Jinsi gani Anti-Virus inavyoweza kubadilika na kuwa chanzo cha matatizo kwenye kompyuta.


Anti-Virus ni programu ambayo hutumika kuilinda kompyuta, kutoka kwa mashambulizi ya virusi ambavyo huathiri mifumo yake na uwezo wake wa kiutendaji kazi.

Jinsi Anti-virus inavyofanya kazi.
kama bodyguard anavyomlinda mtu, basi na anti-virus hulinda kompyuta kwa staili hiyo. Yenyewe huhakiki na kupitia kila kinachofanywa na kompyuta ili kuweza kujua kama kitakuwa na madhara au la!
Mfano:
Unapoingiza tuu flash yako kwenye kompyuta kabla hata hujaifungua anti virus ni ya kwanza kuleta warning kama kuna kirusi au la kwa sababu imeshaipitia kabla.

Tatizo lilipo:
Kutokana na kitendo hicho processor ya kompyuta hufanya kazi mara mbili zaidi kwa kila kitendo kinachofanyika, ya kwanza ikiwa ni kazi ya Anti virus(ukaguzi) na ya pili ikiwa ni kazi ya Operating system(windows) ya kumhudumia mtumiaji matakwa yake.

kwa hali hiyo anti virus kubwa zenye nguvu kama karspesky, avg, avast huhitaji uwezo mkubwa zaidi wa ukokotoaji ili ziweze kufanya kazi na kompyuta na endapo uwezo wa kompyuta ni mdogo, hapo husababisha kompyuta kufanya kazi kwa utaratibu na hata husababisha ukwamaji(stucking) wa kompyuta ikiwa inafanya kazi mara kwa mara.

Ushauri.
kwa matumizi ya sasa unashauriwa kuongeza uwezo wako wa kompyuta mpaka kufikia RAM=4GB na zaidi muone mtaalamu wa tehama ili aweze kukusaidia kusimamia matumizi mazuri ya diski yako inayobeba Operating system iwe na nafasi ya kutosha.

0 comments:

Post a Comment