipo vingi na wanafunzi wanazidiana uwezo 
kwa hiyo inawezekana ubunifu wa hali ya juu ukatokea kwenye chuo ambacho hakipo hata kwenye list hii, 
na pia vyuo vingine vinaweza vikaboresha ufundishaji wake na kuvipiku vyuo vilivyopo sasa.

Na la muhimu college za IT zipo nyingi na kwenye mikoa mingi, kwa hiyo kukosa nafasi kwenye vyuo hapo juu haimaanishi IT yako umeitupa, ila ina maana wewe ndio wa kukin'garisha chuo ulichokuwepo.




Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na magroup ya Whatsapp ya MAXPO Tanzania Maximize your potential  


 





Fahamu kitovu cha teknolojia( Technology Hub) hapa Tanzania ambacho wanafunzi wa chuo na wataalamu katika nyanja mbali mbali za teknolojia yaani Software developers, Web developers, Electricians, Electronics Engineers and Computer Engineers n.k hukutanika na kuvumbua au kuboresha vitu.

Kitovu cha teknolojia au kwa lugha ya kiingereza technology hub ni sehemu ambazo huanzishwa kwa malengo ya uvumbuzi na utatuzi wa matatizo kwa nji ya teknolojia. 


Kwa Afrika, sehemu hizi zimefikia 314 katika miji 93 katika inchi 42 nchi kama South Afrika ikiwa inaongeza kuwa na vitovu vingi.

Kwa hapa Tanzania, tuna kitovu cha teknolojia kimoja ambacho kinaitwa Buni Hub.

BUNI Hub.
Buni huhusika zaidi na kuwasaidia wanafunzi hata watu wabunifu katika teknolojia kwa kuwapa ushauri(mentoring) na kuwaongoza kupata uwezo wa kufanya ujasiriamali kwa kupitia teknolojia n.k.


BUNI huwa inaendesha semina, mafunzo mafupi mara kwa mara ili kuweza kuwajenga wanachama wake katika uanzishwaji wa project na hata usimamizi wa project hizo za kitaalamu na kuwaongoza waweze kufikia malengo yao.
Kwa maelezo zaidi tembelea tovuti ya BUNI hapa na wasiliana nao kuweza kujiunga. 

MANUFAA YA KUJIUNGA.
Utajenga uwezo wako binafsi katika kubuni mambo mbali mbali ya kiteknolojia.


Utakutanishwa na watu ambao wana mawazo kama yako ambao watakusaidia kusimama vizuri zaidi.

Ni sehemu ambayo inaweza ikawa uwanda wa wewe kuelewa njia ya kupata hata ufadhili wa kazi yako. 

Muhimu zaidi chochote ambacho hutumii kitapotea na kama wewe ni mwanafunzi wa IT,au kozi zozote za science ni muhimu kuwa pamoja na watu ambao wana elimu kama yako ili elimu yako isije ikalala na ukaanza kufakamia fani za watu wengine.

Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   

Ulimwengu wa teknolojia ya mtandao yaani Information technology ni mkubwa sana, na  wengi huwa wanajikuta wanashindwa kufikia malengpo yao, kwa  kushindwa kujua tofauti ya kozi zilizopo, hebu fuatilia uelewe kipi ni kipi?

Information Technology

Hii ni kozi ambayo inadili zaidi na mawasiliano ya njia ya kompyuta na uendeshaji wa mifumo/systems ya kompyuta na hata designing. 

kozi hii hutoa watu/professionals ambao ni system administrators,ICT officers, Graphics Designers etc 


watu ambao wapo kwa ajili ya kuwasaidia watu wengine kuweza kutumia vizuri, mifumo ya kompyuta.

Kazi.

Hawa watu wengi huwa wanaajiriwa, 

zaidi ila pia wanaweza kuajiajili kwa katika kufanya maintenance ya vifaa vya ICT, ICT Equipment supply, 

na hata kufunga mifumo ya network sehemu mbali mbali na akijiendeleza huweza kuwa Webmaster wa tovuti mbali mbali.

Kipato.

Mishahara yao hulipwa kulingana na elimu ya Degree au ya diploma aliyonayo kama fani nyingine na Zaidi ikizingatia kazi anayofanya na unyeti wa kazi hiyo.



Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   

Computer science.

Uwanda huu upo ndani zaidi kuliko IT, maana hawa watu mbali na kujua vitu vyote vya kozi ya IT,


pia huweza kujua kutengeneza program za aina mbali mbali za computer, na pia hufundishwa lugha nyingi za computer na huwa wako vizuri kiasi hata kwenye hardware ya computer.

Kazi.

Hawa watu utawakuta kama pia ma system administrators, business analysts, system analysts, ICT Officers, Application programmers, software developers. 

Pia wengi hujiajiari na kuanzisha makampuni/biashara za kutengeneza kompyuta hardware na software, 
websites na kazi nyinginezo nyingi katika uwanda wa technology.

Kipato

Wanapoajiriwa kipato chao hakitofautiani na IT.

Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   

Computer Engineering

Fani hii, hujikita Zaidi na hardware ya computer, huku tunapata watu ambao wanaunda vifaa ambavyo vinaweza fanya kazi na mifumo ya computer. 

Hawa kwa nchi zenye viwanda vya kutengeneza vifaa hivyo,  huwa ni soko kubwa sana, 

ila kwa nchi ambazo zinaendelea huwa bado wana soko dogo sana, na hata huogopwa kuajiriwa kulingana na Title yao ya Kuwa engineer.

Kazi.

Hawa hufanya kazi ya kutengeneza vifaa ila pia huweza kufanya kazi nyingi ambazo mtu wa computer science anafanya, 
pia ni mafundi waliobobea katika kurekebisha computer mbovu.

Kipato

Hawa huwa na mshahara wa juu kuliko IT na Computer Science, maana hulipwa katika kiwango cha ma engineers,

 lakini pia hufungua biashara kubwa za computer maintenance na hardware Suppliers na zaidi...
  

Software engineering

Katika Fani hii tunakutana na watu ambao wanataka kubobea katika kutengeneza programu za computer, 

hawa watadeal na program tuu na kidgo sana mambo mengine katika fani ya teknolojia.


Kazi.

Hawa hufanya kazi kutengeneza program za kila aina, pia huingia kwenye network na kubobea humo,

na huwa pia kuweza kufanya kazi za Computer Science kwa kiasi na hukinzana kabisa na computer engineers maana wao hufanya kazi na hardware.

Kipato

Hawa wana mshahara mkubwa wa kiwango cha Engineer kama computer engineer anavyolipwa na pia huwa wanajiajiri sana na kuanzisha makampuni ya kutengeneza programu.

 

Jinsi ya Kujiendeleza…

Ulimwengu wa Computer umejaa vyeti vya mafunzo mbali, 

ili mtu abobee katika sehemu maalumu hizo huitwa certifications mfano mafunzo ya Network hutoa vyeti,

kama CCNA, CCNP na kuendelea na mafunzo ya database kama Oracle , na hata auditing(Ukaguzi) kwa maelezo Zaidi fuatilia article yangu ya kuhusu certications za IT.


Lakini pia anaweza jiendeleza katika masters degree za vitu mbali na hata kuwa Tutorial au lecturer au professor maana bado kuna upungufu mkubwa mno katika ngazi hizo.

Kwa muongozo zaidi, Wasiliana nami katika email elisanteshibanda@yahoo.com au

Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa