Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   


Jinsi ya Kujifunza Web Design and Graphics Design Kwa urahisi. 

Web Design/Development 

Katika mambo ya tovuti au website huwa zinatengenezwa na Lugha mbali mbali za  computer ambazo ni

  1. HTML 
  2. CSS  
  3. JAVASCRIPT 

Hizo ni lugha kuu lakini website za kisasa zinahitaji Lugha zifuatazi ili ziwe nzuri zaidi JQUEERY, PHP na lugha nyingine za database  mfano SQL na uelewa wa kawaida wajinsi  database zinazyofanya kazi na jinsi ya kuziunganisha na tovuti, pindi tu kama tovuti itahitaji kuwa na uwezo wa kusajili watu na kufanya kazi nyingine.

Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   

JINSI YA KUSOMA

 Siku hzi kila kitu kipo kwenye mtandao wa internet, nakushauri tumia zaidi videos uweze kusoma kwa haraka zaidi,jinsi ya kupata elimu hii ingia kwenye mtandao wa youtube na search kwa njia hii… andika web design for beginners, html for beginners ,css for beginners  and  javascript for beginners 
Au
Ili upate vitabu andika google free HTML,CSS and Javascript for beginners .PDF na kila lugha I search kwa kuishia mwisho .PDF na kuanzia na free.

Blogs. 

Blogs ni rahisi kutengeneza unaweza ukatengeneza hata kama huna knowledge ya Code hata moja au hizo programming language.  Kama kawaida nenda youtube andika how to design a blog or blogging for beginners ili uweze kupata knowledge zaidi juu ya hayo mambo.
 Kuna makampuni kadhaa yanayokupa wewe uwezo wewe wakutengeneza blogu nayo ni Blogger na Wordpress na kumbuka blogu unaweza kuifanya ndio ikawa website kabisa ukiisajili kwenye mtandao kwa malipo maalumu. 
Angalizo. 
Ujuzi wa hizo lugha ni muhimu sana maana utakusadia kuweza pia kuikarabati blogu yako kitaalamu zaidi.

Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   

 Graphics Design

Fani hii inaundwa kwa kujifunza program zinafanya kazi ya kutengeneza vitu ambavyo nimevitaja hapo juu.
Graphics Design inahitaji ujifunze program zifuatazo;

  • Adobe Photoshop**)Kwa ajili ya photo digital editing 
  • Adobe Illustrator**) Kwa ajili ya Drawing/digital art creation. 
  • Adobe InDesign**)Kwa ajili ya kutengeneza vitabu, magazeti au hata vipeperushi.  

Jinsi ya kujifunza ni rahisi sana, Tumia Zaidi mtandao wa Youtube.com search ifuatavyo; 

  1. Kujifunza Photoshop**) Adobe photoshop cc for beginners.
  2.  Kujifunza Illustrator**)Adobe Illustrator CC for beginners.
  3. Kujifunza InDesign**)Adobe indesign CC for beginners. 

Program za kuweka, tafuta program zifuatazo; 

  • Adobe photoshop CC au Adobe Photoshop 2017 
  • Adobe Illustrator CC au Adobe Illustrator 2017 
  • Adobe InDesign CC au Adobe InDesign 2017 

Watu wazuri kwenye Youtube wanaitwa tastetusty wako vizuri sana. 

Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   


Imekuwa ni kawaida kabisa kwa tovuti nyingi hutengenezwa, ili ziweze kuingiza pesa na mojawapo ya njia rahisi ni kuweka matangazo.

Aina ya Matangazo:

  • Matangazo ya baishara nyingine ya moja kwa moja
  • Matangazo ya Google(Google Ads)
Faida ya kuweka matangazo.
Matangazo haya ya moja kwa moja makampuni huweka pesa nyingi sana ili waweze kuwekewa tangazo lao kwa muda maalumu wakati matangazo ya google ads haya google hulipa kiasi kidogo kwa kila mtu anapobofya tangazo lao.

Hasara ya kuweka matangazo.
  1. Inaondoa umakini wa wageni wanaotembelea tovuti yako kwa kuishia kuangalia zaidi matangazo.
  2. Inafanya wageni waondoke haraka, wakati mwingine bila hata kuangalia kilichowaleta kwenye tovuti yako.
  3. Matangazo ya biashara nyingine yanashusha thamani biashara yako, kwa kushindwa kuheshimu kile unachokiuza wewe.
  4. Kwa matangazo ya google kuna wakati unaweza wekewa matangazo ambayo hayaendani na biashara yako na kuishia kuwakwaza wageni wako na wasirudi tena. Mfano mzuri ni tovuti ya dini inaweza wekewa matangazo ya udaku.
Ushauri.
  • Kwa tovuti za makampuni binafsi makubwa au hata makampuni yanayojiweza vizuri si vyema kabisa kuweka matangazo.

  • Kwa makampuni ya habari na mitandao ya kijamii ambapo watu huenda kuenjoy, unaweza weka matangazo
Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   




Kuomba kazi ni hatua ya kwanza muhimu sana katika kufikia malengo yako ya kikazi. Hata kama una elimu au ujuzi mzuri, barua ya maombi ya kazi ndiyo inayoamua kama utaitwa kwenye usaili (interview) au la.

Waajiri wengi hupokea maombi mengi sana, hivyo barua yako inapaswa kuwa fupi, wazi, na yenye mvuto.


🎯 Vigezo Vinavyotumika Kukuchagua Kwa Interview

Wakati wa kuchambua waombaji, waajiri huzingatia mambo yafuatayo:

  • Uwezo wa kufanya kazi kwa ubora kuliko wengine
  • Elimu yako
  • Ujuzi wako wa kazi

👉 Lakini kitu cha kwanza wanachokiona ni barua yako ya maombi


✍️ Mambo Muhimu ya Kuzingatia Unapoandika Barua ya Kazi

1. 🙏 Mtangulize Mungu

Anza na Mungu, yeah kuna watu wana connections, wana ushirikina, yaani kila aina ya fujo, ila ukimtanguliza Mungu utapewa kazi hata hao watakaokua wanakupa kazi watajiuliza umefikaje fikaje mpka umepewa kazi, rafiki nimeyaona haya mambo live bila chenga... niamini Mungu atakusaidia.


2. 📝 Tumia Lugha Rahisi

Kama unaandika kwa Kiingereza au Kiswahili:

  • Tumia maneno rahisi
  • Epuka lugha ngumu au ya kitaalamu kupita kiasi
  • Hakikisha hakuna makosa ya tahajia

3. 📌 Eleza Chanzo cha Taarifa (Reference)

Weka wazi ulipopata tangazo la kazi:

  • Website
  • Newspaper
  • Social media

4. 🏢 Taja Jina Halisi la Kampuni

Usiandike:
❌ “Ningependa kufanya kazi kwenye kampuni hii”

Andika:
✔ “Ningependa kufanya kazi Vodacom”


5. 💡 Onyesha Unavutiwa na Kampuni

Waajiri wanapenda watu wanaojua wanachotaka.


6. 🎯 Elewa Malengo ya Kampuni

Onyesha kuwa umefanya utafiti:

  • Kampuni inafanya nini
  • Ungependa kuchangia vipi

7. 💪 Jieleze Kwa Nini Wewe

Taja sababu za kukufanya uwe bora:

  • Ujuzi wako
  • Bidii yako ya kazi
  • Mapenzi yako kwa kazi
  • Malengo yako yanavyolingana na kampuni

8. 📄 Barua Iwe Fupi

  • Usizidishe maelezo
  • Ukurasa mmoja unatosha

9. 🧑‍💼 Jua Unayemwandikia

HR anataka:

  • Uwazi
  • Urahisi
  • Sio maneno magumu sana

10. ✉️ Kwa Posta – Andika Kwa Mkono

Kama unatuma kwa posta:

  • Andika kwa mkono (kama imeombwa)
  • Itaonekana ya kipekee na ya heshima zaidi

📌 Mfano wa Barua ya Kuomba Kazi

Mpendwa [Jina la Mwajiri],

Ninaandika barua hii kuonyesha nia yangu ya kuomba nafasi ya Afisa wa Teknolojia ya Habari (IT) katika [Jina la Kampuni], kama ilivyotangazwa kupitia [chanzo cha tangazo].

Nina uzoefu katika fani ya IT pamoja na ujuzi wa kubuni tovuti na kusimamia mifumo ya teknolojia. Nimewahi kushiriki katika miradi mbalimbali ya IT, ikiwemo kubuni tovuti za mashirika kama The Green Foundation Services – Zanzibar.

Ninavutiwa sana na [Jina la Kampuni] kutokana na mchango wake katika [eleza lengo la kampuni], na ningependa kuwa sehemu ya timu inayosaidia kufanikisha malengo hayo.

Ninaamini ujuzi wangu katika IT, uwezo wa kutatua matatizo, na moyo wa kufanya kazi kwa bidii utanisaidia kuongeza thamani katika taasisi yako.

Asante kwa kuzingatia maombi yangu. Natarajia kupata nafasi ya mahojiano ili kujadili zaidi jinsi ninavyoweza kuchangia katika timu yako.

Wako kwa dhati,
[Jina lako]


💬 Hitimisho

Barua ya maombi ya kazi si maandishi ya kawaida — ni kibali chako cha kwanza kupata interview.

Ukifanya vizuri hapa, tayari umefanya 70% ya kazi ya kupata ajira.




Tovuti(website) ni kurasa za kielectroniki(webpages) zinazohifadhiwa katika kompyuta server ili ziweze kupatikana kwa urahisi pindi zinapohitajika na watumiaji wengine waliopo kokote kule duniani kwa njia ya mtandao wa intaneti.
Mfano wa kurasa maarufu zaidi ni google.com na facebook.com.

Mambo yanayohitajika kuwepo kwenye tovuti.
  • ·         Utangulizi  mfupi wa biashara yako.
  • ·         Bidhaa zinazopatikana na njia ya kuzipata.
  • ·         Ubora wa bidhaa zako.
  • ·         Upekee wako kwenye soko.
  • ·         Mawasiliano ya kufika kwenye biashara yako.
  • ·         Maono ya biashara yako.

Mambo muhimu ya kuzingatia katika tovuti yako.
  1. · Usiweke taarifa nyeti za biashara yako kwenye tovuti maana kila mtu ataona hata adui wataona na watazitumia kukushinda kwenye biashara.

  1. · Usiweke taarifa nyingi kwenye tovuti, Maelezo mengi hayastahili kuwepo kwenye tovuti maana hakuna atakayesoma Maelezo hayo Zaidi yako, weka Maelezo mafupi na yenye kutosheleza.

  1. · Usiweke picha halisi ya eneo lako la biashara kama halina mvuto au ubora mkubwa.

  1. · Usitumie picha ambazo hazina uhalisia kabisa katika biashara yako au eneo ulipo, mfano kuweka wazungu wakati Wateja wako wengi ni weusi.

  1. · Weka taarifa fupi zile tuu zinazomchochea mtu kutaka kujua zaidi ili apige simu na kufika ofisini.

  1. · Fahamu Wateja wako ni watu wa aina gani ili uweze kuongea nao vizuri mfano kama ni Watu wa daraja la kati na chini kwa kipato na ni watanzania Zaidi hapo tumia lugha ya Kiswahili lakini kama watu wako ni watu wenye pesa na wamataifa mengine mengi tumia kiingereza.

  1. · Tumia wataalamu wazuri wa lugha ili kusiwe na makosa ya sarufi katika tovuti maana hufanya biashara yako  ionekana ya uchwara. 
Fuata hayo na mengine mengi kwa ushauri ntumie barua pepe na mimi nitakusaidia.

  



Karibu upate tovuti  na blogu safi kabisa, za kisasa na kwa bei nafuu sana. Kwa mawasiliano zaidi...

Kwa Taarifa, Maswali, fursa mbali mbali za IT hapa Tanzania na Africa Mashariki, pamoja na kozi fupi za ujuzi mbali mbali katika IT(information Technology),jiunge na group la whatsapp la MAXPO Tanzania Maximize your potential Bonyeza hapa   
Sanaa ya Matangazo ni mojawapo ya vitu vinachangia mvuto mkubwa wa bidhaa inayotangazwa, Nini cha kufanya unapohitaji tangazo bora.

Kwanza kabisa onyesha uhalisia kwa kiasi juu ya biashara yako, unapotengeneza tangazo ambalo ni perfect sana, yaani halina uhalisia wa uwezo wako kiasi au uhalisia wa Nchi husika, husababisha watu wakuone wewe ni feki. lakini zaidi la muhimu zingatia ushauri wa mafundi wa sanaa hii.
Mfano mzuri angalia matangazo ya mitandao ya simu, huvutia wengi.

Kwa ushauri na utengenezaji wa matangazo haya karibu uongee nasi.
Vitendo 100%, utajifunza kutoka kwa walimu na Washauri katika sekta hii ya IT, Field Trip kwa makampuni yaliyobobea katika fani hii na zaidi ya yote tuna ratiba zinazojali muda wako.

Karibu katika madarasa yetu hapa  AMD Academy ghorofa ya 19, RITA Towers, karibu na POSTA MPYA(madarasa yenye viyoyozi safi, mwanga safi and muonekano mzuri wa bahari)...Tupigie AMD Academy 0656480666.
Tovuti ama kwa jina la kiingereza(website) imekuwa ni kama mavazi ya biashara katika mtandao wa Internet.

Nimeona Clients wengi wakibadili mawazo kwa kutembelea tovuti ya biashara ya wahusika mara moja, pale wanapokuta tovuti haina ufanisi wa hali ya juu au inachelewa kufunguka au ina muonekano mbaya.
 Siku zote hakikisha tovuti yako ina uwezo mkubwa, inapendeza na kuvutia watu haswa pale inapofunguka kwenye simu za mkononi na imekuwa hosted katika server bora na zenye ufanisi wa hali ya juu kabisa.

ECL Computer Clinic huwa tunachukua hatua za ziada kutafuta server bora duniani na kuhost tovuti za wateja wetu huku tukihakikisha zinapata usajili wa Tanzania na zinakubalika na watu wote na rika lote mfano Apollo Heavy Equipment Limited , Bright Future Academy  and so on.... karibu ufanye kazi nasi.

Ni vyema kupata ushauri wa kitaalamu kabla ya kufanya mabadiliko yeyote yale yanahusiana na teknolojia...

Ni kwa sababu zifuatazo
Usalama
Katika ulimwengu wa leo, kuna wizi mwingi sana katika mitandao haswa katika teknolojia inayohusiana na kompyuta, na hata tuna taarifa ya kwamza hapa Tanzania tupo katika nchi chache duniani ambapo wizi mwingi hutokea.

Mabadiliko ya Teknolojia
Teknolojia hubadilika mara kwa mara, unayotaka kutumia au kununua leo inaweza ikawa ishatoka katika usasa na ni ya zamani na inatakiwa kubadilishwa kutokana na sababu za kiusalama. Kwa hiyo ukajikuta umepoteza pesa zako nyingi.

Sheria na Matakwa ya Nchi Husika
Sio kila teknolojia unaweza kuitumia Tanzania au nchi nyingine na hata kuna njia ya kutengeneza system yeyote ili ikidhi viwango vya nchi husika mfano katika maswala ya usajili wa tovuti kwa Tanzania kuna sheria mahususi ambazo ni za kipekee kabisa hazipo duniani kote.

Kupata Wataalamu Husika
Sio kila aliye kwenye fani hii ni bora na anafaa kutumiwa, wengine wana uwezo tofauti na utawapata kulingana na mfuko wako.