Miundo Mbali mbali ya maswali ya interview za mchujo zinazoendelea kufanyika nchini na jinsi ya kujiandaa kuzikabili.



Interview za mchujo ni interview za awali, ambazo hutumika kupunguza watu wengi walioomba kazi husika,

ili wabaki wachache kwa ajili ya hatua ya pili ya interview(usaili).
Interview hizi zina sifa kubwa sana ya kuvunja mioyo ya watu walioomba kazi, kwa watu wengi hujikuta wamejiandaa visivyo na kufanya vibaya.



Hebu kwanza tufahamu mambo ya kuzingatia unavyojiandaa na interview.


Muombe Mungu akusaidie kujibu kwa ufasaha, maana ni rahisi sana kujibu visivyo, pamoja ya kuwa unajua kila kitu.



Fahamu kwa undani kazi iliyotangazwa. Ni rahisi kusema, mimi nimesoma chuo kama IT, Computer science N.K na ndio maana kozi yangu imeorodhoshwa na nikaitwa, 
ila kufikiri huko sio sahihi na wengi hufeli maswali yanayohusiana na kazi hiyo. 
Fanya utafiti wa hali ya juu kwenye mtandao au kwa waliokwisha fanya teyari na uelewe.

kozi za IT Tanzania na Soko lake

Fahamu majukumu yaliyotangazwa na kazi husika na uhakikishe unayafahamu jinsi ya kuyatekeleza yote
au kama ukishidwa yote angalau ujue nini kinaendelea,     kwa maana maswali mengine hulenga humo.


Fahamu ni masomo/kozi gani yanayoendana na kazi husika,uliyoyasoma chuoni, halafu uyapitie kwa umakini.



MIUNDO YA MASWALI YA INTERVIEW(USAILI)

Muundo wa 1

Muundo huu utakutana na maswali 40 hadi 50, yanayokuwa ya kuchagua, na huwa yanagusa sehemu mbali mbali, ila zaidi sehemu zinazohusiana na kazi husika na sub course husika mojawapo huonekana kwa wingi.

Mfano:
Kazi ya Business analyst, maswali mengi asilimia 60-70 yatakuwa ya software engineering.

Jinsi ya kujiandaa:
Tafuta subcourse husika na uisome sana gusia maeneo mengine pia.

Muundo wa 2

Muundo huwa na maswali 4 hadi 5, ila maswali huwa yanalenga maeneo husika na yale ya kuzunguka.

Mfano:
System Administrator, maswali 2 yatahusiana na Networking lakini 2 mengine yawaweza kugusa database na hardware.

Jinsi ya kujiandaa:
Soma yote yanayoendana na kozi husika na course zinazoendana na hiyo course.

Muundo wa 3

Muundo huu una maswali 4 hadi 5, na maswali hugusa course husika tuu na huulizwa kwa mfumo wa maswali ya scenario.
Mfano:
System Administrator, maswali yote ni ya networking, na yanaulizwa yakitakiwa kujibiwa kitaalamu na sio kitaaluma
Namaanisha kitaalumu ujibu kama mtu mwenye ujuzi na scenario hiyo  na sio kama mtu aliyakariri kutoka kwenye kitabu. 

Jinsi ya kujiandaa:
kama una uzoefu kumbuka uzoefu wako, kama una mafunzo ya certifications yatumie ipasavyo, lakni kama huna hivyo vyote usijali jiandae vyema na sub course husika nawe utafanikiwa.

Muundo wa 4

Muundo huu huwa na maswali 4 hadi 5, ambayo hujikita zaidi kitaalamu na katika majukumu yaliyorodheshwa na tangazo la kazi.

Jinsi ya Kujiandaa:
Soma kwa umakini yale majukumu ujue jinsi ya kuyatimiliza kivitendo kila moja na kama kuna vigezo vipitie hata ujue tuu kwa mbali nini kinaendelea.

Angalizo:
Ni kawaida kabisa kumaliza mtihani huu usijue kama umefaulu au umefeli, na hali hii huifanya ionekane ngumu sana, ila kabla ya kujibu swali tafakari linahitaji nini na ujibu vizuri ukujibu juu juu uamini kuna watu watajibu kwa umakini kuliko wewe.


Hiyo ni muundo ambayo imekuwapo ila inaweza badilika muda wowote hata kesho ikaja mengine zaidi, na sijakugusia interview za awamu ya pili na za mahojiano,ila kwa hayo chukua hatua, na nikutakie interview njema.
Kwa ushauri zaidi wasiliana nami 


Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   




1 comment:

  1. Je nitapataje maswali ya interview zilizopita za umeme

    ReplyDelete