Kwa nini Degree ya chuo ni Muhimu ukitoa swala la ajira, 2025.

 


Ni kweli unaweza kujifunza IT, mtandaoni kila kitu kuanzia soft eng, network(in part), database etc na ukawa mzuri sana, na ukavuna pesa nyingi sana bila kutia mguu chuoni. Kama lengo lako ni kupata pesa tuu, usiende chuo, ila kama una malengo makubwa zaidi, chuo ni lazima kwa sababu zifuatazo;

Ufahamu ( Mindset)

Kuna tofauti kubwa sana, kati ya mtu aliyeenda chuo na asiyeenda chuo katika kujiamini, kujitambulisha na jinsi ya kuwaza, chuo hakikupi tuu maarifa, kinakugeuza na kukufanya uwe msomi na ujiamini unaposimama kati kati ya jumuia yeyote ile Duniani ya wasomi na wakuu wote wale.

Sifa (Credentials)

Nilipokuwa nafungua kampuni yangu ya IT, niliulizwa na BRELA kuhusu vigezo vya mimi kuendesha kampuni ya IT, nilivyoweka tuu vyeti vyangu vya IT, utaratibu ukaendelea na maswali yakakata, lakini pia tunapochukua Project ya mamilioni ya pesa ya TECH, wawekezaji hupenda pia kuangalia sifa za hao watu wanaotoa pesa zao, kama hauna cheti chochote itakuwia vigumu sana kupata mikataba mikubwa labda uwe na coonections za kutisha.

Ulimwengu wa kimataifa.

degree ni lugha ya kimataifa unaposimama marekani, songea, lilongwe, Pretoria kote huko ukisema mimi ni degree holder wa IT wanakusikiliza na unaweza pata kazi au contract ila ukisema mimi najua tuu haya mambo, inakuwa ngumu sana, labda mpka waone project ulizofanya, na proof ndio wakiuamini, na pia nilishwahi kushiriki mashindano ya kimataifa, confidence niliyopata chuo iliniboost sana.

Team (Timu)

Kama una maono makubwa ya kufanya jambo kubwa, au project kubwa unahitaji Team, kukusanya mtaaani hii timu haiwezekani, unahitaji mazingira ya chuo maana huko kuna talent za kila aina magenious, mainfluencers, wachumi yaani watu wenye uwezo tofauti wa kukusaidia kujenga team bora.

Connection

Mavyuo huwa yana mchanganyiko wa watu wengi ambao wana connection nyingi sana, mfano maproffesors, wafanyabishara wakubwa, mameneja lakni pia huanda events nyingi sana za kuwakutanisha waajiri na wanafunzi, na nirahsi hata kuishia kupata kazi sehemu kwa field uliyofanya ambayo ulipelekwa na chuo.

Kazi

la mwisho bila cheti kupata kazi ni issue, serikalini itakuwa ndio bye bye, na pia hata kama hutaki kuajiliwa kwa uzoefu kuna wakati nilikuwa nafanya shughuli zangu, ila kuna wakati nikachukua kazi kujaziliza mapato yangu, yaani ni cheti ni back up nzuri sana kwenye maisha.

**Tahadhari**

Huko kuna ma motivational speakers wanasema matajiri wa Tech wengi hawana cheti hawajaenda chuo, ndgu ni waongo walivyofanikiwa wote walirudi kusoma chuo, ndio uone pesa pekee haitoshi ukiwa na maono makubwa unahitaji elimu ya chuo, ila kama hauna hela anza na kujifundisha mwenyewe mtandaoni ukipata pesa za kutosha vyuo vipo.



0 comments:

Post a Comment