Katika kozi ambazo zinaongoza kwa watu wake kutokuwa na ajira ni Computer science, Information Technology and nyinginezo za Technology. Ni ajabu lkni ukilinganisha na nature ya ulimwengu wa sasa, ila ndio uhalisia.

Jambo kubwa linalofanya watu hawa kukosa ajira ni kosa ambalo linafanya mavyuoni bila kutambua, vyuo vinajikita katika kuwa expose(funulia) katika ulimwengu mzima wa IT nakusahau kwa fanya wachague mapema sehemu gani wanatakiwa wajikite kwa isiyopungua miaka 2 ya mwisho ya masomo yao.

Kwa kutambua hilo nimejaribu kuchambua maeneo kadhaa unaposoma chuo unahitaji kujikita kulingana na soko halisi huku njee.


Cyber Technology

Hili eneo linahusika na ulimwengu wa Mtandao wa Internet na Network, jinsi gani connection zinafanyika kati ya watu na vifaa na programu mbali mbali, kwa ufupi ukijikita katika cyber technology utajikita zaidi katika ku maintain security ya mifumo isidukuliwe na kulinda data za watu katika mifumo hiyo, hawa watu ni muhimu sana katika kila organization inayotumia mifumo na yenye data nyeti sana mfano serikali, benki na maeneo yanayofanya tafiti na sasa hata chaguzi...

Njia.

Kwanza uwe katika kozi kama computer science au IT,  halafu unatakiwa usomee vyeti vya ujuzi maalumu mfano CompTIA Security+ na Certified Ethical Hacker (CEH) na pia ujichanganye katika mashindano mbali mbali ya mambo hayo yanayotokea ili kujinoa.

Ila vyovyote ufanyavyo unatakiwa uji-update katika Artificial Intelligence maana inachukua nafasi kubwa sana, marobot ndio yanahack siku hizi, na Ai ndio ina ulinzi mkali kuliko watu, so unaweza soma ukashangaa anaajiriwa robot anaitwa Junior kutoka uswisi 😂

KAZI

Peleka CV yako maeneo kama Benki, Nafasi zikitoka serikalini zaidi TCRA, na makampuni ya mitandao ya simu


Application Development

Bila ubishi tunahitaji Apps siku hzi kwa hali na mali na bei ya App moja sasa, unaweza ukajisikia kizungu zungu...kwa sababu wataalamu ni wachache sana na bado tuna mahitaji mengi sana ya App kwa ajili ya mazingira yetu ya Africa, Tanzania.

Njia

Ngoma iko wazi, tutorial lundo mtandaoni chuoni usimuone Prof wa watu yeye ni mkufunzi wewe ndio mhusika haswa na Tech inabadilika kwa speed kubwa sana, ingia website za matorrent badala ya kudownlaod movies download udemy tutorials katika Lugha za Apps kama Javascript na mifumo mbali mbali...YOutube kuna professional watakueleza 1 mpka 10, pa kuanza hadi pa kumaliza.


Server/Computer troubleshooting, maintenance and installation.

Hapa kuna wataalamu wengi ila wamejikita zaidi katika maeneo ya kawaida sana, yaani kutengeneza computer za kawaida tuu, ila katika upande wa servers ni wachache sana, kila kampuni kubwa inahitaji server kuweza kutumia programu za ERP, na nyinginezo nyingi tuu...Lkni pia kutokana na kuboreka kwa mtandao wa Internet, makampuni mengi yamekuwa yakitumia server za njee ya nchi maana kutunza server computer imekuwa gharama sana kuliko kulipa kwa wenye nazo.


Njia

somea Microsoft Certified Solutions Expert (MCSE), CompTIA Server+, Red Hat Certified Engineer (RHCE) na VMware Certified Professional-Data Center Virtualization (VCP-DCV), masomo haya yanapatikana mtandaoni na utabidi ulipie, ili uwe mzuri katika IT ni lazima uingie gharama no shortcut, vyeti hivyo vitakuitisha kwenye interview haraka sana.


Software Sales, maintenance and installations.

Huku unajikita zaidi katika kuuza Programu za kitaalamu, za mifumo mbali mbali ya kuendesha makampuni au taasisi  mfano hospital management, school management, church management N.K 


Njia

Unahitaji unavyosoma uzitatute hizi programu uelewe zinavyofanya kazi na uanze kuziuza, au wewe utengengeneze za kwako. soko lipo kubwa , sehemu nyinginr unahitaji kutoa elimu kabla ya kuuza ila zinahitajika sana hadi sasa.


Network Installations and Maintenance and security.

Eneo hili linahusika na kufunga mtandao kwa njia ya nyaya na bila wire, pamoja na maendeleo makubwa ya teknolojia, badi tunahitaji waya kwa sababu zina ulinzi mzuri wa kuto kutoa nafasi ya kudukuliwa, na pia nimejumuisha kufunga mifumo ya camera za ulinzi kwenye majengo.


Njia

Nenda kasome vyeti vya cisco na pia kaa na wataalamu wa mifumo ya security camera, kama hakuna vyeti hata ujuzi wenyewe unaweza andika katika CV yako ikawa safi sana, na ukapata ajira au kipato haraka.


Computer Rent and sales

Kama una uwezo wa kupata mtaji, fungua duka la kuuza computers au laptops. siku hizi taasisi nyingi zinapenda kukodi computer kwa muda maalumu na kukulipa, kama ukiwa nazo basi utafaidika, anza na kuuza kwanza baadaye ukipata channel nzuri utakodisha, nunua kutoka China maana laptops zimekuwa bei ndgo sana siku hizi.


Professional Software Training.

Sizingumzi kufundisha computer hapa, nazungumzia kufundisha hizi programu za kuendesha taasisi na makampuni mfano za wahasibu, mahospitali, mashule na kadhalika, kuna zile maarufu ukizifahamu zitakufanya uitwe na makampuni kwenda kuziweka, kuziuza na hata kufundisha wafanyakazi wao.


Njia

Jifunze mtandaoni au kama upo kweye sekta mabayo imekuvutia tengeneza mfumo mzuri na uuze kama kuna uhitaji eneo hilo.


Graphics Design

Sanaa ya matangazo ni muhimu siku hzi kwa ukuaji wa biashara, ila imekuwa nyepesi sana maana programu zimekuwa nyepesi kutumia ya kwamba watu wengi wanafanya wao wenyewe. Ila kuna matangazo yanahitaji skills zaidi kama ya Video so jikite huko, nenda mbali zaidi kwenye 3D na motion graphics.

Njia

Youtube ina mafunzo ya kila aina ya programu, tafute mafunzo muhimu ya programu mama kama Adobe Illustrator, Photoshop na Indesign, then hamia katika After effects, Maya, cinema4D na kuendelea kazi zipo nyingi mitandao ya UPwork.



 


Bila shaka App Development(Utengenezaji wa programu za kwenye simu na kompyuta) ni mojawapo ya kazi inayojichotea umaarufu mkubwa sana duniani kwa sasa, tunahitaji wataalamu wengi sana katika upande huu wa teknolojia ukizingatia kila siku zinavyosogea tunazalisha mifumo mingi zaidi ya kutatua changamoto nyingi za kila siku.
Na katika kazi zinazopatikana kwa urahisi ukiwa kokote kule duniani na zenye malipo mazuri basi ni kazi ya App development.

Kutokana na ajira kuwa chache, vijana wengi wamekuwa wakitaka kujikita katika kutengeneza Apps na kubobea katika hii fani wengine wakiwa mavyouni na wengine mtaani, kwa yafuatayo naomba uzingatia kama unataka kuingia katika njia hii.

KUJITENGA

Kazi hii inahitaji kupoteza muda mwingi sana ukikaa mbele ya kompyuta kuandika programu, kwa hali hii inamuhitaji mtu ambaye sio mtokaji sana, yaani mtu anayependa kukaa ndani kwa zaidi ya asilimia 70 ya siku 😕 na ambaye atakuwa teyari kuchelewa kulala kila siku majogoo yaani.

KUWEZA KUFIKIRI HARAKA

Kutokana na kazi imekaa kutatuta changamoto fulani utahitaji kuwa na uwezo wa kufikiri na kutatua matatizo haraka, hataka kama hauna kwa sasa, usijali..unapoendelea ubongo wako utajifunza na kuwa sharp sana katika kutatua changamoto mbali mbali, hii ni nzuri sana.

KUVUNJA MAHUSIANO

Kutokana na kupoteza muda mwingi kufanya shughuli hii especially usiku, "Professor mmoja wa IT aliwaambia wanafunzi wake Oa haraka, zaa haraka zaidi kabla mkeo hajakuacha" 😅 Hawa watu huishia kupata tabu kwenye mahusiano kwa sababu wanakuwa busy sana especially mwanamke gani atapendelea tabia yako ya kukesha...

PESA NYINGI

Yes, sijakosea ukiwa developer mzuri utalipwa katika Dollars, na ukiwa na mawazo endelevu utatengeneza Apps ambazo zitakuingizia pesa kila dakika. so katika yote pes utapata maani si unajua hadi leo ma developer ndio matajiri zaidi duniani kuliko hata ma engineers na kadhalika, uwe unajifunza na kuwekeza mapema kabla umri haujakutupa.

MUDA

Kuna watu wanakuwa na vichwa vizuri na kuendelea na coding maisha yao yote, ila umri wa kufanya coding huwa from 13th mpka miaka 28 hivi, baada ya hapo unahitaji kuwa umeshajiendeleza vya kutosha na kuanza either kuajili watu vijana wafanye na uwalipe au ufanye shughuli nyingine maana utaanza kuwa na majukumu mengi.

MATATIZO YA KIAFYA

Ndgu yangu nini marafiki mpka wamefanyiwa operation za mgongo, ni tatizo moja kubwa sana kwa kukaa kwenye kiti kwa muda mrefu, na kibaya unakuwa hata hujua ya kwamba muda unasogea unashtuka tuu teyari yamepita masaa 6 umekaa tuu, pia uzito ulipitiliza kwa kutofanya mizunguko ya kutosha ni muhimu sana kufanya mazoezi kwa ulazima kuanzia mara 4 kwa wiki.


Kwa haya machache kama Developer pia na Trainer ningependa kuwashauri vijana, kama ni wa kike kuwa makini na muda maana wao ndio wana muda wa kuolewa kwa hiyo usijikute umekaa ndani mpka unashindwa kuonekana na Hamisi wa kutokea Uluguru huko akuoe...😆