Tehama na Mabadiliko yasiyobisha hodi


Tehama inaleta mabadiliko makubwa sana katika ulimwengu wetu tena kwa kasi kubwa mno, kasi hii ina pande mbili  yaani nzuri na upande mwingine ni hatari. Katika uzuri wake ni kweli mtumiaji wa mwisho hupata urahishwaji zaidi wa kazi na ubora zaidi ila kasi hii kwa upande wa biashara na wataalamu waliopo ndani inaweza kukuza na hata kuua biashara kwa kuchelewa kidogo.

Yafuatayo ni mambo 5 muhimu kujua kama unataka kuingia katika ulimwengu huu wa tehama kwa njia ya kusoma au kufanya biashara.


  1. Kubali mabadiliko haraka na zaidi jifunze kuendana nayo kwa uharaka huo huo kama yalivyoingia, kwa sababu unavyoyagomea au kuchelewa kubadilika ni kama kuivisha biashara yako kitanzi.
  2. Mfano :
    kampuni ya zamani ya kutengeneza programu za kusafu(browse) mtandao yaani browser inayoitwa Netscape ilikuwa inauza programu zake na kufaidika sana lakini ghafla kampuni ya Microsoft iliamua kutengeneza na kugawa bure browsers hali iliyopelekea kampuni ya Netscape kwenda mahakamani kuizuia kampuni ya Microsoft ila haikufanikiwa ilikufa baadaye kwa kukataa mabadiliko.
     2. Uwe mtu wa kupenda kujifunza sana kupitia mtandao wa internet na mara kwa mara kuangalia            teknolojia mpya ili usije ukashtuliwa na kuingia kwa teknolojia mpya.
    
    3. Weka maono makubwa na ya mbali yanayoendana na eneo husika na ukuaji wake wa teknolojia          na pia ukilinganisha na ukuaji wa teknolojia hiyo duniani.
       Mfano: unapofungua Internet cafe sehemu nyingine hazihitaji kabisa hiyo huduma kwa sababu             ya jamii husika ina kipato kikubwa na sehemu nyingine inahitaji huduma za printing tuu na              copy, na sehemu nyingine inahitaji zote yaani internet,printing na copy(ila hiyo sio investment               pekee).
        
     4.Kwa Wanafunzi
   Wanafunzi wa ulimwengu huu wa tehama wana kazi mbili ya kwanza ni upokea kinachotoka               chuoni na ya pili ni kuupdate kile kinachotoka chuoni kwa sababu teknolojia hukua kwa kasi na        hata ikibadilishwa mitaara kwa kasi kiasi gani vyuo havitaweza kuendana na kasi hiyo na hata           kuwafanya wanafunzi kupoteza kufahamu misingi ya teknolojia kwa uzuri zaidi.

    5.Kutokana na kubadilika badilika kwa sekta hii inakupasa kuweza kujua kiwango cha mabadiliko ndani ya sekta hii . Mfano biashara ya kuuza simu ina kiwango kikubwa sana cha mabadiliko(simu hupitwa na wakati kwa haraka zaidi ya laptop) ukilinganisha na biashara ya kuuza kompyuta pakato(Laptop) ila zote zinabadilika.

    6.Onana na wafanyabiashara husika na pia IT Professionals au IT Consultants maana wao hujua soko lipoje na faida ipoje katika maeneo mengi ya ICT na kitu cha kuwekeza kwa sasa na kwa njia gani utaanza kuwekeza.

  Kwa ushauri zaidi wasiliana nasi!


0 comments:

Post a Comment