Anti-Virus ni programu ambayo hutumika kuilinda kompyuta, kutoka kwa mashambulizi ya virusi ambavyo huathiri mifumo yake na uwezo wake wa kiutendaji kazi.


Jinsi Anti-virus inavyofanya kazi.
kama bodyguard anavyomlinda mtu, basi na anti-virus hulinda kompyuta kwa staili hiyo. Yenyewe huhakiki na kupitia kila kinachofanywa na kompyuta ili kuweza kujua kama kitakuwa na madhara au la!
Mfano:
Unapoingiza tuu flash yako kwenye kompyuta kabla hata hujaifungua anti virus ni ya kwanza kuleta warning kama kuna kirusi au la kwa sababu imeshaipitia kabla.


Tatizo lilipo:
Kutokana na kitendo hicho processor ya kompyuta hufanya kazi mara mbili zaidi kwa kila kitendo kinachofanyika, ya kwanza ikiwa ni kazi ya Anti virus(ukaguzi) na ya pili ikiwa ni kazi ya Operating system(windows) ya kumhudumia mtumiaji matakwa yake.
kwa hali hiyo anti virus kubwa zenye nguvu kama karspesky, avg, avast huhitaji uwezo mkubwa zaidi wa ukokotoaji ili ziweze kufanya kazi na kompyuta na endapo uwezo wa kompyuta ni mdogo, hapo husababisha kompyuta kufanya kazi kwa utaratibu na hata husababisha ukwamaji(stucking) wa kompyuta ikiwa inafanya kazi mara kwa mara.


Ushauri.
kwa matumizi ya sasa unashauriwa kuongeza uwezo wako wa kompyuta mpaka kufikia RAM=4GB na zaidi muone mtaalamu wa tehama ili aweze kukusaidia kusimamia matumizi mazuri ya diski yako inayobeba Operating system iwe na nafasi ya kutosha.

Je ni nani mwenye kiwanda hichi? na ni kwa nini Rwanda, je kompyuta hizi zina uwezo gani?

Soma zaidi.. Rwanda ni kati ya nchi zinazokua kiuchumi kwa kasi hapa katika Afrika Mashariki na miaka ya hivi karibuni imeanzisha utengenezwaji wa kompyuta, kwa kusaini mkataba na kuiruhusu kampuni ya POSITIVO BGH kuweza kuanza utengenezaji wa kompyuta nchini mwake.

POSITIVO BGH  ni muunganiko wa kampuni 2 kubwa, kutoka Amerika ya kusini, ambazo ni POSITIVO yenye makao yako nchini Brazil na BGH yenye makao yake Argentina, kampuni zilianza tangia muda kufanya biashara kwa kuungana na katika moja ya mipango yake ziliamua kuanzisha kiwanda Afrika ili kupanua soko lake.

Kwa nini Rwanda?
Kutokana na maelezo ya Juan Ponelli, Rais wa POSITIVO Afrika, Rwanda imeonesha juhudi kubwa za kusaka maendeleo na pia ina GDP nzuri ya 8.8% ukilinganisha na nchi nyingine hapa Afrika na pia ina utulivu wa kutosha...soma zaidi

Hii ni mojawapo ya kompyuta zinazotengenezwa..

Positivo BGH 11CLE2-R

Specifications
OS: Windows 8.1 Pro
Processor: Intel® Celeron® N2840
Platform: Bay Trail
RAM Memory: 2 GB
Storage: 320 GB
Screen: 11,6"
Camera: 1 Mpx HD
Video: Intel® HD Graphics; DirectX 11
Audio: High Definition
Ports: VGA y HDMI
Memory Reader: 9-in-1 memory multi reader
Security: Kensington port


Kompyuta ni kama yalivyo magari, yanatembea na ya na kimbi lakini yanatofautiana na yana hadhi na uwezo tofauti kulingana na mtengenezaji.
Kwanza nakupa aina ya kompyuta pamoja na matumizi yanayofaa zaidi.
LAPTOP VS DESKTOP
  • Unashauriwa kutumia desktop maofisini kwa sababu zifuatazo za kiulinzi na za kiusalama, kwani ni rahisi kwa laptop kuibwa na nyaraka nyingi kupotea au kuibiwa kuliko desktop, na pia kompyuta ya desktop  ina uwezo mkubwa sana ukilinganisha na kompyuta ya laptop.
  • Unashauriwa kutumia laptop kama ni mfanyabiashara au mwanafunzi,kwa sababu ya wewe kuhitajika kutembea mara kwa mara na kompyuta yako ila inakupasa kuwa na desktop au external hard drive,  mahali ili kuweza kuwa na back up ya data zako.
MAKAMPUNI YA KOMPYUTA NA SIFA ZAKE
HP
Kompyuta hizi zina uimara mkubwa sana na hudumu kwa muda mrefu sana,pia zina hali ya juu ya utendaji na mara nyingi hutumiwa kwakazi zinazohitaji ukokotoaji mkubwa. Pia hutumika katika kwenye tasnia ya uhandisi na hata designing.

DELL
 Kompyuta hizi zina sifa ya ubora sana zaidi husifika kwa kioo(monitor) chake kizuri sana cha HD(High definition) ambacho ni kizuri kuliko vya computer nyingine.

Kompyuta hizi hutumika sana maofisini na hata kwa kujiliwaza kwa kuangalia videos kutokana na ubora wa kioo chake.

LENOVO
Kompyuta hizi zinasifika kwa kuishi kwa muda mrefu kama ikitumika kwa matumizi ya kawaida, yaani yasiyo hitaji ukokotoaji wa hali ya juu.,kama kuangalia movies sana na kucheza michezo kama fifa, magari.

APPLE
Kompyuta hizi zina ubora wa hali ya juu pamoja na uwezo mkubwa sana na pia hudumu kwa muda mrefu. Katika USALAMA haziingiwi na virus kama kompyuta nyingine na ikitokea vimeingia ni mara chache sana. UTENDAJI wake ni mkubwa maana zina nguvu kubwa za ukokotoaji. Pia ni rahisi kubeba kwa maana ni nyembamba na nyepesi kubeba, na zaidi hutumika zaidi kufanya Graphics Design.

MUHIMU 
Nimejaribu kukupa mwanga kuhusu makampuni haya, haimaanishi mapungufu haya utayakuta katika kompyuta zao zote, kwa maana hushughulika kila siku kuweza kurekebisha mapungufu hayo. Ni bora kununua kompyuta za toleo jipya kuweza kuepukana na shida zozote..


 



Unatafuta kununua laptop Dar es Salaam lakini hujui uanze wapi? Soko la Dar lina laptop mpya, refurbished na mitumba — lakini bila mwongozo sahihi unaweza kupoteza hela au kununua laptop isiyofaa mahitaji yako.

Huu ni mwongozo kamili wa kukusaidia kununua laptop bora kulingana na matumizi yako.


Laptop Bora kwa Wanafunzi na Matumizi ya Ofisini

Kwa matumizi ya kawaida kama Microsoft Office, internet, online classes na software za ofisini, chagua laptop yenye:

  • 8GB RAM minimum

  • Intel Core i3 11th Gen au Ryzen 3 (au zaidi)

  • SSD 512GB(ili upate nafasi ya kuhifadhi vitu vyako, MUHIMU SANA)

  • 64-bit system

Hii ni laptop nzuri kwa wanafunzi wa vyuo, wafanyakazi na biashara ndogo.


Laptop Bora kwa Graphic Design na Gaming Dar es Salaam

Kwa kazi nzito kama video editing, graphic design au gaming, tafuta laptop yenye:

  • 16GB – 32GB RAM

  • Intel Core i5/i7 12th Gen au Ryzen 5/7

  • Graphics card ya NVIDIA GTX/RTX

  • SSD 512GB au 1TB

Hizi ndizo laptop zinazofaa kwa wabunifu na content creators.


Tofauti ya SSD na HDD Drives.

Laptop yenye SSD ina speed sana kuliko HDD, ila SSD ina gharama kubwa hivyo ni rahsi wauzaji kukuuzia space ndgo kama 256GB ambayo baadaye itakuja kuleta shida kwenye performance utakapoanza kuhifadhi vitu vyako na software nyingine.


Ukiona laptop bei ndogo sana lakini ina HDD, fahamu performance itakuwa polepole.


Jinsi ya Kuthibitisha Specs za Laptop

Washa laptop → Right-click This PC → Properties
Angalia RAM, Processor na System type.

Usikubali kununua laptop bila kuthibitisha specs mwenyewe.


Je, Ununue Laptop Mpya au Refurbished Dar es Salaam?

Laptop refurbished inaweza kuwa nzuri kama:

  • Ina warranty

  • Battery iko sawa

  • Haina cracks

Lakini bei lazima iwe chini ya mpya.


Hitimisho

Kununua laptop Dar es Salaam siyo suala la bahati — ni suala la maarifa.

Chagua laptop kulingana na matumizi yako, hakikisha ina SSD, thibitisha specs na nunua sehemu yenye warranty.

Ukifanya hivi, utaepuka hasara na kupata thamani ya pesa yako.


Imeandaliwa na 
Elisante Shibanda.
 
Usipate tabu tena, jifunze computer kwa lugha ya asili yako,lugha unayoielewa, Lugha ya Kiswahili.
Hii ni zawadi kutoka ECL Computer Clinic bure kabisa na wewe ufahamu kutumia computer. Furahia zawadi hii.Soma Kitabu hapa

Nini Maana ya software/program za wizi?
Hizi ni software za computer ambazo hazijapatikana kufuata utaratibu uliowekwa na mtengenezaji wa software hizo.

Njia za kupata software hizi.
  • kuwekewa na mtu asiyeaminika bila kununua kwa pesa halali software hiyo.
  • Kushusha/download programu hiyo  kutoka kwenyesehemu isiyoaminika kwenye Programu  internet.
Madhara
  1. Programu hiyo inaweza kufanya kazi kwa kiwango kidogo kuliko kilichokusudiwa na mtengenezaji kwa sababu ya kuharibiwa ili iweze kuruhusu watu wengi kutumia bila kununua.
  2. Programu hiyo mara nyingi huweza kuingia na virus kutoka kwenye internet na kuharibu computer yako.
  3. wewe unaye download hizi programu za wizi unaweza kugundulika na kukamatwa hata kufungiwa vitu vyako kwenye internet na watu wenye mamlaka husika, mfano kwenye nchi kama Uingereza unaweza kukamatwa pale pale ulipo pindi unaanza kudownload programu hiyo ya wizi. Adhabu ni faini ya pesa nyingi au kifungo.
  4. Programu hizi kutokana na kuharibiwa kwenye mfumo wake ili isidai uhalali wa mtumiaji huwez kuharibika/ crashing muda wowote na kupotea na data/taarifa zako zote muhimu.
  5. Unasaidia kuchochea uharibifu wa mali za watu kwa ujumla.

Ushauri.
Ni muhimu sana kununua programu/software kwa usalama wako binafsi na mali zako na pia kwa maadili mema.
ECL Computer Clinic Advice.




The greatest capital that a professional have is knowledge.

Here are some tips about Professionals
1.      A professional finds his profession in everywhere he goes, actually a professional finds his life in his profession.
2.      A Professional is being developed through a process of learning but not studying.
3.      A University Graduate in not necessarily a professional as the same as a college degree to renounce you as a professional.
4.      Difference between university level and secondary school level is in the way of getting knowledge as “Secondary school requires a student to study mostly but the university level requires a student to learn 100% of the time”.
5.      A college is a ground to develop visions, plans and ways of how to incorporate your professional knowledge into them.
6.      Always measure, refine your knowledge to fit the current professional environment.
7.      Sometimes the knowledge provided by the university may be old and outdated but it is there to teach the foundation of the current application of it.












Differences in lifestyle between normal graduate and a professional graduate both while in College.


Graduate
Professional Graduate
He is much concerned with test scores and GPAs rather than profession.
He is much concerned with profession rather than GPAs and test scores.


He is waiting for the last year to graduate so that people can call him a professional.
He constantly check himself to see what he is gaining and how can he survive with what he have already


He mix a lot with civilians or other students to the point of losing sight in his studies.
He dedicate more of his time to understand more about the profession.


He jokes a lot about the course and keep complaining about how hard the course is.
He takes the hardships of the course as the challenge to master it.


He don’t have his vision rested in hic course or he don’t check the importance of course in accomplishing his vision.
He build his vision in relation to his course

There is extra price to pay, if a student want to become a professional graduate, to become a professional graduate;

·        You need to be updated all the time in the internet reading and exploring the world of your profession.

·        You need to do researches (personal) on your society and how you can apply what you have.

·        You need to dedicate twice the amount of time that the others are dedicating in the course, be a champion pay the price.

·        You need to respect the college and all its staffs so that you don’t waste time fighting with them and keeping you pre occupied with supplementary.

·        You need God to make it to professionalism and mostly your professionalism to be important in your life…and because other features of professionalism are related to godliness i.e. truthful, hardworking.

·        You need to quit too much fooling around with friends and groups and concentrate on yourself and the course.

·        You need to eat well and do exercises so that you can be creative.

“A professional must be creative”


“Creativity lives and dwells in a refreshed mind”


“You need discipline to become a good professional, the right kind of discipline is found in God, all things money, wealth are temporary and cannot satisfy you, even if you have billions still you won’t be satisfied, because things that satisfy us are priceless and  can only  be provided by God, without being satisfied by God, you will try to find satisfaction in more wealth and that will corrupt you and soon you will fall.”


“A good professional is temperate in all things”


By Elisante shibanda.





Hakiki Muonekano wa computer wa njee ukikagua kwa makini michubuko na mipasuko maana inaweza leta shida baadaye.


Washa hiyo computer na iwake hadi mwisho usinunue computer ambayo haiwaki kwa kigezo cha kuaminiana.

Hakiki screen yako, mara kadhaa computer huwa zinauzwa na screen ambazo zinakwenda kuharibika, cheki katika screen yako kama kuna mistari yeyote ambayo haibadiliki na vile ambavyo vinaendelea ndani ya computer.
            
                        


Baada ya computer kuwaka hakiki ukubwa wa hard drive/harddisk/ storage au uhifadhi wa computer kama ndio ule ule ambao umetajiwa.

Hakiki speed ya computer kwa kufungua vitu mbalimbali kama speed ya kucheza videos na hata kufunga na kufungua mafaili au fata maelekezo ambayo umeonyeshwa hapo chini, speed  yenyewe hupimwa katika MB(megabyte) na GB(Gigabyte) .
Hakiki uwezo wa kuingiza charge na muda wa kukaa na charge kwa kukubaliana na muuzaji jinsi ya kutambua muda huo udanganywe kwa jinsi computer ilivyoandika katika tab area...