Sanaa ya Matangazo ni mojawapo ya vitu vinachangia mvuto mkubwa wa bidhaa inayotangazwa, Nini cha kufanya unapohitaji tangazo bora.

Kwanza kabisa onyesha uhalisia kwa kiasi juu ya biashara yako, unapotengeneza tangazo ambalo ni perfect sana, yaani halina uhalisia wa uwezo wako kiasi au uhalisia wa Nchi husika, husababisha watu wakuone wewe ni feki. lakini zaidi la muhimu zingatia ushauri wa mafundi wa sanaa hii.
Mfano mzuri angalia matangazo ya mitandao ya simu, huvutia wengi.

Kwa ushauri na utengenezaji wa matangazo haya karibu uongee nasi.
Vitendo 100%, utajifunza kutoka kwa walimu na Washauri katika sekta hii ya IT, Field Trip kwa makampuni yaliyobobea katika fani hii na zaidi ya yote tuna ratiba zinazojali muda wako.

Karibu katika madarasa yetu hapa  AMD Academy ghorofa ya 19, RITA Towers, karibu na POSTA MPYA(madarasa yenye viyoyozi safi, mwanga safi and muonekano mzuri wa bahari)...Tupigie AMD Academy 0656480666.
Tovuti ama kwa jina la kiingereza(website) imekuwa ni kama mavazi ya biashara katika mtandao wa Internet.

Nimeona Clients wengi wakibadili mawazo kwa kutembelea tovuti ya biashara ya wahusika mara moja, pale wanapokuta tovuti haina ufanisi wa hali ya juu au inachelewa kufunguka au ina muonekano mbaya.
 Siku zote hakikisha tovuti yako ina uwezo mkubwa, inapendeza na kuvutia watu haswa pale inapofunguka kwenye simu za mkononi na imekuwa hosted katika server bora na zenye ufanisi wa hali ya juu kabisa.

ECL Computer Clinic huwa tunachukua hatua za ziada kutafuta server bora duniani na kuhost tovuti za wateja wetu huku tukihakikisha zinapata usajili wa Tanzania na zinakubalika na watu wote na rika lote mfano Apollo Heavy Equipment Limited , Bright Future Academy  and so on.... karibu ufanye kazi nasi.

Ni vyema kupata ushauri wa kitaalamu kabla ya kufanya mabadiliko yeyote yale yanahusiana na teknolojia...

Ni kwa sababu zifuatazo
Usalama
Katika ulimwengu wa leo, kuna wizi mwingi sana katika mitandao haswa katika teknolojia inayohusiana na kompyuta, na hata tuna taarifa ya kwamza hapa Tanzania tupo katika nchi chache duniani ambapo wizi mwingi hutokea.

Mabadiliko ya Teknolojia
Teknolojia hubadilika mara kwa mara, unayotaka kutumia au kununua leo inaweza ikawa ishatoka katika usasa na ni ya zamani na inatakiwa kubadilishwa kutokana na sababu za kiusalama. Kwa hiyo ukajikuta umepoteza pesa zako nyingi.

Sheria na Matakwa ya Nchi Husika
Sio kila teknolojia unaweza kuitumia Tanzania au nchi nyingine na hata kuna njia ya kutengeneza system yeyote ili ikidhi viwango vya nchi husika mfano katika maswala ya usajili wa tovuti kwa Tanzania kuna sheria mahususi ambazo ni za kipekee kabisa hazipo duniani kote.

Kupata Wataalamu Husika
Sio kila aliye kwenye fani hii ni bora na anafaa kutumiwa, wengine wana uwezo tofauti na utawapata kulingana na mfuko wako.


Kama kijana mdogo nisiyekuwa na uzoefu  hata kidogo  wala msaada katika biashara, nilijikuta nikiona jinsi gani duka la Mangi lilikuwa likikua kwa kasi, na la kwangu taratibu mno, nilijiuliza maswali mengi lakini kwa sababu Mangi alikuwa mfanyabiashara mwenzangu na rafiki yangu sikusita kumuomba ushauri, na ndipo aliponiambia mambo haya amabyo yalibadilisha biashara yangu na mtazamo wangu katika uwanda huu wa biashara.

MTAJI.

Unapoanzisha biashara na unapokuwa na mtaji wako wa kiasi fulani , unapokuwa ukipata faida . inakupasa ufanye kila liwezekanalo kutogusa FAIDA, sijakosea sio MTAJI pekee bali FAIDA na MTAJI kwa mwaka mzima, hapo ndipo utaona ukuaji wa duka unaostahili..utapata wapi hela ya kula na matumizi mengine we mtu mzima umiza kichwa.

UENDESHAJI

Imezoeleka kuwaweka ndugu na jamaa au hata watu tuu tunaowaajiri kama wauzaji halafu sio tukaendelea na kufanya kazi nyingine.HAYO NI MAKOSA TENA NI MWIKO KUFANYA HIVYO.
Wafanyakazi waajiriwa wengi wameanzisha maduka yamekufa kwa sababu hiyo.
Wanaopaswa kuendesha duka lako ni "WEWE", "MKEO" na "WEWE+MKEO" kama watu hao hawatakuwepo, tafuta shughuli nyingine ya kufanya na hela yako.

MUNGU

Unaweza ukafanya vizuri kote katika hayo niliyoyasema hapo juu, lakini ukweli ni kwamba biashara zimetawaliwa na nguvu za giza sana, ni lazima uchague utakaa upande gani na ukae huko moto  moto na sio robo au nusu, kama ni uchawi ujue ipo siku utakufa na biashara yako itakufa vibaya na utaangamiza watoto na familia yako so nakushauri mtafute Mungu wako.

NIDHAMU

Watu wengi huchukia mabosi, wakiwaona kama wanawanyanyasa wanavyowashurutisha kufanya kazi, yaani wakitunza nidhamu kazini, lakini ukweli ni kwamba biashara inahitaji nidhamu ya hali ya juu mno, isiyosuburi kukumbushwa...mazoea, uchelewaji, kauli chafu,uvivu huua biashara mara moja.

UTU

lazima uwe na utu, ujali wafanyakazi wako, kimahitaji na hata kimahusiano yaani waheshimu, hata kama umewazidi kipato kiasi gani.
"Kumbuka wamiliki wengi wa biashara wameuawa na majambazi kwa mpango uliosukwa na wafanyakazi wao au hata kuporwa mali kutokana na kisasi walichonacho wafanyakazi"

FULL TIME/PART TIME

Biashara sio part time nik full time job kama hauko teyari kuwekeza muda wako wote nenda kanunue hisa wekeza huko maana huko hauhitajiki sana kama una hisa ndogo na hisa zikizidi bado ushauri wangu utaendelea utakabidhiwa ofisi tuu.

Kwa hayo nimeona nikushirikishe wewe ili kama umejipanga kufanya biashara basi uwe makini usije ukapoteza hela zako bure.
Mangi yeye ni mfanyabishara mkubwa wa maduka ya jumla ya vyakula kwa aina nyingine ya biashara tanua fikra zako.

Tehama inaleta mabadiliko makubwa sana katika ulimwengu wetu tena kwa kasi kubwa mno, kasi hii ina pande mbili  yaani nzuri na upande mwingine ni hatari. Katika uzuri wake ni kweli mtumiaji wa mwisho hupata urahishwaji zaidi wa kazi na ubora zaidi ila kasi hii kwa upande wa biashara na wataalamu waliopo ndani inaweza kukuza na hata kuua biashara kwa kuchelewa kidogo.

Yafuatayo ni mambo 5 muhimu kujua kama unataka kuingia katika ulimwengu huu wa tehama kwa njia ya kusoma au kufanya biashara.


  1. Kubali mabadiliko haraka na zaidi jifunze kuendana nayo kwa uharaka huo huo kama yalivyoingia, kwa sababu unavyoyagomea au kuchelewa kubadilika ni kama kuivisha biashara yako kitanzi.
  2. Mfano :
    kampuni ya zamani ya kutengeneza programu za kusafu(browse) mtandao yaani browser inayoitwa Netscape ilikuwa inauza programu zake na kufaidika sana lakini ghafla kampuni ya Microsoft iliamua kutengeneza na kugawa bure browsers hali iliyopelekea kampuni ya Netscape kwenda mahakamani kuizuia kampuni ya Microsoft ila haikufanikiwa ilikufa baadaye kwa kukataa mabadiliko.
     2. Uwe mtu wa kupenda kujifunza sana kupitia mtandao wa internet na mara kwa mara kuangalia            teknolojia mpya ili usije ukashtuliwa na kuingia kwa teknolojia mpya.
    
    3. Weka maono makubwa na ya mbali yanayoendana na eneo husika na ukuaji wake wa teknolojia          na pia ukilinganisha na ukuaji wa teknolojia hiyo duniani.
       Mfano: unapofungua Internet cafe sehemu nyingine hazihitaji kabisa hiyo huduma kwa sababu             ya jamii husika ina kipato kikubwa na sehemu nyingine inahitaji huduma za printing tuu na              copy, na sehemu nyingine inahitaji zote yaani internet,printing na copy(ila hiyo sio investment               pekee).
        
     4.Kwa Wanafunzi
   Wanafunzi wa ulimwengu huu wa tehama wana kazi mbili ya kwanza ni upokea kinachotoka               chuoni na ya pili ni kuupdate kile kinachotoka chuoni kwa sababu teknolojia hukua kwa kasi na        hata ikibadilishwa mitaara kwa kasi kiasi gani vyuo havitaweza kuendana na kasi hiyo na hata           kuwafanya wanafunzi kupoteza kufahamu misingi ya teknolojia kwa uzuri zaidi.

    5.Kutokana na kubadilika badilika kwa sekta hii inakupasa kuweza kujua kiwango cha mabadiliko ndani ya sekta hii . Mfano biashara ya kuuza simu ina kiwango kikubwa sana cha mabadiliko(simu hupitwa na wakati kwa haraka zaidi ya laptop) ukilinganisha na biashara ya kuuza kompyuta pakato(Laptop) ila zote zinabadilika.

    6.Onana na wafanyabiashara husika na pia IT Professionals au IT Consultants maana wao hujua soko lipoje na faida ipoje katika maeneo mengi ya ICT na kitu cha kuwekeza kwa sasa na kwa njia gani utaanza kuwekeza.

  Kwa ushauri zaidi wasiliana nasi!



Kwa miaka tumekua tukiona watu wanaanzisha mablogu kama michuzi, milardayo na wengineo wengi, na tunafurahi maana wanatuletea taarifa nyingi kwa kweli, lakini unajua hawa wanapata hela nyingi ambazo hata wewe unaweza pata!!!

Blogu ni tovuti ambazo zinaruhusu mtumiaji aweze kuhusishwa na kile ambacho kimewekwa kwenye tovuti, kama habari kwa mfano, mtu anaweza iona na kuandika yeye ameiopokeaje na hata kuwasiliana papo na hapo kwa watu wengine kuhusu habari hiyo.

Je kuanzisha biashara hii inagharimu kiasi gani?
Kuanzisha biashara hii inahitaji uwelewa wa utumiaji wa mtandao, inahitaji uwe na internet zaidi ya hapo hakuna gharama nyingine zaidi...Kumbuka: uelewa huu wa mtandao sio wa kwenda chuo ni uelewa mdogo tuu  ambao unaweza kujua ndani ya wiki 2 au moja tuu.

Nini kinahitajika ili kuanzisha biashara hii?
unahitaji kitu cha kuandika, mfano michuzi yeye kaamua kujikita kwenye habari na kwa hilo amewapata wengi ambao wanatembelea kwenye blogu yake...kama hauna fikiri kwanza ni kitu gani  watu gani wanataka.

Unapataje pesa sasa?
Jinsi blogu yako itakavyo vuta watu wengi na kuingia, basi utapata hela kwa njia zifuatazo;

  • Matangazo
Ukitembelea blogu hizi utakuta matangazo kama ya vodacom na makampuni mengine ambayo hulipa mtu anapoclick tuu na hata mtu anapoliona hilo tangazo. Mfano mkikubaliana mtu anapoclick upate Tsh 100 na kuendelea na kwa mwezi labda ulipwe laki 4 ni wewe utachagua na kukubaliana na mwenye tangazo.

  • Pia unaweza uza vitu kama vitabu vya mtandao vyenye mafunzo mbali mbali kwa njia ya sauti au video kwa watu.

  • Unaweza pia ukauza post zako kwa njia ya kuwaweka kampuni kama ndio wamechangia kuileta...mfano: unawe za kwenye TV kipindi cha Tamthilia unasikia tamthilia hii imeletwa kwenu na Wizara ya afya.
Ukweli ni kwamba huku ubunifu wako utakuletea pesa, na kujitoa kwako na ukitaka kujifunza hivi endelea kutembelea hapa na karibuni tutaleta mafunzo haya bure.

Tehama(ICT) na Teknolojia kwa ujumla imeweza kuajiri zaidi ya milioni 6.7 na inawalipa mara 2 zaidi ya sekta nyingine katika Nchi ya Marekani(compIT), lakini kwa hapa Tanzania bado fani hii ina watu wachache sana na ukizingatia vijana wengi wanalalamika ukosefu wa ajira.

Kwa nini ni jawabu mojawapo la Ajira?

  • Mtaji wake ni mdogo sana na ukilinganisha na maeneo mengine ya kuwekeza kama kilimo na sekta nyingine na pia unalenga vijana zaidi ambao ndio wanakumbwa na tatizo hilo la ukosefu wa ajira.
  • Tehama haihitaji mtu aajiriwe ili aweze kujipatia kipato kwenye sekta hii kwa maana hutegemea zaidi ubunifu wa mtu na juhudi zake binafsi na mahali mtu alipo ndio panaweza geuka ofisi.
  • Unaweza ukajifunza tehama bila hata kuingia darasani au kwenda chuoni na ndani ya mwezi ukawa vizuri kabisa.

Ukitaka kujifunza tehema wasiliana nasi tutakupa mwanga katika tasnia hii.



 Programu bora Afrika
   Afrika hatuna haja ya kushindana kugundua teknolojia kama Mataifa mengine kwa maana huko huhitaji pesa nyingi sana, ila tunaloweza kufanya ni kuitumia teknolojia iliyekuwepo na kuiweka katika mazingira ambayo itatusaidia katika maisha, Pongezi ziwaendee hawa wataalamu hawa wa tehama walivyo weza kufanya haya. Angalizo zipo nyingine sokoni pia ila muda unavyozidi kwenda tutazigundua na kuzitangaza ili zifahamike. Tazama hapa

Hebu jaribu kuchukua nafasi ya Human resource manager(Meneja wa rasilimali za binadamu) akiwa amepokea maombi ya watu 5000 kwa ajili ya nafasi moja ya kazi aliyoitangaza, unadhani atapitia na CV yako kwa jinsi ilivyo? 😓

Basi kama unataka kufanya CV yako, ipendeze kimuonekano na hata iweze kumzuia meneja aliyechoka kupitia CV za watu hebu ingia hapa tengeneza akaunti yako bure na fuata maelekezo maana ni rahisi mno kutumia.