Showing posts with label Information technology. Show all posts
Showing posts with label Information technology. Show all posts

Tehama(Information technology) Katika nchi za chini ya jangwa la Sahara, Afrika Mashariki bado ni changa sana. Na kama inavyofahamika teknolojia hurahisisha sana maisha na hupunguza mzigo mkubwa wa kazi kwa watu.

GUNIA ZITO.

Nimeifananisha na gunia zito kwa sababu kutengeneza teknolojia mbadala ili kuweza kutatua changamoto katika jamii inahitaji mafunzo, moyo wa kujitoa binafsi na jitihada zaidi.

Lakini pia inahitaji macho ya kuona hizo fursa katika jamii ili uweze kuzifanyia kazi. Watu wengi hukimbilia kazi ambazo hazihitaji sana ubunifu lakini huku ubunifu ndio mahali pake, pindi unapokosa akili za  ubunifu basi utashindwa kufanya lolote katika tehama.

LENYE PESA

Kama nilivyoeleza hapo mwanzo, pindi teknolojia hizi zinapotengenezwa na wataalamu, huingia sokoni na kurahisisha maisha ya wengi.
watu wengi, makampuni mengi na watu wengi yametajirika sana duniani kwa tehama, mfano 

kampuni kubwa zaidi ya Tax duniani haimiliki tax hata moja bali imeunganisha wamiliki wa Tax,
lakini tatizo waliloliona ni shida ya kupata Tax pale ambapo unaihitaji na haupo barabarani. 

UBER  kwa sasa inaingiza mabilioni ya Pesa duniani kote, hata hapa Tanzania zipo programu kama za mpesa, tigopesa zinaingiza pesa nyingi mno, 

zipo programu za vituo vya mafuta kama Petronite

zipo programu za maduka kama duka pro,

na programu za masomo kama thL na kadhalika na kadhalika...

JINSI YA KUWA MMOJAWAPO WA WABEBAJI.

1. Uwe na uwezo kujifunza kwa bidii sana, na kukuballi kutatua changamoto mbali mbali hata zisizolipa kwa muda huo.

2. Chukua masomo ya Tehama kuanzia ngazi mbali mbali kama cheti, diploma au degree.

3. Ikiwa huna vigezo, basi ujue kusoma na kuandika kiingereza vizuri na uwe na moyo wa kishujaa wa kusoma zaidi ya wale wanaosoma darasani ila ni lazima utafanikiwa.

Janga la ukosefu wa ajira haliwezi kuisha kama tutaendelea kusaka watu kutoka njee wafungue makampuni ndio tuajiriwe ila tuu kama sisi wenyewe tutakapoamua kutoka na kugeuza changamoto kuwa mtaji wetu.


Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   
au elisanteshibanda@yahoo.com








Tehama(Information Technology), imejaa fursa nyingi, na katika nchi zetu changa, fursa ni nyingi mno.

Katika Tehama juhudi za mtu binafsi na Mungu wake, ndio zitamfanya afinikiwe au asifanikiwe.

Mtaji wa Tehama ni computer tuu, ambayo ni gharama ndogo sana kuipata.

Ni vitu gani mtu anaweza soma/jifunza ili afanikiwe katika Tehama.

Graphics Design(Sanaa ya Matangazo)
Hii ni sanaa ya matangazo ya biashara. Hakuna biashara duniani isiyotaka matangazo

na ukiangalia dunia ya leo, tumezungukwa na matangazo, yanazidi kuwepo na jinsi biashara zinavyozidi kuongezeka kasi ya uhitaji wa matangazo inazidi kuongezeka.

Jinsi ya Kujifunza
@ Chukua kozi fupi ya wiki 6, na wewe utaweza kuwa vizuri kwenye sanaa hii. 
Vigezo: Kuanzia Form Four Leaver
Price: 300,000Tsh
Training: MAXPO training
Mahali: Rains Technologies, Ilala Bungoni, Chunya str.

@Tumia njia ya Video ya kujifunza, kwa kutumia mitandao kama Youtube.






Web Development
Huu ni utaalamu wa kutengeneza tovuti mfano wa tovuti ni kama cnn.com, bbc.co.uk n.k 
Kila biashara inavyokua na kutaka kupita mipaka ya kiwilaya, kimkoa au kitaifa inahitaji tovuti kwa ulazima. Maana tovuti ni ofisi pekee ya kampuni ambayo inaweza fikiwa na mteja ,
Akiwa kokote kule duniani.

Kwa kuangalia uchumi wetu unavyokua na ongezeko la makampuni soko la tovuti litaongezeka maradufu.




Jinsi ya kujifunza
@Chukua kozi fupi ya wiki 8, ujifunze kutengeneza tovuti.
Training: MAXPO Training
Bei: 400,000/-Tsh
Mahali: Rains Technologies, Ilala Bungoni, Chunya str.

@Chukua certificate in InformationTechnology/Diploma/Degree kwa mwaka 1, 2, 3 N.k
Mahali: University of Dar es salaam Computing Centre
Vigezo: Tembelea chuoni.

@Tumia mafunzo ya vitabu na video za kwenye mtandao ili kujifunza kutoka kwa watu mbali mbali.


Computer Application
Kozi hii inakuweza kuifahamu computer ndani na njee, kuendesha stationery, na hata kutumia computer ya windows 10 na Apple computer(MAC OS) kama mtaalam.


Lakini pia inakupa uwezo wa kujifunza microsoft office yote.
Pamoja computer networks.

Jinsi ya kujifunza
@Chukua kozi fupi  ya wiki 4 ya Computer application.
Vigezo: Yeyote
Training: MAXPO Training
Bei: 250,000/-Tsh
Mahali: Rains Technologies, Ilala Bungoni, Chunya str.


@Chukua certificate /diploma/ degree katika Information Technology, computer science, ICT.
Mahali: University of Dar es salaam Computing Centre
Vigezo: Fika Chuoni.

@Tumia mtandao wa youtube kujifunza na google kupata vitabu.

Mafunzo ya Tehama, yanaanza taratibu na ni marahisi kwa mtu mwenye jitihada ya kusoma na nidhamu ya kujifunza bila kukata tamaa.
Kwa mawasiliano zaidi wasiliana nami.




Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   

au katika elisanteshibanda@yahoo.com
                  



Imekuwa ni jambo la kawaida huku mavyuoni kutenganisha ajira na masomo, 
haswa katika vyuo vyetu hapa Tanzania, 
kiasi ambacho tumekuwa na tatizo kubwa la ukosefu wa ajira,
 ambalo ukilatazama kwa umakini kuna uwezo fulani wahitimu wanakosa ndio maana, tatizo linakuwa kubwa mno. 
Lakini pia kuna sababu za msingi tuu ambazo ni za kiuchumi ambazo hata wahitimu hawahusiki ambazo zinakuza tatizo hili.

Kwa upande wa Information Technology na kozi zote zinazoendana na hiyo kozi, 

kuna vitu vifuatavyo ambavyo mwanafunzi akivifanya vinaweza fungua njia au 
kupanua wigo wako wa ajira kwa kiasi kikubwa sana. 


GPA/ UFAULU CHUONI

Huu ni ufaulu wako chuoni, najua ninavyozungumza hivi kwa wingine ni kama kuwaambia wanywe maji ya sumu, ila ndugu zangu hakuna jinsi, 
 GPA ina faida kwanza GPA kubwa inachangia kwa kiasi kukuitisha katika interview ya kazi,

kwa maana inaonesha una uelewa mkubwa na inaonesha kwa kiasi unaweza chapa kazi,
kama ulisoma kwa bidii kwa kiasi hicho basi unaweza ukawa na bidii hata kazini.

Lakini pia mavyuoni tunahitaji wahadhiri na kigezo kikubwa ni GPA ndio utaitwa kwenye interview za huko na hata watu wanaoomba ni wachache sana.
GPA nzuri huanzia 3.5 na kuendelea ila vyuoni ajira zake inategemea huwa inaweza anzia 3.5 wakati mwingine 3.8.


PROFESSIONAL CERTIFICATIONS/ VYETI VYA UTAALAMU.

Hivi ni vyeti vya kitaalamu yaani kubobea katika sehemu fulani, 
hivi havikupi degree au diploma, ila inapewa hadhi ya kuwa mtaalamu katika eneo moja tuu la IT mablo linaweza likawa sio kubwa. 


Mfano 
ukitaka kubobea kwenye networking lazima upitie CCNA Certifications, MCSA na kadhalika. 
Katika kazi kama za System Administrator bila vyeti kama hivi kuapply ni kazi bure na hata kama ukiitwa mitihani inaweza kukushinda kwa ugumu wake. 



SKILLS/UJUZI BINAFSI

 Katika maswala ya IT, swali halipo sana unamefundishwa nini
 ila lipo katika unaweza kufanya nini 
na unajua nini?


Hakuna muda mzuri wa kujifunza lugha mbali mbali za computer 
na kujua jinsi ya kuzitumia kama muda huo, 
maana kuna kujiajiri kwingi sana huko na hata serikali na mashirika,
yanatafuta watu wa kutengeneza software  mbali mbali.
Mfano wa lugha za kujifunza ni Android, Java, HTML, PHP,Javascript, CSS, Ruby, Python N.K.
Na pia uwezo binafsi wa kutengeneza programs peke yako, websites, blogs N.K

PUBLIC WORKING PROJECTS/Project ambazo umefanya na bado zinafanya kazi.

Tofauti ya elimu ya vyuo vyetu na vyuo vya njee,
ni kwamba mkazo uliokuwepo upo kwenye projects au practical,
ni mkubwa sana ukilinganisha na hapa ambao upo kwenye nadharia zaidi. 

Kwa hiyo hakikisha projects unayofanya inatatua matatizo ya jamii.
Hiyo hata kwenye interview sehemu ya projects inaweza mvutia HR kukuita.


IMPORTANT INTERNSHIP EXPERIENCE/MAFUNZO YA VITENDO YENYE TIJA.

Unapofika muda wa kutafuta field usifanye mzaha, tafuta makampuni ya kiteknolojia, ili ijifunze jinsi yanavyofanya kazi na hata kupata kazi kwenye makampuni mengine itakuwa rahisi kwa maana mzigo wa kuku train utakuwa umepungua.


Hayo ni maeneo muhimu ambayo ukiyashughulikia vizuri hautapoteza muda mwingi kutafuta ajira, kama hali itakuwa shwari ya uchumi.
Kwa ushauri zaidi wasiliana nami,


Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   

elisanteshibanda@yahoo.com





Elimu ya IT hapa Tanzania ni changa sana na imejaa ujuzi mwingi na unahitajika sana katika Taifa hili, 
ujuzi wa IT wa ngazi ya chini kabisa, unaweza ukampa mtu uwezo mkubwa tuu wa kujiajiri na  
kuendeleza maisha yake.

Zifuatazo ni kozi ambazo zinaweza kumsaidia yeyote kuwa na uwezo wa kujiajiri.


Jinsi ya kufanya kazi na kulipwa mtandaoni ukiwa Tanzania

Course in Graphics Design.

 Kozi hii itamuwezesha mwanafunzi kufanya yafuatayo;
  • Kuchora chochote kwa njia ya kompyuta.
  • Kubuni/design magazeti, vitabu,vipeperushi,kalenda n.k
  • Kutengeneza matangazo makubwa na madogo kwa ajili ya kuprint au kuweka mtandaoni.
  • Kubuni/design business cards, cover letter, cards za mialiko N.K
  • Kurekebisha picha zilizopigwa na camera kiustadi zaidi na kuboresha muonekano wake.

Course in Web Design

 

Kozi hii inajikita katika kuunda tovuti za aina mbali mbali yaani za kibiashara na binafsi, na hii itampa mwanafunzi uwezo kufanya yafuatayo.
  • Kuweza kuunda tovuti(website) na kuelewa inayoendana na tovuti.
  • Kuipandisha tovuti kwenye mtandao.
  • Kuunda tovuti za kisasa kwa njia tofauti.
  • kutengeneza mablogu(tovuti ambazo watu wanaweza kuongea humo yaani kuchat mfano hii ni blogu) ya aina zote.
  • kusajili tovuti ndani na njee ya nchi.
  

Course in Computer Administration

 


  1. Ujuzi huu utamsaidia mwanafunzi kupata uwezo wa kufanya yafuatayo;
  2. Kufahamu kompyuta na mifumo inayoendana nayo.
  3. Kufahamu Computer Hardware, yaani vifaa vyake  na jinsi inavyofanya kazi, na hata kujua jinsi ya kuitengeneza pale inapoharibika. 
  4. Kufahamu Computer software, yaani programu za kompyuta na aina zake, jinsi ya kuziweka, kuzitoa na hata kuzishughulikia na kuzitibu pale ambapo zinakuwa hazifanyi kazi vizuri.
  5. Kufahamu mfumo wa usalama wa kompyuta, jinsi ya kuilinda kompyuta  yako na mshambulizi ya kimtandao ya virusi na watu wa njee wanaokuzunguka.
  6. Kufahamu mifumo ya mawasiliano(Networks) ya kompyuta, jinsi inavyofanya kazi na jinsi ya kuifunga njia ya kuilinda pia.
  7. Kufahamu jinsi ya kutumia windows 10 na programu nyingine za kuendesha kompyuta mfano windows 8 na Linux.
             



Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na magroup ya Whatsapp ya MAXPO Tanzania  Maximize your potential   

Course in Advanced Microsoft Office

Kozi hii inamsaidia mtu kuweza kufanya shughuli zote za kiofisi kwa njia ya kompyuta, kuanzia zile nyepesi mpaka zile ngumu kufanya kwenye kompyuta.
Kozi hutoa uwezo wa kufanya yafuatayo;

Kutumia programu za microsoft office zifuatazo

        Microsoft Word
        Microsoft Powerpoint
        Microsoft Excel

Kwa kiwango cha juu kabisa katika

        Kukusanya data
        Kuchambua data
        Kupresent/wasilisha data mbele za watu
Na pia kutengeneza njia za kuingiza data na kutumia microsoft office katika biashara yako yoyote ile 

kwa  ajili ya kumbu kumbu na hata kuonyesha muelekeo wa biashara, katika mapato na matumizi. 



Kumalizia kozi zote hizi hupatikana kwenye vyuo vya kitaalamu yaani Professional colleges ambazo zimejikita tuu katika kozi hizi, 
 kuchagua chuo chenye uwezo mdgo utakupelekea kupoteza muda wako na kutoka katika kiwango kibaya.

Nakushauri chukua mafunzo ya MAXPO Tanzania, yanatolewa na Kampuni ya Rains Technologies Co LTD iliyopo Ilala, Bungoni Str/Chunya Str Dar es salaam.

 na wanakupangia ratiba kulingana na ratiba yako na wana Professional Lecturers wenye uzoefu na pia ni wafanyabishara katika Tehama, kwa hiyo utapata, elimu na ushauri na kusaidiwa jinsi ya kuanza, ila pia kuna vyuo vingine vipo ila sina uhakika na hivyo ila pia ukumbuke jitihada zako binafsi zitakusaidia kupata ujuzi zaidi  

Kwa ushauri zaidi wasiliana nami katika 


Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na magroup ya Whatsapp ya MAXPO Tanzania  Maximize your potential   







Katika Upande wa Elimu ya juu, ni vizuri kupata ushauri bora kabla hujaenda kujiunga na chuo chochote.
Kwa maana uamuzi wako huo utaamua mambo yafuatayo katika maisha yako...




JINSI YA KUSOMA IT: Mwongozo kwa Wanafunzi Waliofeli Form Four, 2024

KIPATO CHAKO BINAFSI
Kozi hii ya IT, Kichwa chako ni ofisi yako, kwa hiyo kama utapata elimu mbovu,utapoteza uwezo wako wa kujiajiri na unaweza ishia pabaya.


AJIRA
Interviews za kazi hizi za IT, sio nyepesi, na kwa hali hii itakushinda kushindana na watu waliofundishwa vyema na kuwa wazuri katika maeneo muhimu ya Information Technology.

MCHANGO WAKO KWA TAIFA
Kozi hii au profession hiii au kazi hii ya IT ina mzigo mkubwa katika taifa hili changa kiteknolojia.
Kuna matatizo katika jamii ambayo yanahitaji kutatuliwa kidigitali,kwa sababu hii kama utakuwa na elimu mbovu,

utakuwa mmoja wa walalamikaji badala ya wabunifu na watatuaji matatizo.



VIGEZO VYA CHUO BORA KATIKA IT
Vifuatavyo ni mojawapo ya vigezo muhimu,ila vinaweza vikawepo vingine zaidi.




UBUNIFU UNAOFANYA KAZI
katika mavyuo mengi sikatai kama kuna ubunifu ila mwingi unaishia kwenye makaratasi ya chuo na kutupwa stoo(store). 
Ubunifu hujulikana kwa project ambazo zinavuka mipaka ya chuo na kuifikia jamii.

UFUATILIAJI WA CHUO KWA PROJECT ZA WANAFUNZI.
Kuna mavyuo yanaongoza kwa kutupa store project za wanafunzi lakini pia kutokuchukulia kwa umakini project zinazofanywa na wanafunzi, kiasi kwamba wanafunzi wako huru kuforge project zao na chuo kuzipokea tuu kwa kutokujali ya kwamba hii project imefanyika au laa. 

ASILIMIA YA VITENDO KATIKA ELIMU INAYOTOLEWA.
Ni muhimu kwa chuo kuwa na asilimia kubwa sana ya vitendo kuliko nadharia

VIFAA VYA KUJIFUNZIA IT
Ni muhimu kusoma  kwenye chuo chenye vifaa vya kutosha ili ujue haswa nini kinaendelea makazini ila ni kwa  asilimia ndogo hii pointi ina umuhimu maana IT inakuwa kwa kasi na Vyuo vya haviwezi kuwa na vifaa vya kisasa kila wakati.


"Chuo kinaweza kumtengeneza mhitimu wa IT,ila ni jukumu la mwanafunzi binafsi akiwa chuoni, kutoka chuoni kama mtaalamu,na sio mhitimu pekee kwa maana wahitimu hupata shida sana kutafuta ajira wakati wataalamu hutafutwa na ajira na pia hujiajiri."




Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na magroup ya Whatsapp ya MAXPO Tanzania  Maximize your potential   


VIFUATAVYO NI VYUO BORA KUJIFUNZA IT  TANZANIA.
 1. Dar es salaam Institute of Technology (DIT)

2. St. Joseph University in Tanzania.

3.University of Dar es Salaam.

4. University of Dodoma



Kwa kumalizia, vyuo vipo vingi na wanafunzi wanazidiana uwezo 
kwa hiyo inawezekana ubunifu wa hali ya juu ukatokea kwenye chuo ambacho hakipo hata kwenye list hii, 
na pia vyuo vingine vinaweza vikaboresha ufundishaji wake na kuvipiku vyuo vilivyopo sasa.

Na la muhimu college za IT zipo nyingi na kwenye mikoa mingi, kwa hiyo kukosa nafasi kwenye vyuo hapo juu haimaanishi IT yako umeitupa, ila ina maana wewe ndio wa kukin'garisha chuo ulichokuwepo.




Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na magroup ya Whatsapp ya MAXPO Tanzania Maximize your potential  


 





Fahamu kitovu cha teknolojia( Technology Hub) hapa Tanzania ambacho wanafunzi wa chuo na wataalamu katika nyanja mbali mbali za teknolojia yaani Software developers, Web developers, Electricians, Electronics Engineers and Computer Engineers n.k hukutanika na kuvumbua au kuboresha vitu.

Kitovu cha teknolojia au kwa lugha ya kiingereza technology hub ni sehemu ambazo huanzishwa kwa malengo ya uvumbuzi na utatuzi wa matatizo kwa nji ya teknolojia. 


Kwa Afrika, sehemu hizi zimefikia 314 katika miji 93 katika inchi 42 nchi kama South Afrika ikiwa inaongeza kuwa na vitovu vingi.

Kwa hapa Tanzania, tuna kitovu cha teknolojia kimoja ambacho kinaitwa Buni Hub.

BUNI Hub.
Buni huhusika zaidi na kuwasaidia wanafunzi hata watu wabunifu katika teknolojia kwa kuwapa ushauri(mentoring) na kuwaongoza kupata uwezo wa kufanya ujasiriamali kwa kupitia teknolojia n.k.


BUNI huwa inaendesha semina, mafunzo mafupi mara kwa mara ili kuweza kuwajenga wanachama wake katika uanzishwaji wa project na hata usimamizi wa project hizo za kitaalamu na kuwaongoza waweze kufikia malengo yao.
Kwa maelezo zaidi tembelea tovuti ya BUNI hapa na wasiliana nao kuweza kujiunga. 

MANUFAA YA KUJIUNGA.
Utajenga uwezo wako binafsi katika kubuni mambo mbali mbali ya kiteknolojia.


Utakutanishwa na watu ambao wana mawazo kama yako ambao watakusaidia kusimama vizuri zaidi.

Ni sehemu ambayo inaweza ikawa uwanda wa wewe kuelewa njia ya kupata hata ufadhili wa kazi yako. 

Muhimu zaidi chochote ambacho hutumii kitapotea na kama wewe ni mwanafunzi wa IT,au kozi zozote za science ni muhimu kuwa pamoja na watu ambao wana elimu kama yako ili elimu yako isije ikalala na ukaanza kufakamia fani za watu wengine.

Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   

Ulimwengu wa teknolojia ya mtandao yaani Information technology ni mkubwa sana, na  wengi huwa wanajikuta wanashindwa kufikia malengpo yao, kwa  kushindwa kujua tofauti ya kozi zilizopo, hebu fuatilia uelewe kipi ni kipi?

Information Technology

Hii ni kozi ambayo inadili zaidi na mawasiliano ya njia ya kompyuta na uendeshaji wa mifumo/systems ya kompyuta na hata designing. 

kozi hii hutoa watu/professionals ambao ni system administrators,ICT officers, Graphics Designers etc 


watu ambao wapo kwa ajili ya kuwasaidia watu wengine kuweza kutumia vizuri, mifumo ya kompyuta.

Kazi.

Hawa watu wengi huwa wanaajiriwa, 

zaidi ila pia wanaweza kuajiajili kwa katika kufanya maintenance ya vifaa vya ICT, ICT Equipment supply, 

na hata kufunga mifumo ya network sehemu mbali mbali na akijiendeleza huweza kuwa Webmaster wa tovuti mbali mbali.

Kipato.

Mishahara yao hulipwa kulingana na elimu ya Degree au ya diploma aliyonayo kama fani nyingine na Zaidi ikizingatia kazi anayofanya na unyeti wa kazi hiyo.



Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   

Computer science.

Uwanda huu upo ndani zaidi kuliko IT, maana hawa watu mbali na kujua vitu vyote vya kozi ya IT,


pia huweza kujua kutengeneza program za aina mbali mbali za computer, na pia hufundishwa lugha nyingi za computer na huwa wako vizuri kiasi hata kwenye hardware ya computer.

Kazi.

Hawa watu utawakuta kama pia ma system administrators, business analysts, system analysts, ICT Officers, Application programmers, software developers. 

Pia wengi hujiajiari na kuanzisha makampuni/biashara za kutengeneza kompyuta hardware na software, 
websites na kazi nyinginezo nyingi katika uwanda wa technology.

Kipato

Wanapoajiriwa kipato chao hakitofautiani na IT.

Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   

Computer Engineering

Fani hii, hujikita Zaidi na hardware ya computer, huku tunapata watu ambao wanaunda vifaa ambavyo vinaweza fanya kazi na mifumo ya computer. 

Hawa kwa nchi zenye viwanda vya kutengeneza vifaa hivyo,  huwa ni soko kubwa sana, 

ila kwa nchi ambazo zinaendelea huwa bado wana soko dogo sana, na hata huogopwa kuajiriwa kulingana na Title yao ya Kuwa engineer.

Kazi.

Hawa hufanya kazi ya kutengeneza vifaa ila pia huweza kufanya kazi nyingi ambazo mtu wa computer science anafanya, 
pia ni mafundi waliobobea katika kurekebisha computer mbovu.

Kipato

Hawa huwa na mshahara wa juu kuliko IT na Computer Science, maana hulipwa katika kiwango cha ma engineers,

 lakini pia hufungua biashara kubwa za computer maintenance na hardware Suppliers na zaidi...
  

Software engineering

Katika Fani hii tunakutana na watu ambao wanataka kubobea katika kutengeneza programu za computer, 

hawa watadeal na program tuu na kidgo sana mambo mengine katika fani ya teknolojia.


Kazi.

Hawa hufanya kazi kutengeneza program za kila aina, pia huingia kwenye network na kubobea humo,

na huwa pia kuweza kufanya kazi za Computer Science kwa kiasi na hukinzana kabisa na computer engineers maana wao hufanya kazi na hardware.

Kipato

Hawa wana mshahara mkubwa wa kiwango cha Engineer kama computer engineer anavyolipwa na pia huwa wanajiajiri sana na kuanzisha makampuni ya kutengeneza programu.

 

Jinsi ya Kujiendeleza…

Ulimwengu wa Computer umejaa vyeti vya mafunzo mbali, 

ili mtu abobee katika sehemu maalumu hizo huitwa certifications mfano mafunzo ya Network hutoa vyeti,

kama CCNA, CCNP na kuendelea na mafunzo ya database kama Oracle , na hata auditing(Ukaguzi) kwa maelezo Zaidi fuatilia article yangu ya kuhusu certications za IT.


Lakini pia anaweza jiendeleza katika masters degree za vitu mbali na hata kuwa Tutorial au lecturer au professor maana bado kuna upungufu mkubwa mno katika ngazi hizo.

Kwa muongozo zaidi, Wasiliana nami katika email elisanteshibanda@yahoo.com au

Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa