Tofauti kati ya IT na ICT

Hapo awali kulikuwa na ulimwengu tofauti wa Computer na Mawasiliano,  Ulimwengu wa computer ulitumia njia zake ndani ya njia za mawasiliano, na haukufananishwa sana na mawasiliano kwa sababu  tulitumia computer kufanya mambo makubwa sana na kidgo sana kuwasiliana na hiyo ni kutokana na kutokuwa na urahisi wa kupata na kutumia computer ndio maana ulikuwa umejiweka tofauti...(SImu zote za smartphone ni computer hizo, kama laptop na desktops)
Sasa tunavyozidi kwenda mbele computer zimekuwa gharama nafuu na ndio zimekuwa njia kuu za mawasiliano, na ndio maana kwa ufupi tunaondoka katika kuita tuu IT(information technology) na kuita ICT(information Communication Technology)

Angalizo.
Natumia lugha nyepesi ili kila mtu aelewe, kuna vitu vingi vya kitaalamu nitaviacha.

IT(INFORMATION TECHNOLOGY)
Huu ni ulimwengu wa computer ambao kwa sasa una maanisha mifumo ya computer inayoendesha biashara, taasisi, mabenki n.k lakini unajumuisha fani mbali mbali kama systems administrator, programming, system analysis, computer science, database administration n.k..

ICT(Information Communication Technology)
Huu ni uwanda wa IT lakni ambao umeongezewa mawasiliano ndani yake. Hapo awali kulikuwa na field iliyokuwa inaitwa Telecommunication ambayo ilikuwa inajikita katika njia za mawasiliano. Mfano hawa watu unawaona wana deal na minara ya simu, nyaya huwa tunawaita telecommunication engineers lakni katika IT kuna watu hao wanadili na Network ila wao tunawaita Network engineers.

Kufupisha zaidi ICT ni pana zaidi na inajumisha field yote IT pamoja na njia za mawasiliano.

Ila ieleweke watu wa telecomunications ni tofauti kabisa na watu wa IT hata wanavyosema na kazi zao hawawezi kubadilishana.

Pia term ya ICT inatumika tuu katika kutoa Elimu ya IT na mawasiliano lakini katika kikazi zaidi tunatumia IT.
Unaweza soma kozi ya bachelor of science in ICT, lakni ukimaliza usije ukajiita wewe ni ICT professional utatia aibu, wewe katika field wewe ni IT professional.

Kwa hiyo hili wimbi la ma Vyuo kubadili majina ya course kutoka IT kwenda ICT lisikutishe, ujue tuu hiyo term ya ICT inatumika zaidi katika Elimu, ila ukimaliza wewe ni IT kama kawaida.



Kwa Maelezo zaidi wasiliana nami kupitia elisanteshibanda@yahoo.com. au jiunge la MAXPO Tanzania ukutane na wataalamu wengine wa IT.