Athari za matangazo kwenye tovuti(website)



Imekuwa ni kawaida kabisa kwa tovuti nyingi hutengenezwa, ili ziweze kuingiza pesa na mojawapo ya njia rahisi ni kuweka matangazo.

Aina ya Matangazo:

  • Matangazo ya baishara nyingine ya moja kwa moja
  • Matangazo ya Google(Google Ads)
Faida ya kuweka matangazo.
Matangazo haya ya moja kwa moja makampuni huweka pesa nyingi sana ili waweze kuwekewa tangazo lao kwa muda maalumu wakati matangazo ya google ads haya google hulipa kiasi kidogo kwa kila mtu anapobofya tangazo lao.

Hasara ya kuweka matangazo.
  1. Inaondoa umakini wa wageni wanaotembelea tovuti yako kwa kuishia kuangalia zaidi matangazo.
  2. Inafanya wageni waondoke haraka, wakati mwingine bila hata kuangalia kilichowaleta kwenye tovuti yako.
  3. Matangazo ya biashara nyingine yanashusha thamani biashara yako, kwa kushindwa kuheshimu kile unachokiuza wewe.
  4. Kwa matangazo ya google kuna wakati unaweza wekewa matangazo ambayo hayaendani na biashara yako na kuishia kuwakwaza wageni wako na wasirudi tena. Mfano mzuri ni tovuti ya dini inaweza wekewa matangazo ya udaku.
Ushauri.
  • Kwa tovuti za makampuni binafsi makubwa au hata makampuni yanayojiweza vizuri si vyema kabisa kuweka matangazo.

  • Kwa makampuni ya habari na mitandao ya kijamii ambapo watu huenda kuenjoy, unaweza weka matangazo
Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   


0 comments:

Post a Comment