Ninavyozungumzia Information technology course najumuisha computer science, computer engineering, Software engineering etc.
Sasa zingatia vigezo vifuatavyo kwa ngazi tofauti.

CHETI


Utahitaji cheti cha form four (CSEE) chenye kuanzia pass 4 (Ukiondoa masomo ya dini)


au 
     

Utahitaji  cheti cha National vocational training award level 3.


au


Kwa kwenda kusoma business Informational technology unaweza ukapeleka hata National Business certificate stage 1 kikiwa na pass 2.




DIPLOMA

Utahitaji cheti cha advanced Certificate of Secondary Education(ACSE) ukiwa na principal pass 1 na subsidiary pass 1


au

Basic Technician Certificate (NTA Level 4) katika kozi za certificate in computer science, IT, Business IT, Computer Engineering na Electrical Engineering.


DEGREE

Utahitaji cheti cha advanced Certificate of Secondary Education(ACSE) ukiwa na principal pass 2 ambayo mojawapo lazima iwe Advanced Mathematics 

au 

ufaulu wa pass katika masomo yeyote mawili ya sayansi na Advanced Mathematics uwe na ufaulu wa subsidiary pass.

au 

Uwe na ufaulu wa GPA zaidi ya 3.0 katika ngazi ya Diploma.


Kwa maelezo zaidi wasiliana na uongozi wa vyuo vinavyotoa IT kwa kutembelea tovuti zao. Kila la kheri.

Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na magroup ya Whatsapp ya MAXPO Tanzania  Maximize your potential 





Fahamu Kozi za IT Zinazotolewa Tanzania na Fursa Zake za Ajira (2026)

Maana ya Misamiati

Self Employing – Unaweza kujiajiri kwa urahisi kupitia freelancing, consultancy, startup au biashara binafsi.

Highly Marketable – Ajira nyingi na mahitaji makubwa sokoni.

Marketable – Ajira zipo na fursa ni nzuri.

Less Marketable – Ajira zipo lakini ushindani ni mkubwa au soko ni dogo.

Specialized Market – Ajira zipo katika taasisi au sekta maalum.


KOZI ZA DEGREE

1. Business Information Systems (BIS)

Status: Highly Marketable

Kozi hii inachanganya biashara na teknolojia. Wahitimu wanaweza kufanya kazi kama:

  • Business Analyst

  • Systems Analyst

  • ERP Consultant

  • Digital Transformation Officer

Maoni: Moja ya kozi zenye mahitaji makubwa kwa sasa.


2. Computer and Information Systems Security (Cyber Security)

Status: Highly Marketable

Kutokana na kuongezeka kwa cyber attacks, taasisi nyingi zinahitaji wataalamu wa usalama wa mifumo.

Ajira:

  • Cyber Security Analyst

  • Security Consultant

  • Risk Analyst

Maoni: Ina thamani kubwa zaidi ukiendelea na certifications kama CEH, CompTIA Security+, au Master's.


3. Computer Engineering

Status: Marketable (Specialized)

Inajikita kwenye hardware, embedded systems na electronics.

Ajira:

  • Hardware Engineer

  • Network Infrastructure Engineer

  • Embedded Systems Developer

Maoni: Sio maarufu kama Software Engineering lakini ina nafasi nzuri kwenye telecoms, viwanda na hardware industry.


4. Computer Science

Status: Highly Marketable & Self Employing

Kozi yenye flexibility kubwa zaidi.

Ajira:

  • Software Developer

  • AI Engineer

  • Data Analyst

  • Systems Developer

Maoni: Miongoni mwa kozi bora zaidi kwa sasa kutokana na AI, cloud computing na software development.


5. Geoinformatics

Status: Specialized Market

Ajira:

  • GIS Specialist

  • Mapping Analyst

  • Survey and Spatial Data Expert

Waajiri:

  • Serikali

  • Mining

  • Utilities

  • Environmental Organizations

Maoni: Soko si kubwa lakini wataalamu ni wachache.


6. ICT Mediated Content Development

Status: Emerging Market

Ajira:

  • E-learning Specialist

  • Digital Content Developer

  • Instructional Designer

Maoni: Mahitaji yanaongezeka kutokana na online learning lakini bado ni kozi mpya.


7. Information Systems

Status: Highly Marketable

Inalenga kuunganisha biashara na teknolojia.

Ajira:

  • Systems Analyst

  • IT Officer

  • Business Systems Administrator

Maoni: Inafanana kwa karibu na BIS na ina nafasi nzuri sana.


8. Multimedia Technology and Animation

Status: Self Employing & Marketable

Ajira:

  • Animator

  • Video Editor

  • Motion Graphics Designer

  • Content Creator

Maoni: Inafaa sana kwa freelancing na media industry.


9. Software Engineering

Status: Highly Marketable & Self Employing

Ajira:

  • Software Engineer

  • Mobile App Developer

  • Web Developer

  • DevOps Engineer

Maoni: Miongoni mwa kozi zenye fursa nyingi zaidi duniani kwa sasa.


10. Telecommunication Engineering

Status: Marketable

Ajira:

  • Telecom Engineer

  • Network Engineer

  • Infrastructure Engineer

Waajiri:

  • Telecom Companies

  • ISPs

  • Data Centers

Maoni: Bado ina nafasi nzuri Tanzania.


KOZI ZA DIPLOMA

1. Computer and Business Management

Status: Marketable & Self Employing

Mchanganyiko wa IT na biashara.

Ajira:

  • Office Systems Administrator

  • Business Support Officer


2. Computer Networks

Status: Marketable

Ajira:

  • Network Technician

  • Network Administrator

Maoni: Ina soko zuri ukiiongezea certifications kama CCNA.


3. Computer Systems Administration

Status: Highly Marketable

Ajira:

  • Systems Administrator

  • IT Support Officer

  • Technical Support Specialist


4. Graphics Design and Web Technology

Status: Self Employing & Marketable

Ajira:

  • Graphic Designer

  • Web Designer

  • Digital Content Creator

Maoni: Inafaa sana kwa freelancing.


5. Information and Telecommunication Technology

Status: Marketable

Ajira:

  • Telecom Support

  • Network Support

  • IT Support


6. Information Technology (IT)

Status: Highly Marketable

Ajira:

  • IT Officer

  • Technical Support

  • Systems Administrator

  • IT Consultant

Maoni: Diploma yenye nafasi nyingi zaidi za kuingia kwenye sekta ya IT.


Top 5 IT Courses Zenye Fursa Kubwa Tanzania (2026)

  1. Software Engineering

  2. Computer Science

  3. Cyber Security

  4. Information Systems / Business Information Systems

  5. Information Technology (IT)

Top 5 IT Courses Bora kwa Kujiajiri

  1. Software Engineering

  2. Computer Science

  3. Graphics Design and Web Technology

  4. Multimedia Technology and Animation

  5. Business Information Systems

Hitimisho

Kwa mwaka 2026, kozi zinazohusiana na Software Development, Artificial Intelligence, Cyber Security, Cloud Computing, Data Analytics na Digital Transformation ndizo zenye ukuaji mkubwa zaidi wa ajira duniani na Tanzania. Wanafunzi wanashauriwa kuchagua kozi sio kwa jina pekee, bali kwa kuangalia mahitaji ya soko, uwezo wao binafsi na malengo yao ya muda mrefu.

 






Kama unasoma IT, tambua CV yako haitakiwi kuishia na diploma/degree pekee  inatakiwa kuwe na certifications au skills ili uweze kuwa na tija kwa waajiri.
Certifications zinahitaji pesa, skills hazihitaji pesa ila zinahitaji jitihada binafsi na kujifunza.

App Development.

Siku hizi kuna soko kubwa sana la application za android na iOS maana watu wanatumia sana smart phones ambazo zinafanya vizuri zaidi katika hizo application/programu. Na kwa sasa gharama za kutengeneza App moja ya Android inafika millioni 5, ukisoma mtandaoni kwa njia ya video unaweza tengeneza ila sio vyepesi ni ngumu sana.
Kazi ambazo utapita kirahisi ukiwa na ujuzi huu ni Software Engineer, System Analyst, Business Analyst etc.

Networking

Huu ni ujuzi wa kufunga networks za computer, ujuzi huu huwa na certifications za Cisco ila kuufahamu kutakusaidia kupita kwenye interview nyingi za Kazi za IT.

Cyber security

Kama Networking na hii ni certification, ila unaweza soma online kwa bei nafuu na kuwa na hichi cheti utakua lulu katika kazi za makampuni ya mawasiliano, TCRA, na mabenki huwachukua mara moja watu hawa.

Comp TIA

Huu ni ujuzi wa computer in general maintenance na zaidi, harwdare na software ukiwa nao huuu kazi za ICT Officer utakuwa una nafasi kubwa sana za kuzipata..unaweza ukasoma yote bure mtandaoni ukafahamu ujuzi au ukasoma na kulipia certfication yake ukawa nayo.


Web Development

Huu ni ujuzi wa kutengeneza tovuti/website, kampuni nyingu huingia gharama za kuwaajiri watu kutengeneza website na kuzi maintain na nyignine bado hazina, ukiwa na huu ujuzi unaweza hata uka suggest katika application letter ya kwamba unaweza ukatengeneza na website ya kampuni pia.


Graphics Design

Hakuna kampuni isiyojitangaza na makampuni hulipia gharama kubwa sana kudesign haya matangazo, so ukiwa na ujuzi huu, utaokoa pesa kwenye kampuni inayotaka kukuajiri na hyo ukijtetea hata kwenye application letter wanaweza wakaona una umuhimu zaidi kuliko watu wengine kwenye interview.

Na skills nyingine kama za MS office, database na kadhalika...zote hizi kama upo chuo basi hakikisha unazizoa kwa hali na mali maana chuoni una muda huko njee hakuna muda wa kujifunza kuna muda wa kufanya tuu.






Rekebisha haya ili CV yako in'gae na upate kuitwa kwenye interviews/usaili.

Daftari/kitabu

Usiandike kitabu na experience ya kuandika huna, acha iwe page 1 au 2 tuu inatosha, kwa nini? Mfano wewe ndio afisa rasilimali watu ina CV 300 mezani utasoma CV ndefu?


Usiandike majukumu yako uliyokuwa unafanya awali.

Yeah naona kuna mtu alikuwa anakula baada ya kusoma hiyo anatafuna taratibu sasa, NDIO andika mafanikio na sio majukumu, mfano wewe ni mwalimu usiandike nilikuwa nafundisha, natunga mitihani, na kusahihisha instead andika nimefanikiwa kufundisha wanafunzi 500 geography na katika hao walifaulu 400, rafiki unaitwa haraaakaaa kuanza kazi.


kuweka vipengelea ambavyo havihusiani na kazi unayoitiwa.

CV sio ukishatengeneza basi ndio imetoka hapana, ukiitwa kwenye kazi ya jamii CV yako ioneshe sehemu ulijitolea hata kwenye vikundi vya dini, kuonyesha uongozi,  ila ukiitwa kazi ya ofisini, toa vipengele vya vikundi vya kijamii unavyojitolea maana utaonekana uko busy na kazi yao unaweza lipua au ukawa na visingizio vingi vya kutoka kazini.


Hobbies

Kama bado unaweka hizi acha huu uhuni.


Referees.

Usiweke mtu ambaye hajawahi kuwa supervisor wako au boss wako, kama unatoka chuo si  ulienda field? kawatafute huko, na utafute lecturer  hata mmoja, chondechonde usimuweke ndugu yako.


BONUS

Hebu nenda katafute muundo mzuri wa CV mambo ya CV Kuonekana kama CV ya Chifu Mashuposhupo acha...tembelea cvmkr.com itakusaidia.

Kwa ushauri na mawasiliano tembelea rainstech.com wasiliana nasi kupitia live chats






Ili uweze kufanya kazi mtandaoni unahitaji kuwa na ujuzi ambao mtu anaweza kuutumia ujuzi wako bila kuonana na wewe, na pia uwe na ujuzi wa lugha ya kiingereza vizuri ikiwezekana na lugha nyingine kubwa kama kifaransa.

Na hapo ndio unaona ujuzi wa IT huongoza katika hili lakini pia hata secretarial ila hizi kuna program nyingi ambazo zinafanya kazi zaidi ya secretary.

ujuzi au skills ambazo huhitajika mara kwa mara na watu haujiriwa  na kulipwa mtandaoni ni kama ziifuatazo:

Advanced microsoft office Skills( Excel, Word, Powerpoint, access)

Application development(Android, IOS, web applications)

Web design

Graphics Design( artworks, branding, video editing, adverts etc)

Mitandao inayotoa ajira hizi, inahitaji vitambulisho na sometimes ukitaka kuwa member basi utagharamia membership kama 10 dollars inategemea ila huwa ni bure, na katika kila malipo yako utakwatwa hela hapo.

Freelancer.com

upwork.com

Guru.com

na mingineyo ila hiyo ndio naona vijana wa Tanzania hapa hapa wanalipwa hela.

.



IT(Information Technology) ni kozi nzuri sana kwa vijana na pia ni mojawapo ya sekta ambayo makampuni yaliyowekeza humo yanatengeneza pesa nyingi sana.

Na tunapokwenda IT Imekuwa ikifuta nafasi za kazi nyingi sana kwa kompyuta kuzifanya hizo kazi, mfano;

Assembly line & factory workers

Phone Operators and receptionists

Cashiers

Bank tellers and clerks

Pilots

Journalists and reporters

Stock traders

Postal workers

Travel agents

Accountants

Na kadhalika ni kazi nyingi zinapotea,hatuwezi maliza ila pia IT inatengeneza ajira zake nyingi sana, nyingine hazihitaji hata uajiriwe na mtu.

NJIA  YA SHULE KUPITIA ADVANCE HIGH SCHOOL

Kuanza kama ni mwanafunzi wa sekondari hakikisha unasoma masomo ya science na biashara na uendelee advance na masomo hayo hlafu ukifika chuo  chagua kozi za IT.


NJIA YA SHULE KUPITIA CHUO

Soma mpaka form four masomo ya science na biashara, halafu chukua certificate ya IT, halafu diploma halafu degree. Vyuo bora ni University of Dodoma, St.Joseph University in Tanzania, Dar es salaam Institute of Technology,College of Information and Communication Technologies (CoICT) - University of Dar es salaam na University of Dar es salaam Computing centre.


NJIA YA  KUTOKEA CHUO NA KUENDELEA.

Soma kozi yeyote halafu ukimaliza unaweza nenda kwenye vyuo vya IT, kama unaweza soma degree nyingine ya IT au nenda kwenye vyuo vinavyotoa ujuzi wa IT na ujifunze unaotaka.

Mfano Degree ya Uchumi ila unapenda IT. basi nenda kwenye chuo kinachotoa IT, tafuta Ujuzi unaoutaka mfano:

Application Development

Networking(Inategemea vigezo)

Cyber security(Inategemea vigezo)

Computer TIA

Web development

Graphics Design.

Accounting package Training.

Halafu tafuta college inayotoa ujuzi husika katika vyuo nilivyoviorodhosha hapo juu.

Mara nyingi kozi nyingine hapo huwa hazifundiswi mavyuoni mfano cyber security au App development kwa hizi kozi inabidi ufanye paid online training katika mitandao kama Udemy, Tutsplus etc.


NJIA YA BURE

Kama unapenda IT na hauna hela zaidi ya hela ya bundle, basi chagua kozi unayotaka kusoma, halafu nenda kwa wanao download movies mtandaoni waambia wakusaidie kukutafutia hizo online courses then wakuwekee kwenye hard drive ili ukajifunze wemyewe privately, na watu wengi wamejifunza kwa njia hii, ila hautapata cheti chochote zaidi ya ujuzi.




Tehama(Information technology) Katika nchi za chini ya jangwa la Sahara, Afrika Mashariki bado ni changa sana. Na kama inavyofahamika teknolojia hurahisisha sana maisha na hupunguza mzigo mkubwa wa kazi kwa watu.

GUNIA ZITO.

Nimeifananisha na gunia zito kwa sababu kutengeneza teknolojia mbadala ili kuweza kutatua changamoto katika jamii inahitaji mafunzo, moyo wa kujitoa binafsi na jitihada zaidi.

Lakini pia inahitaji macho ya kuona hizo fursa katika jamii ili uweze kuzifanyia kazi. Watu wengi hukimbilia kazi ambazo hazihitaji sana ubunifu lakini huku ubunifu ndio mahali pake, pindi unapokosa akili za  ubunifu basi utashindwa kufanya lolote katika tehama.

LENYE PESA

Kama nilivyoeleza hapo mwanzo, pindi teknolojia hizi zinapotengenezwa na wataalamu, huingia sokoni na kurahisisha maisha ya wengi.
watu wengi, makampuni mengi na watu wengi yametajirika sana duniani kwa tehama, mfano 

kampuni kubwa zaidi ya Tax duniani haimiliki tax hata moja bali imeunganisha wamiliki wa Tax,
lakini tatizo waliloliona ni shida ya kupata Tax pale ambapo unaihitaji na haupo barabarani. 

UBER  kwa sasa inaingiza mabilioni ya Pesa duniani kote, hata hapa Tanzania zipo programu kama za mpesa, tigopesa zinaingiza pesa nyingi mno, 

zipo programu za vituo vya mafuta kama Petronite

zipo programu za maduka kama duka pro,

na programu za masomo kama thL na kadhalika na kadhalika...

JINSI YA KUWA MMOJAWAPO WA WABEBAJI.

1. Uwe na uwezo kujifunza kwa bidii sana, na kukuballi kutatua changamoto mbali mbali hata zisizolipa kwa muda huo.

2. Chukua masomo ya Tehama kuanzia ngazi mbali mbali kama cheti, diploma au degree.

3. Ikiwa huna vigezo, basi ujue kusoma na kuandika kiingereza vizuri na uwe na moyo wa kishujaa wa kusoma zaidi ya wale wanaosoma darasani ila ni lazima utafanikiwa.

Janga la ukosefu wa ajira haliwezi kuisha kama tutaendelea kusaka watu kutoka njee wafungue makampuni ndio tuajiriwe ila tuu kama sisi wenyewe tutakapoamua kutoka na kugeuza changamoto kuwa mtaji wetu.


Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   
au elisanteshibanda@yahoo.com








Tehama(Information Technology), imejaa fursa nyingi, na katika nchi zetu changa, fursa ni nyingi mno.

Katika Tehama juhudi za mtu binafsi na Mungu wake, ndio zitamfanya afinikiwe au asifanikiwe.

Mtaji wa Tehama ni computer tuu, ambayo ni gharama ndogo sana kuipata.

Ni vitu gani mtu anaweza soma/jifunza ili afanikiwe katika Tehama.

Graphics Design(Sanaa ya Matangazo)
Hii ni sanaa ya matangazo ya biashara. Hakuna biashara duniani isiyotaka matangazo

na ukiangalia dunia ya leo, tumezungukwa na matangazo, yanazidi kuwepo na jinsi biashara zinavyozidi kuongezeka kasi ya uhitaji wa matangazo inazidi kuongezeka.

Jinsi ya Kujifunza
@ Chukua kozi fupi ya wiki 6, na wewe utaweza kuwa vizuri kwenye sanaa hii. 
Vigezo: Kuanzia Form Four Leaver
Price: 300,000Tsh
Training: MAXPO training
Mahali: Rains Technologies, Ilala Bungoni, Chunya str.

@Tumia njia ya Video ya kujifunza, kwa kutumia mitandao kama Youtube.






Web Development
Huu ni utaalamu wa kutengeneza tovuti mfano wa tovuti ni kama cnn.com, bbc.co.uk n.k 
Kila biashara inavyokua na kutaka kupita mipaka ya kiwilaya, kimkoa au kitaifa inahitaji tovuti kwa ulazima. Maana tovuti ni ofisi pekee ya kampuni ambayo inaweza fikiwa na mteja ,
Akiwa kokote kule duniani.

Kwa kuangalia uchumi wetu unavyokua na ongezeko la makampuni soko la tovuti litaongezeka maradufu.




Jinsi ya kujifunza
@Chukua kozi fupi ya wiki 8, ujifunze kutengeneza tovuti.
Training: MAXPO Training
Bei: 400,000/-Tsh
Mahali: Rains Technologies, Ilala Bungoni, Chunya str.

@Chukua certificate in InformationTechnology/Diploma/Degree kwa mwaka 1, 2, 3 N.k
Mahali: University of Dar es salaam Computing Centre
Vigezo: Tembelea chuoni.

@Tumia mafunzo ya vitabu na video za kwenye mtandao ili kujifunza kutoka kwa watu mbali mbali.


Computer Application
Kozi hii inakuweza kuifahamu computer ndani na njee, kuendesha stationery, na hata kutumia computer ya windows 10 na Apple computer(MAC OS) kama mtaalam.


Lakini pia inakupa uwezo wa kujifunza microsoft office yote.
Pamoja computer networks.

Jinsi ya kujifunza
@Chukua kozi fupi  ya wiki 4 ya Computer application.
Vigezo: Yeyote
Training: MAXPO Training
Bei: 250,000/-Tsh
Mahali: Rains Technologies, Ilala Bungoni, Chunya str.


@Chukua certificate /diploma/ degree katika Information Technology, computer science, ICT.
Mahali: University of Dar es salaam Computing Centre
Vigezo: Fika Chuoni.

@Tumia mtandao wa youtube kujifunza na google kupata vitabu.

Mafunzo ya Tehama, yanaanza taratibu na ni marahisi kwa mtu mwenye jitihada ya kusoma na nidhamu ya kujifunza bila kukata tamaa.
Kwa mawasiliano zaidi wasiliana nami.




Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   

au katika elisanteshibanda@yahoo.com
                  





Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   



Interview za mchujo ni interview za awali, ambazo hutumika kupunguza watu wengi walioomba kazi husika,

ili wabaki wachache kwa ajili ya hatua ya pili ya interview(usaili).
Interview hizi zina sifa kubwa sana ya kuvunja mioyo ya watu walioomba kazi, kwa watu wengi hujikuta wamejiandaa visivyo na kufanya vibaya.



Hebu kwanza tufahamu mambo ya kuzingatia unavyojiandaa na interview.


Muombe Mungu akusaidie kujibu kwa ufasaha, maana ni rahisi sana kujibu visivyo, pamoja ya kuwa unajua kila kitu.



Fahamu kwa undani kazi iliyotangazwa. Ni rahisi kusema, mimi nimesoma chuo kama IT, Computer science N.K na ndio maana kozi yangu imeorodhoshwa na nikaitwa, 
ila kufikiri huko sio sahihi na wengi hufeli maswali yanayohusiana na kazi hiyo. 
Fanya utafiti wa hali ya juu kwenye mtandao au kwa waliokwisha fanya teyari na uelewe.

kozi za IT Tanzania na Soko lake

Fahamu majukumu yaliyotangazwa na kazi husika na uhakikishe unayafahamu jinsi ya kuyatekeleza yote
au kama ukishidwa yote angalau ujue nini kinaendelea,     kwa maana maswali mengine hulenga humo.


Fahamu ni masomo/kozi gani yanayoendana na kazi husika,uliyoyasoma chuoni, halafu uyapitie kwa umakini.



MIUNDO YA MASWALI YA INTERVIEW(USAILI)

Muundo wa 1

Muundo huu utakutana na maswali 40 hadi 50, yanayokuwa ya kuchagua, na huwa yanagusa sehemu mbali mbali, ila zaidi sehemu zinazohusiana na kazi husika na sub course husika mojawapo huonekana kwa wingi.

Mfano:
Kazi ya Business analyst, maswali mengi asilimia 60-70 yatakuwa ya software engineering.

Jinsi ya kujiandaa:
Tafuta subcourse husika na uisome sana gusia maeneo mengine pia.

Muundo wa 2

Muundo huwa na maswali 4 hadi 5, ila maswali huwa yanalenga maeneo husika na yale ya kuzunguka.

Mfano:
System Administrator, maswali 2 yatahusiana na Networking lakini 2 mengine yawaweza kugusa database na hardware.

Jinsi ya kujiandaa:
Soma yote yanayoendana na kozi husika na course zinazoendana na hiyo course.

Muundo wa 3

Muundo huu una maswali 4 hadi 5, na maswali hugusa course husika tuu na huulizwa kwa mfumo wa maswali ya scenario.
Mfano:
System Administrator, maswali yote ni ya networking, na yanaulizwa yakitakiwa kujibiwa kitaalamu na sio kitaaluma
Namaanisha kitaalumu ujibu kama mtu mwenye ujuzi na scenario hiyo  na sio kama mtu aliyakariri kutoka kwenye kitabu. 

Jinsi ya kujiandaa:
kama una uzoefu kumbuka uzoefu wako, kama una mafunzo ya certifications yatumie ipasavyo, lakni kama huna hivyo vyote usijali jiandae vyema na sub course husika nawe utafanikiwa.

Muundo wa 4

Muundo huu huwa na maswali 4 hadi 5, ambayo hujikita zaidi kitaalamu na katika majukumu yaliyorodheshwa na tangazo la kazi.

Jinsi ya Kujiandaa:
Soma kwa umakini yale majukumu ujue jinsi ya kuyatimiliza kivitendo kila moja na kama kuna vigezo vipitie hata ujue tuu kwa mbali nini kinaendelea.

Angalizo:
Ni kawaida kabisa kumaliza mtihani huu usijue kama umefaulu au umefeli, na hali hii huifanya ionekane ngumu sana, ila kabla ya kujibu swali tafakari linahitaji nini na ujibu vizuri ukujibu juu juu uamini kuna watu watajibu kwa umakini kuliko wewe.


Hiyo ni muundo ambayo imekuwapo ila inaweza badilika muda wowote hata kesho ikaja mengine zaidi, na sijakugusia interview za awamu ya pili na za mahojiano,ila kwa hayo chukua hatua, na nikutakie interview njema.
Kwa ushauri zaidi wasiliana nami 


Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa