Tunavyosoma Chuoni, mavyuo hujitahidi kukupa uwezo kutambua maeneo mengi iwezekanavyo ya Information Technology, na wanafanya hivyo kwa dhumuni zuri la kukuhakikishia unaelewa kwa asilimia kubwa kitu gani kinaendelea katika maeneo mbali mbali ya IT.

Tatizo linakuja pale unapochukua hiyo elimu ambayo huwa ni fupi(shallow), kutoka nayo huku njee ukiamini ya kwamba umepata elimu, na hapo ndio soko la ajira linakuona hufai na hauna chochote cha maana cha kuwasaidia.


Mfano:

Unaposoma Network ukamaliza ukirudi kwenye soko la ajira, wewe bado sio mtaalamu wa Network, unahitaji vyeti vya CISCO, SERVERS, ETHICAL HACKING etc hapo ndio utapata kipaumbele na utakuwa na practical knowledge ya Networking katika IT.


Suluhisho:

  • Wakati ukiwa Chuoni, soma hivyo vyeti vingine mtandaoni kama nivyoviainisha hapo juu, na zaidi katika kila maeneo vingine ni bure, vingine vitakugharimu.

Note: 

Chagua wapi kwa kubobea na sio usome coding, network umo, hapana...chagua sehemu then bobea kuelekea huko...na gharama zitapoa pia.

  

  • Hudhuria semina na michuano ya IT Tech world mfano  hackathon ambapo watu wa IT zaidi wanafunzi hukutanika nakutengeneza Apps kwa muda mfupi huko utajifunza mengi...mara ya mwisho CRDB na makampuni mengi yalijitokeza kudhamini tukio mojawapo hapa Dar es salaam.

  • Jiunge na TECH Hubs zenye Uhai maana huko utapata ma IT wengi mnaweza hata kukutana na mkapata wazo la kufanya jambo fulani la IT kuliko kukaa mtaani na wabeba zege wanaojiona wao ni bora kuliko wewe.

  • Kama utafanikiwa tafuta field kwenye kampuni za IT, ila ukishindwa achana nayo maana na wenyewe huwa ni wagumu sana kutoa field kwa wanafunzi.

  • Kikubwa zaidi kumbuka chuo kinakupa 25% tuu ya maarifa, shughulika kupata mengine kabla hujatoka uanze kukataliwa kila mahali.

  • Jiunge na online communities za Tech, mfano mzuri ni GitHub huko unaweza changia hata open source software na zaidi...na mengine mengi.


 

Katika kozi ambazo zinaongoza kwa watu wake kutokuwa na ajira ni Computer science, Information Technology and nyinginezo za Technology. Ni ajabu lkni ukilinganisha na nature ya ulimwengu wa sasa, ila ndio uhalisia.

Jambo kubwa linalofanya watu hawa kukosa ajira ni kosa ambalo linafanya mavyuoni bila kutambua, vyuo vinajikita katika kuwa expose(funulia) katika ulimwengu mzima wa IT nakusahau kwa fanya wachague mapema sehemu gani wanatakiwa wajikite kwa isiyopungua miaka 2 ya mwisho ya masomo yao.

Kwa kutambua hilo nimejaribu kuchambua maeneo kadhaa unaposoma chuo unahitaji kujikita kulingana na soko halisi huku njee.


Cyber Technology

Hili eneo linahusika na ulimwengu wa Mtandao wa Internet na Network, jinsi gani connection zinafanyika kati ya watu na vifaa na programu mbali mbali, kwa ufupi ukijikita katika cyber technology utajikita zaidi katika ku maintain security ya mifumo isidukuliwe na kulinda data za watu katika mifumo hiyo, hawa watu ni muhimu sana katika kila organization inayotumia mifumo na yenye data nyeti sana mfano serikali, benki na maeneo yanayofanya tafiti na sasa hata chaguzi...

Njia.

Kwanza uwe katika kozi kama computer science au IT,  halafu unatakiwa usomee vyeti vya ujuzi maalumu mfano CompTIA Security+ na Certified Ethical Hacker (CEH) na pia ujichanganye katika mashindano mbali mbali ya mambo hayo yanayotokea ili kujinoa.

Ila vyovyote ufanyavyo unatakiwa uji-update katika Artificial Intelligence maana inachukua nafasi kubwa sana, marobot ndio yanahack siku hizi, na Ai ndio ina ulinzi mkali kuliko watu, so unaweza soma ukashangaa anaajiriwa robot anaitwa Junior kutoka uswisi 😂

KAZI

Peleka CV yako maeneo kama Benki, Nafasi zikitoka serikalini zaidi TCRA, na makampuni ya mitandao ya simu


Application Development

Bila ubishi tunahitaji Apps siku hzi kwa hali na mali na bei ya App moja sasa, unaweza ukajisikia kizungu zungu...kwa sababu wataalamu ni wachache sana na bado tuna mahitaji mengi sana ya App kwa ajili ya mazingira yetu ya Africa, Tanzania.

Njia

Ngoma iko wazi, tutorial lundo mtandaoni chuoni usimuone Prof wa watu yeye ni mkufunzi wewe ndio mhusika haswa na Tech inabadilika kwa speed kubwa sana, ingia website za matorrent badala ya kudownlaod movies download udemy tutorials katika Lugha za Apps kama Javascript na mifumo mbali mbali...YOutube kuna professional watakueleza 1 mpka 10, pa kuanza hadi pa kumaliza.


Server/Computer troubleshooting, maintenance and installation.

Hapa kuna wataalamu wengi ila wamejikita zaidi katika maeneo ya kawaida sana, yaani kutengeneza computer za kawaida tuu, ila katika upande wa servers ni wachache sana, kila kampuni kubwa inahitaji server kuweza kutumia programu za ERP, na nyinginezo nyingi tuu...Lkni pia kutokana na kuboreka kwa mtandao wa Internet, makampuni mengi yamekuwa yakitumia server za njee ya nchi maana kutunza server computer imekuwa gharama sana kuliko kulipa kwa wenye nazo.


Njia

somea Microsoft Certified Solutions Expert (MCSE), CompTIA Server+, Red Hat Certified Engineer (RHCE) na VMware Certified Professional-Data Center Virtualization (VCP-DCV), masomo haya yanapatikana mtandaoni na utabidi ulipie, ili uwe mzuri katika IT ni lazima uingie gharama no shortcut, vyeti hivyo vitakuitisha kwenye interview haraka sana.


Software Sales, maintenance and installations.

Huku unajikita zaidi katika kuuza Programu za kitaalamu, za mifumo mbali mbali ya kuendesha makampuni au taasisi  mfano hospital management, school management, church management N.K 


Njia

Unahitaji unavyosoma uzitatute hizi programu uelewe zinavyofanya kazi na uanze kuziuza, au wewe utengengeneze za kwako. soko lipo kubwa , sehemu nyinginr unahitaji kutoa elimu kabla ya kuuza ila zinahitajika sana hadi sasa.


Network Installations and Maintenance and security.

Eneo hili linahusika na kufunga mtandao kwa njia ya nyaya na bila wire, pamoja na maendeleo makubwa ya teknolojia, badi tunahitaji waya kwa sababu zina ulinzi mzuri wa kuto kutoa nafasi ya kudukuliwa, na pia nimejumuisha kufunga mifumo ya camera za ulinzi kwenye majengo.


Njia

Nenda kasome vyeti vya cisco na pia kaa na wataalamu wa mifumo ya security camera, kama hakuna vyeti hata ujuzi wenyewe unaweza andika katika CV yako ikawa safi sana, na ukapata ajira au kipato haraka.


Computer Rent and sales

Kama una uwezo wa kupata mtaji, fungua duka la kuuza computers au laptops. siku hizi taasisi nyingi zinapenda kukodi computer kwa muda maalumu na kukulipa, kama ukiwa nazo basi utafaidika, anza na kuuza kwanza baadaye ukipata channel nzuri utakodisha, nunua kutoka China maana laptops zimekuwa bei ndgo sana siku hizi.


Professional Software Training.

Sizingumzi kufundisha computer hapa, nazungumzia kufundisha hizi programu za kuendesha taasisi na makampuni mfano za wahasibu, mahospitali, mashule na kadhalika, kuna zile maarufu ukizifahamu zitakufanya uitwe na makampuni kwenda kuziweka, kuziuza na hata kufundisha wafanyakazi wao.


Njia

Jifunze mtandaoni au kama upo kweye sekta mabayo imekuvutia tengeneza mfumo mzuri na uuze kama kuna uhitaji eneo hilo.


Graphics Design

Sanaa ya matangazo ni muhimu siku hzi kwa ukuaji wa biashara, ila imekuwa nyepesi sana maana programu zimekuwa nyepesi kutumia ya kwamba watu wengi wanafanya wao wenyewe. Ila kuna matangazo yanahitaji skills zaidi kama ya Video so jikite huko, nenda mbali zaidi kwenye 3D na motion graphics.

Njia

Youtube ina mafunzo ya kila aina ya programu, tafute mafunzo muhimu ya programu mama kama Adobe Illustrator, Photoshop na Indesign, then hamia katika After effects, Maya, cinema4D na kuendelea kazi zipo nyingi mitandao ya UPwork.



 


Bila shaka App Development(Utengenezaji wa programu za kwenye simu na kompyuta) ni mojawapo ya kazi inayojichotea umaarufu mkubwa sana duniani kwa sasa, tunahitaji wataalamu wengi sana katika upande huu wa teknolojia ukizingatia kila siku zinavyosogea tunazalisha mifumo mingi zaidi ya kutatua changamoto nyingi za kila siku.
Na katika kazi zinazopatikana kwa urahisi ukiwa kokote kule duniani na zenye malipo mazuri basi ni kazi ya App development.

Kutokana na ajira kuwa chache, vijana wengi wamekuwa wakitaka kujikita katika kutengeneza Apps na kubobea katika hii fani wengine wakiwa mavyouni na wengine mtaani, kwa yafuatayo naomba uzingatia kama unataka kuingia katika njia hii.

KUJITENGA

Kazi hii inahitaji kupoteza muda mwingi sana ukikaa mbele ya kompyuta kuandika programu, kwa hali hii inamuhitaji mtu ambaye sio mtokaji sana, yaani mtu anayependa kukaa ndani kwa zaidi ya asilimia 70 ya siku 😕 na ambaye atakuwa teyari kuchelewa kulala kila siku majogoo yaani.

KUWEZA KUFIKIRI HARAKA

Kutokana na kazi imekaa kutatuta changamoto fulani utahitaji kuwa na uwezo wa kufikiri na kutatua matatizo haraka, hataka kama hauna kwa sasa, usijali..unapoendelea ubongo wako utajifunza na kuwa sharp sana katika kutatua changamoto mbali mbali, hii ni nzuri sana.

KUVUNJA MAHUSIANO

Kutokana na kupoteza muda mwingi kufanya shughuli hii especially usiku, "Professor mmoja wa IT aliwaambia wanafunzi wake Oa haraka, zaa haraka zaidi kabla mkeo hajakuacha" 😅 Hawa watu huishia kupata tabu kwenye mahusiano kwa sababu wanakuwa busy sana especially mwanamke gani atapendelea tabia yako ya kukesha...

PESA NYINGI

Yes, sijakosea ukiwa developer mzuri utalipwa katika Dollars, na ukiwa na mawazo endelevu utatengeneza Apps ambazo zitakuingizia pesa kila dakika. so katika yote pes utapata maani si unajua hadi leo ma developer ndio matajiri zaidi duniani kuliko hata ma engineers na kadhalika, uwe unajifunza na kuwekeza mapema kabla umri haujakutupa.

MUDA

Kuna watu wanakuwa na vichwa vizuri na kuendelea na coding maisha yao yote, ila umri wa kufanya coding huwa from 13th mpka miaka 28 hivi, baada ya hapo unahitaji kuwa umeshajiendeleza vya kutosha na kuanza either kuajili watu vijana wafanye na uwalipe au ufanye shughuli nyingine maana utaanza kuwa na majukumu mengi.

MATATIZO YA KIAFYA

Ndgu yangu nini marafiki mpka wamefanyiwa operation za mgongo, ni tatizo moja kubwa sana kwa kukaa kwenye kiti kwa muda mrefu, na kibaya unakuwa hata hujua ya kwamba muda unasogea unashtuka tuu teyari yamepita masaa 6 umekaa tuu, pia uzito ulipitiliza kwa kutofanya mizunguko ya kutosha ni muhimu sana kufanya mazoezi kwa ulazima kuanzia mara 4 kwa wiki.


Kwa haya machache kama Developer pia na Trainer ningependa kuwashauri vijana, kama ni wa kike kuwa makini na muda maana wao ndio wana muda wa kuolewa kwa hiyo usijikute umekaa ndani mpka unashindwa kuonekana na Hamisi wa kutokea Uluguru huko akuoe...😆




 


Project ni kitu muhimu sana katika kutimiza masomo ya kozi ya IT/Computer Science/Comp Eng./Software Eng etc ila pia inaweza kukusaidia kukutoa kimaisha ukiwa chuoni na hata baada ya kumaliza chuo.

MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA:

  • Kupata wazo jipya kabisa ambalo halijawahi kufanyika, haiwezekani kwa 78%.
  • Programu au App inayofanya kazi na kupendwa na watu Ulaya, inaweza isifanye kazi vizuri Africa..sababu ni Tamaduni, miundo mbinu..etc.
  • Sio kila wazo la Tech, haijalishi ni zuri kiasi gani, ni muda wake, mengine watu wanaweza wasilipokee au wasilipende kwa sababu tuu ya muda bado.
  • Mawazo mazuri sio lazima yawe "complicated"magumu yaani hata tech yake, coding lundo...Hell No 😤 Issue ya muhimu ni moja tuu, kurahisisha utendaji wa kazi, na tumia technolojia ya bure kwa nafasi kubwa sana...
  • Kuchukua wazo la mtu na kuliboresha ni ubunifu pia, ila vizuri uombe kibali na pia uliboreshe kwa viwango vya hali ya juu isije ikaonekana umecopy tuu.
  • Ukitaka baadaye uwe unafanya software development, hakikisha kwenye project unajifunza ku code, yaani wewe ndio uwe mwandika code, usifanye uhuni wa kurukia rukia na kuwaachia wengine.
  • Usipende shortcuts katika coding, itakufanya ushidwe kudevelop uwezo mzuri wa kuandika programu baadaye.
  • Usiogope kupresent wazo, kwa sababu litatumia lugha nyingi au hujui utatumia lugha ghani ya computer kulitimiza, niamini utapata tuu lugha za kutumia, na utajifunza vizuri na utaweza bila shida yeyote...nimepita hapo naelewa pressure yake unaweza unahisi unataka kuaga dunia..😂
  • Sio lazima uwe programmer kama ni kiongozi mzuri unaweza tengeneza Team na ukasonga mbele😎 ila Programmer akisusa utajuta.😥
  • Mawazo mazuri ya Project ni matatizo ya kila siku, katika maeneo ya kazi, katika jamii..mfano tunaona Uber ni mtu aliona matax yanazingua..etc.

Muhimu kuliko vyote RELAAAAXXXXX...mambo yatakuwa  sawa tuu..


Kama una wazo la project na unatafuta mtu kupata kujua utalifanyaje na lugha ghani utumie wasiliana nami kupitia email yangu ya elisanteshibanda@yahoo.com, kuwa mpole utajibiwa 





 

Field training/ mafunzo ya vitendo ni muhimu sana, kama mojawapo ya mafunzo ya degree/diploma na umuhimu wake upo katika;

  1. Kukusaidia kujua sehemu ya kubobea katika profession yako ya IT.
  2. Kupata ujuzi wa kwanza wa kuweka katika CV yako, kuna tofauti unaposema umefanya field MIcrosoft Tanzania na serikali ya Mtaa wa kwa Tumbo😜
  3. Kufahamu ujuzi gani una soko  zaidi ndani ya IT.
  4. Kukusaidia kupata connection na waajiri, na kukutanisha na IT Professionals.

Vigezo vya sehemu ya kufanya field bora.

  1. Kuwe na kitengo cha IT imara katika sehemu zifuatazo kama Networking, computers configuration and maintenance, software/web development, graphics design  au Tech Training(Universities/colleges)

Networking:

Nenda kwa makampuni ya Networks au ISP(Internet service Providers) mfano Raha Telecom, Simba Networks ila sehemu nyepesi na nzuri zaidi kupata ni TTCL.


Computer Config. and Maintenance:

Nenda kwa wauzaji na wasambazaji wa computers kwa ukubwa na kwa mafundi wa computer though hii fani haina malipo makubwa sana katika Tech. labda kuwe na tenda za kufanya haya mambo katika makampuni.

Software/Web develop.

Nenda kwenye makampuni yanayotengeneza Apps and websites mfano shule soft, Nyumbani creative, smart codes na mengine mengi.
Note.
Makampuni haya huwa na wafanyakazi wachache sana so huwa hawachukui sana trainees, na wakikuchukua huwa hawana muda wa kumfundisha mtu sana sasa ujitume kweli kujifunze huku ukiwauliza maswali ya hapa na pale.

Graphics Design:

Nenda kwenye makampuni ya habari kama TBC, ITV na TV nyingine zinazotengeneza matangazo kwa wingi hata kama ni za mtandaoni.

PLAN B

Umetafuta field umekosa kabisa, muda unakwenda na chuo kinaweza  kikakuzingua, nenda sehemu ambayo haina hata IT kabisa, 
 ila iwe na Internet ya Maana nzuri , mfano halmashauri nyingi siku hizi zina network na ziko safi,  pale utajaziwa fomu zako,  ila  tumia  muda wako na internet yao kusoma online courses  za programming na vinginevyo yaani utatoka bomba kuliko hata hao waliopata field microsoft....na utaweza kufanya kazi za mtandaoni(Freelancing) kabla hata ya kumaliza chuo...na unaweza anzisha kampuni yako baadaye ni wewe tuu.


USHAURI WANGU KUPITIA MAPITO YANGU BINAFSI

Kwa kipindi tulicho nacho sasa, PLAN B ni bora zaidi, makazini na makampuni makubwa mengi hayakupi nafasi za kujifunza sana, na pia ajira nyingi siku hizi ni za freelancing kuna vijana wanapata mamilioni kwa mwezi kuwashinda hata wale waliojariwa.
chagua kipi bora ila unaweza fanya vyote pia plan A na Plan B ila tuu ujitoe kweli kweli.


SEHEMU ZISIZOFAA KWENDA FIELD

Benki:

Kwa sababu ya usalama hawatakuruhusu katika mifumo yako so utabakia kuwa mapokezi na hiyo inaboa sana.

Mashuleni:
utaishia kutengeneza kompyuta ya mwalimu mkuu na lab ambayo ina  kompyuta hovyo sana.

Serikali za mtaa.

Sehemu ambazo kuna LAN na INTERNET nenda kafanye plan B, ila tuu pakiwa haposomeki usiende.

Sehemu zote zenye matumizi madogo ya Tech usiende.

Tumia  muda vizuri, wahi na kuwa mwepesi wa kujifunza na tengeneza connection ukiwa huko, unaweza ukaitwa tena kama ni private.

Kama una maswali zaidi nitumie katika email yangu ya  elisanteshibanda@yahoo.com


 


Tofauti kati ya IT na ICT

Hapo awali kulikuwa na ulimwengu tofauti wa Computer na Mawasiliano,  Ulimwengu wa computer ulitumia njia zake ndani ya njia za mawasiliano, na haukufananishwa sana na mawasiliano kwa sababu  tulitumia computer kufanya mambo makubwa sana na kidgo sana kuwasiliana na hiyo ni kutokana na kutokuwa na urahisi wa kupata na kutumia computer ndio maana ulikuwa umejiweka tofauti...(SImu zote za smartphone ni computer hizo, kama laptop na desktops)
Sasa tunavyozidi kwenda mbele computer zimekuwa gharama nafuu na ndio zimekuwa njia kuu za mawasiliano, na ndio maana kwa ufupi tunaondoka katika kuita tuu IT(information technology) na kuita ICT(information Communication Technology)

Angalizo.
Natumia lugha nyepesi ili kila mtu aelewe, kuna vitu vingi vya kitaalamu nitaviacha.

IT(INFORMATION TECHNOLOGY)
Huu ni ulimwengu wa computer ambao kwa sasa una maanisha mifumo ya computer inayoendesha biashara, taasisi, mabenki n.k lakini unajumuisha fani mbali mbali kama systems administrator, programming, system analysis, computer science, database administration n.k..

ICT(Information Communication Technology)
Huu ni uwanda wa IT lakni ambao umeongezewa mawasiliano ndani yake. Hapo awali kulikuwa na field iliyokuwa inaitwa Telecommunication ambayo ilikuwa inajikita katika njia za mawasiliano. Mfano hawa watu unawaona wana deal na minara ya simu, nyaya huwa tunawaita telecommunication engineers lakni katika IT kuna watu hao wanadili na Network ila wao tunawaita Network engineers.

Kufupisha zaidi ICT ni pana zaidi na inajumisha field yote IT pamoja na njia za mawasiliano.

Ila ieleweke watu wa telecomunications ni tofauti kabisa na watu wa IT hata wanavyosema na kazi zao hawawezi kubadilishana.

Pia term ya ICT inatumika tuu katika kutoa Elimu ya IT na mawasiliano lakini katika kikazi zaidi tunatumia IT.
Unaweza soma kozi ya bachelor of science in ICT, lakni ukimaliza usije ukajiita wewe ni ICT professional utatia aibu, wewe katika field wewe ni IT professional.

Kwa hiyo hili wimbi la ma Vyuo kubadili majina ya course kutoka IT kwenda ICT lisikutishe, ujue tuu hiyo term ya ICT inatumika zaidi katika Elimu, ila ukimaliza wewe ni IT kama kawaida.



Kwa Maelezo zaidi wasiliana nami kupitia elisanteshibanda@yahoo.com. au jiunge la MAXPO Tanzania ukutane na wataalamu wengine wa IT.


 


Ninachopenda kuhusu IT na fani hii kwa ujumla ni jinsi ilivyo na uwezo kumpa mtu yeyote fursa ya kufanikiwa na jinsi ilivyounganisha dunia nzima.
katika miaka ya karibuni Watu na makampuni mashuhuri makubwa yamekuwa yakija Africa na Asia na hata Ulaya pia kufanya mashindano ya kutafuta watu wenye mawazo makubwa yanayoweza kugeuka biashara kubwa na pia kutatua changamoto duniani, yote katika fani ya teknolojia.

Vigezo

  • Uwe na biashara/kampuni ya IT, yenye wazo zuri ambalo limeshaanza kufanya kazi, na maanisha kama una software uwe umshatengeneza atlleast linaonekana au kama ni tech nyingine basi umeshaanza ku operate na watu wameipokea ila hauna uwezo wa kukua kibiashara.

  • Usiwe peke yako tuu, kuanzia wawili au watatu(Tech IT, Business, Administration)

  • Uwe na uwezo mzuri wa kujieleza kiingereza kwa maaana utakutana na watu kutoka mataifa yote duniani.

  • Uwe na ujasiri wakusimama mbele za watu wengi na kutetea wazo lako.

  • Hakikisha wazo lako liwe kweli linatatua changamoto ambayo inaikabili jamii, iili watu wakimbilie kununua solution yako haraka.

Mashindano hayo ni kama yafuatayo, yabonyeze vichwa vyake vya habari kujua zaidi...

MEST AFRICA CHALLENGE



START UP WORLD CUP



NETPRENEUR PRIZE



PROPTECH INNOVATION AWARD







START PRIZE



START UP ENERGY TRANSITION AWARD


 
Watanzania waliowahi kushinda mashindano haya ni


Wengine tumeshiriki ila hatukufanikiwa (MEST AFRICA) safari bado inaendelea, ila kuna wengine wengi zaidi wameshinda ila sina taarifa zao kama wewe umeshawahi kushiriki naomba unitafute tuongeze maelezo zaidi ili wengi wapate mwanga zaidi.