Zingatia haya unapotaka kufanya manunuzi kwa njia ya internet ili kuepuka wezi.

Kutokana na  maendeleo ya kiteknolojia, sio jambo la kuepuka tena kufanya manunuzi kwa njia mtandao wa internet, maana umejaa vitu vya thamani ndogo na vizuri lakini pia umejaa wezi.  Fuatilia haya ili uweze kufanya manunuzi bila kujutia...

  1. Fungua akaunti pekee benki ambayo itatumika kwa ajili ya matumizi hayo ya manunuzi tuu, na uweke hela tuu pale pindi unapotaka kununua vitu, tunafanya hivyo ili endapo akaunti ikafikiwa na wezi wasiweze kuiba chochote.
  2. Pata elimu ya kutosha benki juu ya kitu gani cha kulinda kuhusu taarifa zako.
  3. Nunua sehemu maarufu au kwenye tovuti zinazofahamika dunia nzima kwa manunuzi mfano...GooglePlay, Amazon,eBay na alibaba.
  4. Usimtumie mtu usiyemfahamu taarifa zako za kibenki kwa njia ya email au yeyote ile.
  5. Hakikisha katika browser yako wakati unataka kufanya manunuzi pale kwenye sehemu ya address  imeandikwa au inaanza address kwa njia hii "HTTPS://....." na sio "HTTP://...." ina maana ya kitaalamu "Hyper text transfer protocol secure"
  6. Jiridhishe ya kwamba hiyo ndio tovuti yenyewe au kuna mtu ametengeneza tovuti feki ili kukuibia taarifa zako.
  7. Ukimaliza kufanya manunuzi yako ni vyema zaidi ukafuta browsing history yako yote ili kufuta cookies zenye mabaki ya taarifa zako.
  8. Muone mtaalamu wa Ecommerce ili akusaidie unapotaka kufanya manunuzi makubwa.

0 comments:

Post a Comment