Maeneo maalumu ya kujikita (Kubase) na kurahisisha zoezi la kupata ajira au kujiajiri katika IT, 2023.

 

Katika kozi ambazo zinaongoza kwa watu wake kutokuwa na ajira ni Computer science, Information Technology and nyinginezo za Technology. Ni ajabu lkni ukilinganisha na nature ya ulimwengu wa sasa, ila ndio uhalisia.

Jambo kubwa linalofanya watu hawa kukosa ajira ni kosa ambalo linafanya mavyuoni bila kutambua, vyuo vinajikita katika kuwa expose(funulia) katika ulimwengu mzima wa IT nakusahau kwa fanya wachague mapema sehemu gani wanatakiwa wajikite kwa isiyopungua miaka 2 ya mwisho ya masomo yao.

Kwa kutambua hilo nimejaribu kuchambua maeneo kadhaa unaposoma chuo unahitaji kujikita kulingana na soko halisi huku njee.


Cyber Technology

Hili eneo linahusika na ulimwengu wa Mtandao wa Internet na Network, jinsi gani connection zinafanyika kati ya watu na vifaa na programu mbali mbali, kwa ufupi ukijikita katika cyber technology utajikita zaidi katika ku maintain security ya mifumo isidukuliwe na kulinda data za watu katika mifumo hiyo, hawa watu ni muhimu sana katika kila organization inayotumia mifumo na yenye data nyeti sana mfano serikali, benki na maeneo yanayofanya tafiti na sasa hata chaguzi...

Njia.

Kwanza uwe katika kozi kama computer science au IT,  halafu unatakiwa usomee vyeti vya ujuzi maalumu mfano CompTIA Security+ na Certified Ethical Hacker (CEH) na pia ujichanganye katika mashindano mbali mbali ya mambo hayo yanayotokea ili kujinoa.

Ila vyovyote ufanyavyo unatakiwa uji-update katika Artificial Intelligence maana inachukua nafasi kubwa sana, marobot ndio yanahack siku hizi, na Ai ndio ina ulinzi mkali kuliko watu, so unaweza soma ukashangaa anaajiriwa robot anaitwa Junior kutoka uswisi 😂

KAZI

Peleka CV yako maeneo kama Benki, Nafasi zikitoka serikalini zaidi TCRA, na makampuni ya mitandao ya simu


Application Development

Bila ubishi tunahitaji Apps siku hzi kwa hali na mali na bei ya App moja sasa, unaweza ukajisikia kizungu zungu...kwa sababu wataalamu ni wachache sana na bado tuna mahitaji mengi sana ya App kwa ajili ya mazingira yetu ya Africa, Tanzania.

Njia

Ngoma iko wazi, tutorial lundo mtandaoni chuoni usimuone Prof wa watu yeye ni mkufunzi wewe ndio mhusika haswa na Tech inabadilika kwa speed kubwa sana, ingia website za matorrent badala ya kudownlaod movies download udemy tutorials katika Lugha za Apps kama Javascript na mifumo mbali mbali...YOutube kuna professional watakueleza 1 mpka 10, pa kuanza hadi pa kumaliza.


Server/Computer troubleshooting, maintenance and installation.

Hapa kuna wataalamu wengi ila wamejikita zaidi katika maeneo ya kawaida sana, yaani kutengeneza computer za kawaida tuu, ila katika upande wa servers ni wachache sana, kila kampuni kubwa inahitaji server kuweza kutumia programu za ERP, na nyinginezo nyingi tuu...Lkni pia kutokana na kuboreka kwa mtandao wa Internet, makampuni mengi yamekuwa yakitumia server za njee ya nchi maana kutunza server computer imekuwa gharama sana kuliko kulipa kwa wenye nazo.


Njia

somea Microsoft Certified Solutions Expert (MCSE), CompTIA Server+, Red Hat Certified Engineer (RHCE) na VMware Certified Professional-Data Center Virtualization (VCP-DCV), masomo haya yanapatikana mtandaoni na utabidi ulipie, ili uwe mzuri katika IT ni lazima uingie gharama no shortcut, vyeti hivyo vitakuitisha kwenye interview haraka sana.


Software Sales, maintenance and installations.

Huku unajikita zaidi katika kuuza Programu za kitaalamu, za mifumo mbali mbali ya kuendesha makampuni au taasisi  mfano hospital management, school management, church management N.K 


Njia

Unahitaji unavyosoma uzitatute hizi programu uelewe zinavyofanya kazi na uanze kuziuza, au wewe utengengeneze za kwako. soko lipo kubwa , sehemu nyinginr unahitaji kutoa elimu kabla ya kuuza ila zinahitajika sana hadi sasa.


Network Installations and Maintenance and security.

Eneo hili linahusika na kufunga mtandao kwa njia ya nyaya na bila wire, pamoja na maendeleo makubwa ya teknolojia, badi tunahitaji waya kwa sababu zina ulinzi mzuri wa kuto kutoa nafasi ya kudukuliwa, na pia nimejumuisha kufunga mifumo ya camera za ulinzi kwenye majengo.


Njia

Nenda kasome vyeti vya cisco na pia kaa na wataalamu wa mifumo ya security camera, kama hakuna vyeti hata ujuzi wenyewe unaweza andika katika CV yako ikawa safi sana, na ukapata ajira au kipato haraka.


Computer Rent and sales

Kama una uwezo wa kupata mtaji, fungua duka la kuuza computers au laptops. siku hizi taasisi nyingi zinapenda kukodi computer kwa muda maalumu na kukulipa, kama ukiwa nazo basi utafaidika, anza na kuuza kwanza baadaye ukipata channel nzuri utakodisha, nunua kutoka China maana laptops zimekuwa bei ndgo sana siku hizi.


Professional Software Training.

Sizingumzi kufundisha computer hapa, nazungumzia kufundisha hizi programu za kuendesha taasisi na makampuni mfano za wahasibu, mahospitali, mashule na kadhalika, kuna zile maarufu ukizifahamu zitakufanya uitwe na makampuni kwenda kuziweka, kuziuza na hata kufundisha wafanyakazi wao.


Njia

Jifunze mtandaoni au kama upo kweye sekta mabayo imekuvutia tengeneza mfumo mzuri na uuze kama kuna uhitaji eneo hilo.


Graphics Design

Sanaa ya matangazo ni muhimu siku hzi kwa ukuaji wa biashara, ila imekuwa nyepesi sana maana programu zimekuwa nyepesi kutumia ya kwamba watu wengi wanafanya wao wenyewe. Ila kuna matangazo yanahitaji skills zaidi kama ya Video so jikite huko, nenda mbali zaidi kwenye 3D na motion graphics.

Njia

Youtube ina mafunzo ya kila aina ya programu, tafute mafunzo muhimu ya programu mama kama Adobe Illustrator, Photoshop na Indesign, then hamia katika After effects, Maya, cinema4D na kuendelea kazi zipo nyingi mitandao ya UPwork.



0 comments:

Post a Comment