Tunavyosoma Chuoni, mavyuo hujitahidi kukupa uwezo kutambua maeneo mengi iwezekanavyo ya Information Technology, na wanafanya hivyo kwa dhumuni zuri la kukuhakikishia unaelewa kwa asilimia kubwa kitu gani kinaendelea katika maeneo mbali mbali ya IT.

Tatizo linakuja pale unapochukua hiyo elimu ambayo huwa ni fupi(shallow), kutoka nayo huku njee ukiamini ya kwamba umepata elimu, na hapo ndio soko la ajira linakuona hufai na hauna chochote cha maana cha kuwasaidia.


Mfano:

Unaposoma Network ukamaliza ukirudi kwenye soko la ajira, wewe bado sio mtaalamu wa Network, unahitaji vyeti vya CISCO, SERVERS, ETHICAL HACKING etc hapo ndio utapata kipaumbele na utakuwa na practical knowledge ya Networking katika IT.


Suluhisho:

  • Wakati ukiwa Chuoni, soma hivyo vyeti vingine mtandaoni kama nivyoviainisha hapo juu, na zaidi katika kila maeneo vingine ni bure, vingine vitakugharimu.

Note: 

Chagua wapi kwa kubobea na sio usome coding, network umo, hapana...chagua sehemu then bobea kuelekea huko...na gharama zitapoa pia.

  

  • Hudhuria semina na michuano ya IT Tech world mfano  hackathon ambapo watu wa IT zaidi wanafunzi hukutanika nakutengeneza Apps kwa muda mfupi huko utajifunza mengi...mara ya mwisho CRDB na makampuni mengi yalijitokeza kudhamini tukio mojawapo hapa Dar es salaam.

  • Jiunge na TECH Hubs zenye Uhai maana huko utapata ma IT wengi mnaweza hata kukutana na mkapata wazo la kufanya jambo fulani la IT kuliko kukaa mtaani na wabeba zege wanaojiona wao ni bora kuliko wewe.

  • Kama utafanikiwa tafuta field kwenye kampuni za IT, ila ukishindwa achana nayo maana na wenyewe huwa ni wagumu sana kutoa field kwa wanafunzi.

  • Kikubwa zaidi kumbuka chuo kinakupa 25% tuu ya maarifa, shughulika kupata mengine kabla hujatoka uanze kukataliwa kila mahali.

  • Jiunge na online communities za Tech, mfano mzuri ni GitHub huko unaweza changia hata open source software na zaidi...na mengine mengi.