Uchanga wa Tehama Tanzania ni sawa na gunia la pesa linalohitaji wabebaji

Tehama(Information technology) Katika nchi za chini ya jangwa la Sahara, Afrika Mashariki bado ni changa sana. Na kama inavyofahamika teknolojia hurahisisha sana maisha na hupunguza mzigo mkubwa wa kazi kwa watu.

GUNIA ZITO.

Nimeifananisha na gunia zito kwa sababu kutengeneza teknolojia mbadala ili kuweza kutatua changamoto katika jamii inahitaji mafunzo, moyo wa kujitoa binafsi na jitihada zaidi.

Lakini pia inahitaji macho ya kuona hizo fursa katika jamii ili uweze kuzifanyia kazi. Watu wengi hukimbilia kazi ambazo hazihitaji sana ubunifu lakini huku ubunifu ndio mahali pake, pindi unapokosa akili za  ubunifu basi utashindwa kufanya lolote katika tehama.

LENYE PESA

Kama nilivyoeleza hapo mwanzo, pindi teknolojia hizi zinapotengenezwa na wataalamu, huingia sokoni na kurahisisha maisha ya wengi.
watu wengi, makampuni mengi na watu wengi yametajirika sana duniani kwa tehama, mfano 

kampuni kubwa zaidi ya Tax duniani haimiliki tax hata moja bali imeunganisha wamiliki wa Tax,
lakini tatizo waliloliona ni shida ya kupata Tax pale ambapo unaihitaji na haupo barabarani. 

UBER  kwa sasa inaingiza mabilioni ya Pesa duniani kote, hata hapa Tanzania zipo programu kama za mpesa, tigopesa zinaingiza pesa nyingi mno, 

zipo programu za vituo vya mafuta kama Petronite

zipo programu za maduka kama duka pro,

na programu za masomo kama thL na kadhalika na kadhalika...

JINSI YA KUWA MMOJAWAPO WA WABEBAJI.

1. Uwe na uwezo kujifunza kwa bidii sana, na kukuballi kutatua changamoto mbali mbali hata zisizolipa kwa muda huo.

2. Chukua masomo ya Tehama kuanzia ngazi mbali mbali kama cheti, diploma au degree.

3. Ikiwa huna vigezo, basi ujue kusoma na kuandika kiingereza vizuri na uwe na moyo wa kishujaa wa kusoma zaidi ya wale wanaosoma darasani ila ni lazima utafanikiwa.

Janga la ukosefu wa ajira haliwezi kuisha kama tutaendelea kusaka watu kutoka njee wafungue makampuni ndio tuajiriwe ila tuu kama sisi wenyewe tutakapoamua kutoka na kugeuza changamoto kuwa mtaji wetu.


Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   
au elisanteshibanda@yahoo.com




0 comments:

Post a Comment