Fahamu sehemu ya kujiendeleza zaidi katika teknolojia (Kitovu cha teknolojia/technology hub) hapa Tanzania.

Fahamu kitovu cha teknolojia( Technology Hub) hapa Tanzania ambacho wanafunzi wa chuo na wataalamu katika nyanja mbali mbali za teknolojia yaani Software developers, Web developers, Electricians, Electronics Engineers and Computer Engineers n.k hukutanika na kuvumbua au kuboresha vitu.

Kitovu cha teknolojia au kwa lugha ya kiingereza technology hub ni sehemu ambazo huanzishwa kwa malengo ya uvumbuzi na utatuzi wa matatizo kwa nji ya teknolojia. 


Kwa Afrika, sehemu hizi zimefikia 314 katika miji 93 katika inchi 42 nchi kama South Afrika ikiwa inaongeza kuwa na vitovu vingi.

Kwa hapa Tanzania, tuna kitovu cha teknolojia kimoja ambacho kinaitwa Buni Hub.

BUNI Hub.
Buni huhusika zaidi na kuwasaidia wanafunzi hata watu wabunifu katika teknolojia kwa kuwapa ushauri(mentoring) na kuwaongoza kupata uwezo wa kufanya ujasiriamali kwa kupitia teknolojia n.k.


BUNI huwa inaendesha semina, mafunzo mafupi mara kwa mara ili kuweza kuwajenga wanachama wake katika uanzishwaji wa project na hata usimamizi wa project hizo za kitaalamu na kuwaongoza waweze kufikia malengo yao.
Kwa maelezo zaidi tembelea tovuti ya BUNI hapa na wasiliana nao kuweza kujiunga. 

MANUFAA YA KUJIUNGA.
Utajenga uwezo wako binafsi katika kubuni mambo mbali mbali ya kiteknolojia.


Utakutanishwa na watu ambao wana mawazo kama yako ambao watakusaidia kusimama vizuri zaidi.

Ni sehemu ambayo inaweza ikawa uwanda wa wewe kuelewa njia ya kupata hata ufadhili wa kazi yako. 

Muhimu zaidi chochote ambacho hutumii kitapotea na kama wewe ni mwanafunzi wa IT,au kozi zozote za science ni muhimu kuwa pamoja na watu ambao wana elimu kama yako ili elimu yako isije ikalala na ukaanza kufakamia fani za watu wengine.

Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   

0 comments:

Post a Comment