Rekebisha haya ili CV yako in'gae na upate kuitwa kwenye interviews/usaili.
Daftari/kitabu
Usiandike kitabu na experience ya kuandika huna, acha iwe page 1 au 2 tuu inatosha, kwa nini? Mfano wewe ndio afisa rasilimali watu ina CV 300 mezani utasoma CV ndefu?
Usiandike majukumu yako uliyokuwa unafanya awali.
Yeah naona kuna mtu alikuwa anakula baada ya kusoma hiyo anatafuna taratibu sasa, NDIO andika mafanikio na sio majukumu, mfano wewe ni mwalimu usiandike nilikuwa nafundisha, natunga mitihani, na kusahihisha instead andika nimefanikiwa kufundisha wanafunzi 500 geography na katika hao walifaulu 400, rafiki unaitwa haraaakaaa kuanza kazi.
kuweka vipengelea ambavyo havihusiani na kazi unayoitiwa.
CV sio ukishatengeneza basi ndio imetoka hapana, ukiitwa kwenye kazi ya jamii CV yako ioneshe sehemu ulijitolea hata kwenye vikundi vya dini, kuonyesha uongozi, ila ukiitwa kazi ya ofisini, toa vipengele vya vikundi vya kijamii unavyojitolea maana utaonekana uko busy na kazi yao unaweza lipua au ukawa na visingizio vingi vya kutoka kazini.
Hobbies
Kama bado unaweka hizi acha huu uhuni.
Referees.
Usiweke mtu ambaye hajawahi kuwa supervisor wako au boss wako, kama unatoka chuo si ulienda field? kawatafute huko, na utafute lecturer hata mmoja, chondechonde usimuweke ndugu yako.
BONUS
Hebu nenda katafute muundo mzuri wa CV mambo ya CV Kuonekana kama CV ya Chifu Mashuposhupo acha...tembelea cvmkr.com itakusaidia.
Kwa ushauri na mawasiliano tembelea rainstech.com wasiliana nasi kupitia live chats
Ili uweze kufanya kazi mtandaoni unahitaji kuwa na ujuzi ambao mtu anaweza kuutumia ujuzi wako bila kuonana na wewe, na pia uwe na ujuzi wa lugha ya kiingereza vizuri ikiwezekana na lugha nyingine kubwa kama kifaransa.
Na hapo ndio unaona ujuzi wa IT huongoza katika hili lakini pia hata secretarial ila hizi kuna program nyingi ambazo zinafanya kazi zaidi ya secretary.
ujuzi au skills ambazo huhitajika mara kwa mara na watu haujiriwa na kulipwa mtandaoni ni kama ziifuatazo:
Advanced microsoft office Skills( Excel, Word, Powerpoint, access)
Application development(Android, IOS, web applications)
Web design
Graphics Design( artworks, branding, video editing, adverts etc)
Mitandao inayotoa ajira hizi, inahitaji vitambulisho na sometimes ukitaka kuwa member basi utagharamia membership kama 10 dollars inategemea ila huwa ni bure, na katika kila malipo yako utakwatwa hela hapo.
na mingineyo ila hiyo ndio naona vijana wa Tanzania hapa hapa wanalipwa hela.
.
IT(Information Technology) ni kozi nzuri sana kwa vijana na pia ni mojawapo ya sekta ambayo makampuni yaliyowekeza humo yanatengeneza pesa nyingi sana.
Na tunapokwenda IT Imekuwa ikifuta nafasi za kazi nyingi sana kwa kompyuta kuzifanya hizo kazi, mfano;
Assembly line & factory workers
Phone Operators and receptionists
Cashiers
Bank tellers and clerks
Pilots
Journalists and reporters
Stock traders
Postal workers
Travel agents
Accountants
Na kadhalika ni kazi nyingi zinapotea,hatuwezi maliza ila pia IT inatengeneza ajira zake nyingi sana, nyingine hazihitaji hata uajiriwe na mtu.
NJIA YA SHULE KUPITIA ADVANCE HIGH SCHOOL
Kuanza kama ni mwanafunzi wa sekondari hakikisha unasoma masomo ya science na biashara na uendelee advance na masomo hayo hlafu ukifika chuo chagua kozi za IT.
NJIA YA SHULE KUPITIA CHUO
Soma mpaka form four masomo ya science na biashara, halafu chukua certificate ya IT, halafu diploma halafu degree. Vyuo bora ni University of Dodoma, St.Joseph University in Tanzania, Dar es salaam Institute of Technology,College of Information and Communication Technologies (CoICT) - University of Dar es salaam na University of Dar es salaam Computing centre.
NJIA YA KUTOKEA CHUO NA KUENDELEA.
Soma kozi yeyote halafu ukimaliza unaweza nenda kwenye vyuo vya IT, kama unaweza soma degree nyingine ya IT au nenda kwenye vyuo vinavyotoa ujuzi wa IT na ujifunze unaotaka.
Mfano Degree ya Uchumi ila unapenda IT. basi nenda kwenye chuo kinachotoa IT, tafuta Ujuzi unaoutaka mfano:
Application Development
Networking(Inategemea vigezo)
Cyber security(Inategemea vigezo)
Computer TIA
Web development
Graphics Design.
Accounting package Training.
Halafu tafuta college inayotoa ujuzi husika katika vyuo nilivyoviorodhosha hapo juu.
Mara nyingi kozi nyingine hapo huwa hazifundiswi mavyuoni mfano cyber security au App development kwa hizi kozi inabidi ufanye paid online training katika mitandao kama Udemy, Tutsplus etc.
NJIA YA BURE
Kama unapenda IT na hauna hela zaidi ya hela ya bundle, basi chagua kozi unayotaka kusoma, halafu nenda kwa wanao download movies mtandaoni waambia wakusaidie kukutafutia hizo online courses then wakuwekee kwenye hard drive ili ukajifunze wemyewe privately, na watu wengi wamejifunza kwa njia hii, ila hautapata cheti chochote zaidi ya ujuzi.
Tehama(Information technology) Katika nchi za chini ya jangwa la Sahara, Afrika Mashariki bado ni changa sana. Na kama inavyofahamika teknolojia hurahisisha sana maisha na hupunguza mzigo mkubwa wa kazi kwa watu.
Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa
Price: 300,000Tsh
Training: MAXPO training
Bei: 400,000/-Tsh
Pamoja computer networks.
Vigezo: Yeyote
Bei: 250,000/-Tsh
Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa
Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa
Interview za mchujo ni interview za awali, ambazo hutumika kupunguza watu wengi walioomba kazi husika,
ili wabaki wachache kwa ajili ya hatua ya pili ya interview(usaili).
Interview hizi zina sifa kubwa sana ya kuvunja mioyo ya watu walioomba kazi, kwa watu wengi hujikuta wamejiandaa visivyo na kufanya vibaya.
Hebu kwanza tufahamu mambo ya kuzingatia unavyojiandaa na interview.
Muombe Mungu akusaidie kujibu kwa ufasaha, maana ni rahisi sana kujibu visivyo, pamoja ya kuwa unajua kila kitu.
kozi za IT Tanzania na Soko lake
MIUNDO YA MASWALI YA INTERVIEW(USAILI)
Muundo wa 1
Muundo wa 2
Muundo wa 3
Muundo wa 4
Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa
Imekuwa ni jambo la kawaida huku mavyuoni kutenganisha ajira na masomo,
haswa katika vyuo vyetu hapa Tanzania,
kiasi ambacho tumekuwa na tatizo kubwa la ukosefu wa ajira,
ambalo ukilatazama kwa umakini kuna uwezo fulani wahitimu wanakosa ndio maana, tatizo linakuwa kubwa mno.
Lakini pia kuna sababu za msingi tuu ambazo ni za kiuchumi ambazo hata wahitimu hawahusiki ambazo zinakuza tatizo hili.
Kwa upande wa Information Technology na kozi zote zinazoendana na hiyo kozi,
kuna vitu vifuatavyo ambavyo mwanafunzi akivifanya vinaweza fungua njia au
kupanua wigo wako wa ajira kwa kiasi kikubwa sana.
GPA/ UFAULU CHUONI
Huu ni ufaulu wako chuoni, najua ninavyozungumza hivi kwa wingine ni kama kuwaambia wanywe maji ya sumu, ila ndugu zangu hakuna jinsi,GPA ina faida kwanza GPA kubwa inachangia kwa kiasi kukuitisha katika interview ya kazi,
kwa maana inaonesha una uelewa mkubwa na inaonesha kwa kiasi unaweza chapa kazi,
kama ulisoma kwa bidii kwa kiasi hicho basi unaweza ukawa na bidii hata kazini.
Lakini pia mavyuoni tunahitaji wahadhiri na kigezo kikubwa ni GPA ndio utaitwa kwenye interview za huko na hata watu wanaoomba ni wachache sana.
GPA nzuri huanzia 3.5 na kuendelea ila vyuoni ajira zake inategemea huwa inaweza anzia 3.5 wakati mwingine 3.8.
PROFESSIONAL CERTIFICATIONS/ VYETI VYA UTAALAMU.
Hivi ni vyeti vya kitaalamu yaani kubobea katika sehemu fulani,hivi havikupi degree au diploma, ila inapewa hadhi ya kuwa mtaalamu katika eneo moja tuu la IT mablo linaweza likawa sio kubwa.
Mfano
ukitaka kubobea kwenye networking lazima upitie CCNA Certifications, MCSA na kadhalika.
Katika kazi kama za System Administrator bila vyeti kama hivi kuapply ni kazi bure na hata kama ukiitwa mitihani inaweza kukushinda kwa ugumu wake.
SKILLS/UJUZI BINAFSI
Katika maswala ya IT, swali halipo sana unamefundishwa niniila lipo katika unaweza kufanya nini
na unajua nini?
Hakuna muda mzuri wa kujifunza lugha mbali mbali za computer
na kujua jinsi ya kuzitumia kama muda huo,
maana kuna kujiajiri kwingi sana huko na hata serikali na mashirika,
yanatafuta watu wa kutengeneza software mbali mbali.
Mfano wa lugha za kujifunza ni Android, Java, HTML, PHP,Javascript, CSS, Ruby, Python N.K.
Na pia uwezo binafsi wa kutengeneza programs peke yako, websites, blogs N.K
PUBLIC WORKING PROJECTS/Project ambazo umefanya na bado zinafanya kazi.
Tofauti ya elimu ya vyuo vyetu na vyuo vya njee,ni kwamba mkazo uliokuwepo upo kwenye projects au practical,
ni mkubwa sana ukilinganisha na hapa ambao upo kwenye nadharia zaidi.
Kwa hiyo hakikisha projects unayofanya inatatua matatizo ya jamii.
Hiyo hata kwenye interview sehemu ya projects inaweza mvutia HR kukuita.
IMPORTANT INTERNSHIP EXPERIENCE/MAFUNZO YA VITENDO YENYE TIJA.
Unapofika muda wa kutafuta field usifanye mzaha, tafuta makampuni ya kiteknolojia, ili ijifunze jinsi yanavyofanya kazi na hata kupata kazi kwenye makampuni mengine itakuwa rahisi kwa maana mzigo wa kuku train utakuwa umepungua.Hayo ni maeneo muhimu ambayo ukiyashughulikia vizuri hautapoteza muda mwingi kutafuta ajira, kama hali itakuwa shwari ya uchumi.
Kwa ushauri zaidi wasiliana nami,
Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa
elisanteshibanda@yahoo.com
Elimu ya IT hapa Tanzania ni changa sana na imejaa ujuzi mwingi na unahitajika sana katika Taifa hili,
ujuzi wa IT wa ngazi ya chini kabisa, unaweza ukampa mtu uwezo mkubwa tuu wa kujiajiri na
kuendeleza maisha yake.
Zifuatazo ni kozi ambazo zinaweza kumsaidia yeyote kuwa na uwezo wa kujiajiri.
Jinsi ya kufanya kazi na kulipwa mtandaoni ukiwa Tanzania
Course in Graphics Design.
Kozi hii itamuwezesha mwanafunzi kufanya yafuatayo;- Kuchora chochote kwa njia ya kompyuta.
- Kubuni/design magazeti, vitabu,vipeperushi,kalenda n.k
- Kutengeneza matangazo makubwa na madogo kwa ajili ya kuprint au kuweka mtandaoni.
- Kubuni/design business cards, cover letter, cards za mialiko N.K
- Kurekebisha picha zilizopigwa na camera kiustadi zaidi na kuboresha muonekano wake.
Course in Web Design
Kozi hii inajikita katika kuunda tovuti za aina mbali mbali yaani za kibiashara na binafsi, na hii itampa mwanafunzi uwezo kufanya yafuatayo.
- Kuweza kuunda tovuti(website) na kuelewa inayoendana na tovuti.
- Kuipandisha tovuti kwenye mtandao.
- Kuunda tovuti za kisasa kwa njia tofauti.
- kutengeneza mablogu(tovuti ambazo watu wanaweza kuongea humo yaani kuchat mfano hii ni blogu) ya aina zote.
- kusajili tovuti ndani na njee ya nchi.
Course in Computer Administration
- Ujuzi huu utamsaidia mwanafunzi kupata uwezo wa kufanya yafuatayo;
- Kufahamu kompyuta na mifumo inayoendana nayo.
- Kufahamu Computer Hardware, yaani vifaa vyake na jinsi inavyofanya kazi, na hata kujua jinsi ya kuitengeneza pale inapoharibika.
- Kufahamu Computer software, yaani programu za kompyuta na aina zake, jinsi ya kuziweka, kuzitoa na hata kuzishughulikia na kuzitibu pale ambapo zinakuwa hazifanyi kazi vizuri.
- Kufahamu mfumo wa usalama wa kompyuta, jinsi ya kuilinda kompyuta yako na mshambulizi ya kimtandao ya virusi na watu wa njee wanaokuzunguka.
- Kufahamu mifumo ya mawasiliano(Networks) ya kompyuta, jinsi inavyofanya kazi na jinsi ya kuifunga njia ya kuilinda pia.
- Kufahamu jinsi ya kutumia windows 10 na programu nyingine za kuendesha kompyuta mfano windows 8 na Linux.
Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na magroup ya Whatsapp ya MAXPO Tanzania Maximize your potential
Course in Advanced Microsoft Office
Kozi hii inamsaidia mtu kuweza kufanya shughuli zote za kiofisi kwa njia ya kompyuta, kuanzia zile nyepesi mpaka zile ngumu kufanya kwenye kompyuta.
Kozi hutoa uwezo wa kufanya yafuatayo;
Kutumia programu za microsoft office zifuatazo
Microsoft WordMicrosoft Powerpoint
Microsoft Excel
Kwa kiwango cha juu kabisa katika
Kukusanya dataKuchambua data
Kupresent/wasilisha data mbele za watu
Na pia kutengeneza njia za kuingiza data na kutumia microsoft office katika biashara yako yoyote ile
kwa ajili ya kumbu kumbu na hata kuonyesha muelekeo wa biashara, katika mapato na matumizi.
Kumalizia kozi zote hizi hupatikana kwenye vyuo vya kitaalamu yaani Professional colleges ambazo zimejikita tuu katika kozi hizi,
kuchagua chuo chenye uwezo mdgo utakupelekea kupoteza muda wako na kutoka katika kiwango kibaya.
Nakushauri chukua mafunzo ya MAXPO Tanzania, yanatolewa na Kampuni ya Rains Technologies Co LTD iliyopo Ilala, Bungoni Str/Chunya Str Dar es salaam.
na wanakupangia ratiba kulingana na ratiba yako na wana Professional Lecturers wenye uzoefu na pia ni wafanyabishara katika Tehama, kwa hiyo utapata, elimu na ushauri na kusaidiwa jinsi ya kuanza, ila pia kuna vyuo vingine vipo ila sina uhakika na hivyo ila pia ukumbuke jitihada zako binafsi zitakusaidia kupata ujuzi zaidi
Kwa ushauri zaidi wasiliana nami katika
Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na magroup ya Whatsapp ya MAXPO Tanzania Maximize your potential






















