Usifanye haya kwenye mitandao ya kijamii kwa usalama wako na wa unaowajali!!

  1. Usiishi katika mitandao ya kijamii HAMNA MAISHA HUKO UNAJIDANGANYA TUU!!
Siku ina masaa 24, usitumie masaa mengi huko maana sio maisha halisi kama unavyodhani. kaa na watu unaowajali zaidi, watu halisi wa karibu yako ie majirani,utakapoumwa au kuwa na tatizo la ghafla huyo rafiki yako mbelgiji au mnamibia au muafrika ya kusini hataweza kukusaidia.

    2.Usipende kuandika ujinga.
Katika ulimwengu wa sasa, watu wengi hutafuta kuwafahamu wengine katika uelewana hekima kwa vile wanavyoandika kwenye mitandao ya kijamii, kwa hali hiyo waajiri kama serikali na makampuni huhakiki sana watu kabla hawajawaajiri kuwa ni wema.

   3.Usipige picha za ajabu na zisizona maadili.
Hili wote tulishuhudia pale muheshimiwa alipoteua wanawake kadhaa na pindi tuu walipoingia ofisini ghafla picha zao za ajabu zikaibuka mitandaoni zikiwachafua wao na muheshimiwa kwa ujumla akishushiwa hadhi yake.

   4.Usipende kuandika taarifa zinazoonyesha mahali ulipo.
Ni vyema kushare mahali ulipo kama ni pazuri lakini kumbuka kuna waovu wengi wanaweza kuchukulia hiyo kama nafasi ya kukufanyia uhalifu wewe au familia yako ulipoiacha...hizi ni nyakati ngumu.

   5.Usitaje majina ya watu mashuhuri au yeyote yule pale unapoandika kitu.
Sheria ya Tanzania ya mtandao ni kali sana, hata kama mamia wamemtaja wewe unashauriwa usimtaje maana huo ndio utakuwa ushahidi tosha wa kukufunga...Hili limekuwa tatizo hata tunaona muheshimiwa raisi amekuwa akikamata wengi ambao wanamtukana, hafanyi ubabe au hayuko njee ya sheria, yuko katika sheria kabisa na ana haki ya kumshtaki yeyote atakayemnenea vibaya bila kibali chake.

   6.Unapotumiwa picha chafu na mtu yeyote yule futa na umkanye huyo mtu na kama una uwezo nenda hata polisi kama utakuwa hujafuta hizo picha kama unataka huyo mtu akamatwe.

   7.Usikubali kuwa tagged katika post zozote zile za uchochezi au uchafu wowote ule.

  8.Kama una addiction au tatizo la kutumia mitandao hii bila kipimo, vunja kwa kutafuta kitu cha kuchukua nafasi yake hiyo taratibu taratibu..mfano anza kujiuliza taratibu maswali kama "Una hela za kutosha? unaenda wapi? uko wapi?" pia FANYA KAZI,  Omba Mungu akusaidie na incase ACHA UMBEA.

0 comments:

Post a Comment