Hebu jaribu kuchukua nafasi ya Human resource manager(Meneja wa rasilimali za binadamu) akiwa amepokea maombi ya watu 5000 kwa ajili ya nafasi moja ya kazi aliyoitangaza, unadhani atapitia na CV yako kwa jinsi ilivyo?

Basi kama unataka kufanya CV yako, ipendeze kimuonekano na hata iweze kumzuia meneja aliyechoka kupitia CV za watu hebu ingia hapa tengeneza akaunti yako bure na fuata maelekezo maana ni rahisi mno kutumia.
 
  • Kwanza Relax acha uoga na punguza presha, kutype ni kitu chepesi sana.
  • Fahamu herifu za kompyuta zilipo na ukumbuke taratibu taratibu mahali zilipo kila moja hata ikiwa moja kwa siku.
  • Acha kutype kwa kidole kimoja, tafadhali weka mikono yako yote kwenye keyboard na yote ifanye kazi ya kutype.
  • Acha kutumia kidole kimoja kwa kutype kwa kila mkono, tumia vidole vyote kwa kila mkono.
  •  Hakikisha kila kidole kina herufi ambazo kina husika na kutype zinaweza zikawa mbili au tatu ...mfano kidole changu kidogo kinahusika na herufi A,Q huku kidole gumba kikitumika kwa space.
  • Usiogope kukosea kutype herufi pindi unapotype kwa haraka maana hamna shortcut lazima ukubali makosa ili uweze kupata spidi nzuri ya kutype.
  • Tumia programu za bure kabisa za kukufundisha kutype ndani ya wiki moja utakuwa vizuri kabisa. mfano: tembelea hapoa ujipatie programu yako ya bure www.typingmaster.com
  1. Usiishi katika mitandao ya kijamii HAMNA MAISHA HUKO UNAJIDANGANYA TUU!!
Siku ina masaa 24, usitumie masaa mengi huko maana sio maisha halisi kama unavyodhani. kaa na watu unaowajali zaidi, watu halisi wa karibu yako ie majirani,utakapoumwa au kuwa na tatizo la ghafla huyo rafiki yako mbelgiji au mnamibia au muafrika ya kusini hataweza kukusaidia.

    2.Usipende kuandika ujinga.
Katika ulimwengu wa sasa, watu wengi hutafuta kuwafahamu wengine katika uelewana hekima kwa vile wanavyoandika kwenye mitandao ya kijamii, kwa hali hiyo waajiri kama serikali na makampuni huhakiki sana watu kabla hawajawaajiri kuwa ni wema.

   3.Usipige picha za ajabu na zisizona maadili.
Hili wote tulishuhudia pale muheshimiwa alipoteua wanawake kadhaa na pindi tuu walipoingia ofisini ghafla picha zao za ajabu zikaibuka mitandaoni zikiwachafua wao na muheshimiwa kwa ujumla akishushiwa hadhi yake.

   4.Usipende kuandika taarifa zinazoonyesha mahali ulipo.
Ni vyema kushare mahali ulipo kama ni pazuri lakini kumbuka kuna waovu wengi wanaweza kuchukulia hiyo kama nafasi ya kukufanyia uhalifu wewe au familia yako ulipoiacha...hizi ni nyakati ngumu.

   5.Usitaje majina ya watu mashuhuri au yeyote yule pale unapoandika kitu.
Sheria ya Tanzania ya mtandao ni kali sana, hata kama mamia wamemtaja wewe unashauriwa usimtaje maana huo ndio utakuwa ushahidi tosha wa kukufunga...Hili limekuwa tatizo hata tunaona muheshimiwa raisi amekuwa akikamata wengi ambao wanamtukana, hafanyi ubabe au hayuko njee ya sheria, yuko katika sheria kabisa na ana haki ya kumshtaki yeyote atakayemnenea vibaya bila kibali chake.

   6.Unapotumiwa picha chafu na mtu yeyote yule futa na umkanye huyo mtu na kama una uwezo nenda hata polisi kama utakuwa hujafuta hizo picha kama unataka huyo mtu akamatwe.

   7.Usikubali kuwa tagged katika post zozote zile za uchochezi au uchafu wowote ule.

  8.Kama una addiction au tatizo la kutumia mitandao hii bila kipimo, vunja kwa kutafuta kitu cha kuchukua nafasi yake hiyo taratibu taratibu..mfano anza kujiuliza taratibu maswali kama "Una hela za kutosha? unaenda wapi? uko wapi?" pia FANYA KAZI,  Omba Mungu akusaidie na incase ACHA UMBEA.
Kutokana na  maendeleo ya kiteknolojia, sio jambo la kuepuka tena kufanya manunuzi kwa njia mtandao wa internet, maana umejaa vitu vya thamani ndogo na vizuri lakini pia umejaa wezi.  Fuatilia haya ili uweze kufanya manunuzi bila kujutia...

  1. Fungua akaunti pekee benki ambayo itatumika kwa ajili ya matumizi hayo ya manunuzi tuu, na uweke hela tuu pale pindi unapotaka kununua vitu, tunafanya hivyo ili endapo akaunti ikafikiwa na wezi wasiweze kuiba chochote.
  2. Pata elimu ya kutosha benki juu ya kitu gani cha kulinda kuhusu taarifa zako.
  3. Nunua sehemu maarufu au kwenye tovuti zinazofahamika dunia nzima kwa manunuzi mfano...GooglePlay, Amazon,eBay na alibaba.
  4. Usimtumie mtu usiyemfahamu taarifa zako za kibenki kwa njia ya email au yeyote ile.
  5. Hakikisha katika browser yako wakati unataka kufanya manunuzi pale kwenye sehemu ya address  imeandikwa au inaanza address kwa njia hii "HTTPS://....." na sio "HTTP://...." ina maana ya kitaalamu "Hyper text transfer protocol secure"
  6. Jiridhishe ya kwamba hiyo ndio tovuti yenyewe au kuna mtu ametengeneza tovuti feki ili kukuibia taarifa zako.
  7. Ukimaliza kufanya manunuzi yako ni vyema zaidi ukafuta browsing history yako yote ili kufuta cookies zenye mabaki ya taarifa zako.
  8. Muone mtaalamu wa Ecommerce ili akusaidie unapotaka kufanya manunuzi makubwa.
Battery hutumika kuendesha umeme ndani ya laptop yako endapo pale unapokuwa hujaichomeka kwenye charge laptop yako.


Uharibifu unaofanyika.
  1. Unapotumia laptop ikiwa imechomekwa kwenye umeme siku nzima bila kuichomoa pale battery inapojaa.
  2. Unaposafiri kwa muda mrefu au kiacha laptop bila kuitumia kwa muda mrefu, na kuiacha battery ya laptop ndani ya laptop bila kuitoa.
  3. Unaponunua adapter feki ili kuchaji battery ya laptop yako.
Ufumbuzi.
  • Laptop ikijaa charge chomoa kwenye umeme na ikiisha chomeka.
  • Ukiona unasumbuka na chomeka chomoa ya hapo juu, tafuta energy management software hiyo itakusadia.
  • Unaposafiri kwa muda mrefu zaidi ya siku moja au kupanga kuto kuitumia laptop yako kwa muda mrefu, chomoa battery ya laptop na uihifadhi mahali salama.
  • Tumia vifaa au adapter original vya laptop husika vyenye meno matatu(Earth,Live and Neutral).
  • Ukiona hali inakuwa mbaya omba msaada.